Utenzi Mahiri..........Gogo

CAMARADERIE

JF-Expert Member
Mar 3, 2011
4,419
1,920
Kuna gogo la muanga, njiani limeanguka
Waja mafundi kuchonga, kibanzi kutobanjika
Watu wavunjika nyonga, kwa kupanda na kushuka
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala

Waja wenye mbinu zao, hupanda wakadunguka
Waja na wavamiao, kwa papara na haraka
Wako pia waliao, gogo lipo lawacheka
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala

Letu sote gogo hili, kilitaka lakutaka
Afanyae hatambuli, mja huyo asumbuka
Thamani yake ni ghali, wala hili si dhihaka
Kula ajaye na shoka, katu hawi seremala

Hili gogo madhubuti, si rahisi kukatika
Tukishindwa tukaketi, bandu mwisho hubanduka
Tukikosa jizatiti, gogo litaja anguka
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala

Bandu humaliza gogo, hilo sheti kukumbuka
Tusijitie mikogo, kudharau kila shoka
Tusilikimbie zogo, pembeni jema kuweka
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala
 
Lapokuwa gumu gogo, Shoka linapozidiwa,
Lipaswi pewa kisogo, Mbinu mpya hutakiwa,
Kwani gogo la mhogo, lishindwe kupasuliwa?
Seremala mwenye fani, shoka siyo la lazima.

Msumeno ntatumia, gogo kulibanjuani,
Mbele kiushindilia, banzi walitakiani?
Nyuma kiurudishia, gogo lina gumu gani?
Seremala mwenye fani, shoka siyo la lazima.

Shoka kazi yake kuni, Mpishi lampatia,
Kumletea jikoni, kuni za kumpikia,
Zikishapigwa juani, shoka inazipatia,
Seremala mwenye fani, shoka siyo la lazima.
 
Lapokuwa gumu gogo, Shoka linapozidiwa,
Lipaswi pewa kisogo, Mbinu mpya hutakiwa,
Kwani gogo la mhogo, lishindwe kupasuliwa?
Seremala mwenye fani, shoka siyo la lazima.

Msumeno ntatumia, gogo kulibanjuani,
Mbele kiushindilia, banzi walitakiani?
Nyuma kiurudishia, gogo lina gumu gani?
Seremala mwenye fani, shoka siyo la lazima.

Shoka kazi yake kuni, Mpishi lampatia,
Kumletea jikoni, kuni za kumpikia,
Zikishapigwa juani, shoka inazipatia,
Seremala mwenye fani, shoka siyo la lazima.

Swadakta........
 
Kwanza ejaribu Chali, mchanjaji wa Msuka
Kisha akakwea Duli, kwa dhihaka akashuka
Nasabawe Mizamyuli, gogo helitaharuka
Gogo haliebu shoka, li kweche lakwerezuka

Akapanda Sefu Chalyo, baba la miraba nyuka
Akarudi na miyayo, mpwawe Miza mizuka
Alimasi yake yayo, mpini ukapasuka
Gogo haliebu shoka, li kweche lakwerezuka

Seremala hachanjili, apikia kwa nkaa
Nyie mwamleta Chili, mchomaji wa chokaa
Hapa tumtaje Pili, kwa mipingo kachakaa
Gogo haliebu shoka, li kweche lakwerezuka
 
muruwa kabisa enzi za wasomaji mashairi maarufu kina mariam ponda na mzee khalifani wangeghani vizuri
 
Naaam.........Swadakta, ushairi at its best, fani hii ni adimu na si sote wenye uwezo wa kucheza na lugha/ ghani namna hii, Heshima kwako

Kuna gogo la muanga, njiani limeanguka<br />
Waja mafundi kuchonga, kibanzi kutobanjika<br />
Watu wavunjika nyonga, kwa kupanda na kushuka<br />
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala<br />
<br />
Waja wenye mbinu zao, hupanda wakadunguka<br />
Waja na wavamiao, kwa papara na haraka<br />
Wako pia waliao, gogo lipo lawacheka<br />
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala<br />
<br />
Letu sote gogo hili, kilitaka lakutaka<br />
Afanyae hatambuli, mja huyo asumbuka<br />
Thamani yake ni ghali, wala hili si dhihaka<br />
Kula ajaye na shoka, katu hawi seremala<br />
<br />
Hili gogo madhubuti, si rahisi kukatika<br />
Tukishindwa tukaketi, bandu mwisho hubanduka<br />
Tukikosa jizatiti, gogo litaja anguka<br />
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala<br />
<br />
Bandu humaliza gogo, hilo sheti kukumbuka<br />
Tusijitie mikogo, kudharau kila shoka<br />
Tusilikimbie zogo, pembeni jema kuweka<br />
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala
<br />
<br />
 
Naam........Nadiriki kusema nimejifunza na naendelea kujifunza mengi toka ktk tungo zako, sijamuona mwalimu wangu klorokwini, hapiti huku?


