BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Date: 2/20/2010
Kila mbunge kuvuna Sh46 milioni za kiinua mgongo
*Ni asilimia 40 ya mishara yate ya miaka mitano
Exuper Kachenje
Mwananchi
KILA Mbunge ataondoka na zaidi ya Sh46milioni kama kiinua mgongo baada ya Rais Jakaya Kikwete kulivunja Bunge Julai mwaka huu.
Bunge hilo litavunjwa baada ya mkutano wa bajeti unaotarajiwa kumalizika mwishoni mwa Agosti mwaka huu kwa ajili ya kujiandaa uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba.
Fedha hizo ni sawa na asilimia 40 ya mishahara ya miaka yote mitano ya utumishi bungeni ambapo mshahara wa kila mbunge kwa sasa anafikia jumla ya Sh1,921,000 kwa mwezi.
Kwa mujibu wa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashilillah, wabunge watalipwa fedha zao mara baada ya Bunge kuvunjwa.
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lina wabunge 325, kati yao 49 ni mawaziri na manaibu waziri. Ukiondoa mawaziri na manaibu wao ambao kinua mgongo chao hulipwa na serikali, hivyo watakao lipwa na Bunge ni 276. Kwa mantiki hiyo jumla ya Sh12,724,704,000 zitalipwa kama kiinua mgongo kwa wabunge hao ukiondoa mawaziri.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa malipo ya wabunge hao, yatatolewa kwa mujibu wa sheria ya mafao ya viongozi wa kisiasa ya mwaka 1999 ambayo ilianza kutumika 2000.
Kwa mujibu wa sheria hiyo, iliyotokana na marekebisho ya sheria ya awali ya mafao ya viongozi maalum wa kitaifa ya mwaka 1986, kila mbunge atalipwa asilimia 40 ya mshahara wake alioupokea kwa kipindi chote cha miaka mitano.
Marekebisho ya mishahara ya viongozi wakuu wa nchi na viongozi wa kisiasa yaliyofanywa Julai mwaka jana, yameonyesha kuwa, mbunge anapokea Sh1,921,000milioni kwa mwezi.
Hata hivyo sheria imeeleza kuwa sio wabunge wote watakaovuna kiasi hicho cha fedha, kwa kuwa muda wao wa kuwa bungeni unatofautiana.
Afisa mmoja mwandamizi katika ofisi ya Bunge ambaye hakutaka kutajwa gazetini alilidokeza gazeti hili jana kuwa wabunge watapata mafao hayo baada ya Rais Kikwete kulivunja Bunge.
"Mimi si msemaji wa Bunge lakini, kwa kukusaidia tu fedha hizo zitalipwa baada tu ya rais kutangaza rasmi kulivunja Bunge.
Wabunge watazikuta fedha hizo kwenye akaunti zao kati ya Julai na Agosti," alisema na kuongeza:
"Malipo hayo yatafanywa kwa kuzingatia Sheria ya Mafao ya Viongozi wa Kisiasa ya mwaka 1999 iliyopo sasa, iliyoanza kutumika mwaka 2000. Sheria hiyo ilitokana na marekebisho yaliyofanywa kwa sheria ya awali, ambayo ni Sheria ya mafao ya viongozi maalum wa kitaifa ya mwaka 1986".
Katibu wa Bunge Dk Thomas Kashilillah alilithibitishia Mwananchi kuwa malipo hayo ya kiinua mgongo yatafanyika kwa kutumia sheria hiyo baada ya bunge kuvunjwa.
"Sheria iliyopo ndiyo itakayotumika na ndiyo itayoongoza kufanya malipo hayo. Sheria hiyo ni ya Mafao ya Viongozi wa Kisiasa ya mwaka 1999 iliyoanza kutumika mwaka 2000," alisema Dk Kashilillah.
Alifafanua zaidi akiasema: "Malipo yanaweza kufanyika 'at either' (wakati wowote), kabla au baada ya kuvunjwa Bunge".
Kuhusu kiinua mgongo kwa mawaziri na manaibu wao Kashilillah alisema sheria ipo wazi kuhusu viongozi hao na kueleza kuwa hawalipwi mishahara na Bunge bali serikali kupitia wizara husika.
