Utendaji wa jeshi la polisi Tanzaniai ni fedheha kubwa kwa taifa

nderingosha

JF-Expert Member
Mar 20, 2011
4,281
3,243
Jeshi la polisi TZ ni moja ya taasisi ya muungano...yaani linafanya kazi zake Tanganyika na Zanzibar..na linatakiwa lisioneshe bias kiutendaji katika sehemu hizi mbili za muungano....Kuna mambo yanayofanywa na jeshi letu la polisi TZ yamenifanya niwe na maswali mengi kuhusu agenda za utendaji wa jeshi la polisi TZ....ebu tafakari haya matendo ya jeshi hili alafu kila mtu atakuwa na conclusion yake......

  • Ni jambo la kawaida nchini TZ kuona wanafunzi wa vyuo vikuu wenye matatizo ya msingi wanapoamua kuandamana/kutembea kwa amani ili kudai haki zao wakitokewa na kupigwa na kutawanywa na polisi wenye magari yenye maji ya pilipili na mabomu ya machozi....wengine hupigwa na polisi na kuumizwa vibaya...tena wale polisi wanaoitwa FFU....tena mabomu hupigwa kama vile wanaoandamana ni magaidi......
  • Ni jambo la kawaida TZ kuona wanaharakati wenye kubeba jumbe za msingi sana kijamaii wanapoamua kuandamana/kutembea kwa amani..hutokewa na kupigwa/kutawanywa na jeshi la polisi....tena kwa kutumia silaha za moto yakiwemo mabomu ya machozi na maji yenye pilipili....mfano...jikumbushe yaliyotokea wakati wanaharakati walipoandamana kushinikiza serikali itatue madai ya madaktari.....walipotokewa na kutawanywa na jeshi la polisi na wengine hata kushikwa na kuwekwa rumande......
  • Ni jambo la kawaida TZ kuona jeshi la polisi likizuia maandamano/matembezi ya amani ya vyama vya siasa kuelekea kwenye mikutano yao.....tena waandamanaji hutawanywa kwa mabomu ya machozi na hata kupigwa vibaya na pia kukamatwa na polisi....kumbuka yaliyotokea CDM kule arusha....na pia kumbuka jeshi la polisi walivyowazuia wafuasi wa CDM wasitembee kwa miguu hivi majuzi kuelekea kwenye mkutano wao jangwani.....
  • Tumeona jeshi la polisi wakiwapiga hadi kuwaua raia wasio na hatia kule songea walipoandaman/tembea kwa amani kudai haki yao ya msingi ya kulindwa na polisi.......
  • LAKINI HIVI MAJUZI KULE ZANZIBAR TUMEONA WAHUNI/WAHALIFU/MAJAMBAZI WAKIANDAMANA NA KUCHOMA HADI MAKANISA.....BILA KUONA HATUA YOYOTE YA POLISI KUINGILIA KWA MABOMU YA MACHOZI AU MAJI PILIPILI AU SILAHA ZA MOTO....KAMA WANAVYOFANYA KWENYE MAANDAMANO/MATEMBEZI YA AMANI TANGANYIKA......HAINGII AKILINI NI KWA VIPI RAIA WALIUWAWA KULE SONGEA KWA KUANDAMANA KWA AMANI...WAKATI WAHALIFU/MAJAMBAZI WAMECHOMA MAKANISA ZENJ HUKU WAKISHUHUDIWA NA HAO HAO POLISI!!!!!!!!HIVI HILI JAMBO LINACHUKULIWAJE???????TAFAKARI........
 
hujafanya research yako vizuri. hata hao wa zenj walipigwa mabomu ya machozi na risasi za mpira walipojaribu kumtoa polisi kiongozi wao aliyekamatwa awali. ndipo wakasambaa na kwenda kufanya fujo hizo ikiwamo kuchoma makanisa.
 
hujafanya research yako vizuri. hata hao wa zenj walipigwa mabomu ya machozi na risasi za mpira walipojaribu kumtoa polisi kiongozi wao aliyekamatwa awali. ndipo wakasambaa na kwenda kufanya fujo hizo ikiwamo kuchoma makanisa.
wakati wanafanya hizo fujo za kuchoma makanisa polisi walikuwa wapi?...na waliwakamata wangapi???
 
Ukwe'e ni kwamba polisi na serikali ya muungano wanaiogopa sana zenj na wanawaogopa sana waislam wa zenj ndo maana tumefika hapa.
 
Ukwe'e ni kwamba
polisi na serikali ya muungano wanaiogopa sana zenj na wanawaogopa sana
waislam wa zenj ndo maana tumefika hapa.

hujui unachoandik chogo wale waliochoma kanisa walifanya baada ya kufukuzwa town na askari ndipo wakaenda mtaani kufanya matukio ya uhalifu kwa kushitukiza ww ulitaka polisi wafanye nn
 
Unachofanya wewe ni kupandikiza chuki tu dhidi ya polisi...JAMBO USILOLIJUA NI SAWA NA USIKU WA GIZA.
 
Hii double standard haiko kwa polisi tu, iko kwa Watanzania walio wengi. Tunapenda kuwasujudia na ku kiss ass "waheshimiwa" wetu. Ndio maana tunawapa kura kwa kishindo CCM inayotunyanyasa na kutufisadi kila siku. Pindi CCM itakapotoka madarakani nao watapingwa mabomu tu unless CDM waingilie kati. Watanzania waliopevuka ndio wanaweza kuchambua kati ya mbichi na mbivu sio hao polisi wachumia tumbo na the rest of wabongo lala.
 
Police thithiem sina imani nao,nikikumbuka kilichotea Mwanza kwa wabunge wa cdm huku police wapo aibu tupu.
 
Unachofanya wewe ni kupandikiza chuki tu dhidi ya polisi...JAMBO USILOLIJUA NI SAWA NA USIKU WA GIZA.
chuki ipi sasa...wewe usiejua ndie unahitaji kuamshwa....Kwa taarifa ya askofu Mokiwa(mwakilishi wa makanisa yooote TZ)....tayari yameshachomwa moto makanisa 25 kule zenj mpaka sasa....yote hayo yamefanyika... polisi wapo..na hakuna mhusika aliyechukuliwa hatua mpaka leo...sasa wewe usiejua unasemaje juu ya hili????hao polisi wako kwa ajili ya kuwalinda nani????wewe usiejua ebu soma hii taarifa hapa Guardian (kama unajua kusoma na kutafakari)...soma hapa...:: IPPMEDIA
 
Mkuu hii double standard iko wazi -fuatilia pia uzi wangu katika jamvi hilihili kwa jana asubuhi unaosema Double standard na kids gloves haitatufikisha mbali, mtoa mada karibu...
 
Unachofanya wewe ni kupandikiza chuki tu dhidi ya polisi...JAMBO USILOLIJUA NI SAWA NA USIKU WA GIZA.
chuki ipi sasa...wewe usiejua ndie unahitaji kuamshwa....Kwa taarifa ya askofu Mokiwa(mwakilishi wa makanisa yooote TZ)....tayari yameshachomwa moto makanisa 25 (kuanzia mwaka 2001) kule zenj mpaka sasa....yote hayo yamefanyika... polisi wapo..na hakuna mhusika aliyechukuliwa hatua mpaka leo...sasa wewe usiejua unasemaje juu ya hili????hao polisi wako kwa ajili ya kuwalinda nani????wewe usiejua ebu soma hii taarifa hapa Guardian (kama unajua kusoma na kutafakari)...soma hapa...:: IPPMEDIA
 
Malaria Sugu alisema ni 'zamu yao' ...kwamba mpaka Kikwete anatoka madarakani watakaokuwa wanashughulikiwa na polisi ni CHADEMA na wanaharakati wengine lakini siyo waislam...Kuna ka ukweli ndani yake ukiangalia matukio yaliyotokea...!
 
wakati wanafanya hizo fujo za kuchoma makanisa polisi walikuwa wapi?...na waliwakamata wangapi???

Watu 74 wamekamatwa na wameshafunguliwa Mashtaka siku ya Jumatatu!! Katika hao kuna ambao ni Majeruhi waliopo chini ya Ulinzi Mkali kwenye hospitali ya Mnazi Mmoja! Sikiliza Habari utapata kinachojiri Znz!!
 
Malaria Sugu alisema ni 'zamu yao' ...kwamba mpaka Kikwete anatoka madarakani watakaokuwa wanashughulikiwa na polisi ni CHADEMA na wanaharakati wengine lakini siyo waislam...Kuna ka ukweli ndani yake ukiangalia matukio yaliyotokea...!

Upuuzi huu!! Kwani waliochoma Makanisa ni Polisi au Serikali??
 
Watu 74 wamekamatwa na wameshafunguliwa Mashtaka siku ya Jumatatu!! Katika hao kuna ambao ni Majeruhi waliopo chini ya Ulinzi Mkali kwenye hospitali ya Mnazi Mmoja! Sikiliza Habari utapata kinachojiri Znz!!
dada kwa taarifa yako nafatilia taarifa za zenj kuliko ujuavyo...maana ndugu zangu walioko zenj nao kanisa lao limechomwa....hoj yangu ya msingi hapa ni kwamba....iweje hawa polisi wanakuwa fasta sana kwenye yale matukio Tanganyika ambayo mara nyingi hayaashirii uhalifu au uvunjifu wa amani ...tena wanatumia nguvu nyingi...lakini yanapokuja matukio yenye uvunjifu wa amani wa dhahiri/uhalifu....kama haya ya zenj..wao polisi wanakuwa slow kuchukua na kutumia nguvu...na hata watu wanapokamatwa hatua dhidi yao hazichukuliwi....Refer case 25 za kuchomwa makanisa zenj tangu 2001..alafu tuambie polisi wamefanya nini??????...Kwanini tusiamini kuwa hawa polisi wanashiriki agenda chafu za siri kama utendaji wao una utata kwa kiasi hiki????.........Kwa taarifa yako...soma magazeti ya zenj ya leo.....tayari kuna tamko jipya kubwa la viongozi wa dini kule zenj....dhidi ya matendo ya hawa hawa polisi.....
 
Tatizo ktk jeshi la Polisi lipo ktk maadili kuanzia kwenye vyuo vya polisi.uteuzi wa maafisa wa polisi. Kujingiza kwenye masuala ya kisiasa badala ya kufuata sheria zinazongoza jeshi la polisi. Mfumo wa utawala wa nchi ndiyo tatizo la jeshi la polisi kujikita ktk siasa.
 
Back
Top Bottom