Lapokuwa gumu gogo, Shoka linapozidiwa,<br />
Lipaswi pewa kisogo, Mbinu mpya hutakiwa,<br />
Kwani gogo la mhogo, lishindwe kupasuliwa?<br />
Seremala mwenye fani, shoka siyo la lazima.<br />
<br />
Msumeno ntatumia, gogo kulibanjuani,<br />
Mbele kiushindilia, banzi walitakiani?<br />
Nyuma kiurudishia, gogo lina gumu gani?<br />
Seremala mwenye fani, shoka siyo la lazima.<br />
<br />
Shoka kazi yake kuni, Mpishi lampatia,<br />
Kumletea jikoni, kuni za kumpikia,<br />
Zikishapigwa juani, shoka inazipatia,<br />
Seremala mwenye fani, shoka siyo la lazima.
<br />
<br />
 
Si jiti hili ni gogo, kijasho kiliwatoka
Migongo yengia pogo, walichoka wakauka
Kimewashinda kigogo, walia watu wacheka
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala

Mashoka yao ya vyuma, wageni mbali metoka
Kuja gogo kulipima, kijasho kikawatoka
Kuona isitiqama, gogo lilivyotukuka
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala

Gogo mevuka viunzi, vya kiangazi masika
Limekabili mionzi, bila ya kutetereka
Kalilinda Mwenye Enzi, thabiti halina shaka
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala

Muhali gani malenga, na gogo lisochangika
Gogo hili sio changa, kwa kweli limepevuka
Limebeba nyingi kunga, na siri za mamlaka
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala

Ukiliona karibu, vile lilivyoongoka
Ukapewa masahibu, na vile lilivyon'goka
Utatamani kutubu, mlinzi Mola Rabuka
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala

Wazamani na wa sasa, gogo walilizunguka
Kwa hila walipapasa, wajuzi walosifika
Gogo limekuwa tasa, katu halikupasuka
Kila ajaye na shoka, katu hawi seremala
 
Gogo ukilijuulia,katu halitashindika.
kwanza nikulipandia,halafu ukashuka.
liguseguse ubavuni,kama laparuzika.
ukiliona laini.hapo usibebe shoka.
sikila gogo ,lachanjwalo kwa shoka.

Ukucha ni zana, pia yaweza tumika.
Ukijulia kuliparura,lazima litabambuka.
Anza na matawi, kuyakuchakucha.
Ukifika kigogoni,lishaanza kuchimbuka.
Sikila kigumu,chachanjwa na skoka.

Ziko zana kali,zishindazo shoka.
Simsumeno, panga na sishoka,
ni mfano wa patsi,ilioviringika.
zavunjazo magogo,yalioanguka.
Si magogo yote,yachanjwayo kwashoka

Yataka hekima,hadi kupasuka.
Ukilipatia pakuanzia,lile hutetemeka.
Hutoka maji shinani,likaanza kuweweseka.
Ukiingiza patasi,laanza kubogojeka.
Ugumu ni mwanzoni,ukitumiaakili lakatika.

ISIMBA MKALI ALINYESHWA CHAI, NINI CHASHINDIKA?.
 
Tungo zenu nimesoma, nyote mlotangulia
Gogo limefanya goma, au hamjajulia?
Ya nini kushika tama, acheni kulia lia
Gogo hilo gogo gani, hakuna alikatae?

Kateni mbele na nyuma, hakika litabanjuka
zana zenu ziwe vyuma, vile visivyo pindika
msifanye ya hujuma, ustadi wahitajika
Gogo hilo gogo gani, hakuna alikatae?
 
Gogo liso chanjika

ukataji mbele nyuma,hili lakubalika
ongeza kwa kujituma,huku walishikashika
siache kulisukuma,lengo liweze banjika
Gogo liso chanjika,faidae iko wapi?

Nini wajipa kadhia,kwa gogo liso chanjika
Mwishoe waja tufia,na ndugu uwape shaka
Ni bora kujiachilia,hilo halina baraka
Gogo liso chanjika,faidae iko wapi?

Kuzidi lazimishia,ni wewe wajiumiza
hutopata yafidia, gogo hilo miujiza
Muda wako tajutia,na lengo hutotimiza
Gogo liso chanjika,faidae iko wapi?

Ni vyema useme basi,ni tendo la uungwana
sitoe tena nafasi,gogo halina maana
Hata unoe patasi,huwezi lichanachana
Gogo liso chanjika,faidae iko wapi?

Gogo hilo ni la tasa,umri limezidia
ona ya kwake mikasa, nuksi tajipatia
mfano wake ni kasa,chunguza utanambia
Gogo liso chanjika,faidae iko wapi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom