Flowerpot
Senior Member
- Aug 30, 2021
- 179
- 254
Mimewahi cheki movie moja imetengenezwa na iphone 6 kama sijasahau. Huwezi jua ni movie ya simu kama hujaambiwa. Sasa nilikuwa naangalia uzinduzi wa products za apple uliofanyika jana. Hii iphone 13 wameiunda kwaajili ya movie hasa. Utengenezaji wa movie umekuwa rahisi kabisa.
Pia niulize, nilisikia kwenye onpoint ya clouds kuwa hii iphone 13 unaweza kupiga picha maneno halafu ukaextract maneno tu. Maana nilielewa kuwa unaweza kupiga picha kitabu halafu ukakiconvert kuwa word document. Lakini sijasikia apple wenyewe wakisema.
Hii feature ni kweli ipo? Kama ipo itarahisisha sana maisha.
Ukiona hizo shot on iphone movie ujue zimeundwa kwa mazingira perfect kabisa kama mwanga sahihi, kupunguza mtikisiko kwa kutumia gimbal nk. Kwahiyo haireflect matumizi ya kawaida. Yaani ni kama cheating hivi. Wewe ukichukua video haiwezi fanana na yao. Na physics siku zote lazima ishinde, sensor za simu kwa ukubwa ni ndogo sana ukilinganisha na sensor za camera za kawaida. Kwahiyo lazima zitaingiza mwanga mwingi na kutengeneza natural bokeh.