"Kuna mafao ya Bunge na serikali, sisi hatulipi mishahara ya mawaziri, bali ya wabunge. Mawaziri wanalipwa mishahara na serikali, sheria ipo wazi, ukiisoma imeweka wazi hilo," alisema Dk Kashilillah.
Sheria hiyo imeainisha pia viwango vya malipo vya viongozi wa juu serikalini ikiwamo rais, makamu wake na waziri mkuu.
Aidha, imewajumuisha mawaziri na manaibu wao, wakuu wa mikoa, wilaya, Spika wa Bunge na Naibu wake.
Spika wa Bunge na naibu wake watapata kiinua mgongo cha kiwango sawa na rais mstaafu, lakini, watatofautiana kwenye baadhi ya mafao.
Kwa mahesabu ya viwango vya mishahara yao, mawaziri na manaibu wao watuchukua jumla ya Sh2,658,768,000 kama kiinua mgongo chao.
Mwaka uliopita serikali iliwaongezea mishahara viongozi wakuu wa nchi na viongozi wa kisiasa ambapo mishahara ya wabunge ilipanda kutoka Sh1,840,000 hadi 1,921,000 na naibu Spika kutoka Sh Sh2,080,000 hadi Sh2,172,000.
"Viwango vya mishahara kwa viongozi wa serikali vinawekwa na serikali, mimi hainihusu hivyo siwezi kuthibitisha hilo. Nimesikia tu kama mlivyosikia ninyi," Katibu wa Bunge Dk Thomas Kashilillah aliliambia gazeti hili alipotakiwa kuthibitisha ongezeko hilo la mishahara mwaka jana.
Hata hivyo, viwango hivyo vya mishahara, havijumuishi posho za vikao, mafuta ya gari na fedha za kujikimu ambapo sasa Mbunge mmoja anapata Sh135,000 kama posho kwa kikao kimoja cha Bunge ambayo pia mawaziri na manaibu hunufaika nayo.
Kila mbunge kuvuna Sh46 milioni za kiinua mgongo
*Ni asilimia 40 ya mishara yate ya miaka mitano
Exuper Kachenje
Mwananchi
KILA Mbunge ataondoka na zaidi ya Sh46milioni kama kiinua mgongo baada ya Rais Jakaya Kikwete kulivunja Bunge Julai mwaka huu.
Bunge hilo litavunjwa baada ya mkutano wa bajeti unaotarajiwa kumalizika mwishoni mwa Agosti mwaka huu kwa ajili ya kujiandaa uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba.
Fedha hizo ni sawa na asilimia 40 ya mishahara ya miaka yote mitano ya utumishi bungeni ambapo mshahara wa kila mbunge kwa sasa anafikia jumla ya Sh1,921,000 kwa mwezi.
Kwa mujibu wa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashilillah, wabunge watalipwa fedha zao mara baada ya Bunge kuvunjwa.
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lina wabunge 325, kati yao 49 ni mawaziri na manaibu waziri. Ukiondoa mawaziri na manaibu wao ambao kinua mgongo chao hulipwa na serikali, hivyo watakao lipwa na Bunge ni 276. Kwa mantiki hiyo jumla ya Sh12,724,704,000 zitalipwa kama kiinua mgongo kwa wabunge hao ukiondoa mawaziri.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa malipo ya wabunge hao, yatatolewa kwa mujibu wa sheria ya mafao ya viongozi wa kisiasa ya mwaka 1999 ambayo ilianza kutumika 2000.
Kwa mujibu wa sheria hiyo, iliyotokana na marekebisho ya sheria ya awali ya mafao ya viongozi maalum wa kitaifa ya mwaka 1986, kila mbunge atalipwa asilimia 40 ya mshahara wake alioupokea kwa kipindi chote cha miaka mitano.
Marekebisho ya mishahara ya viongozi wakuu wa nchi na viongozi wa kisiasa yaliyofanywa Julai mwaka jana, yameonyesha kuwa, mbunge anapokea Sh1,921,000milioni kwa mwezi.
Hata hivyo sheria imeeleza kuwa sio wabunge wote watakaovuna kiasi hicho cha fedha, kwa kuwa muda wao wa kuwa bungeni unatofautiana.
Afisa mmoja mwandamizi katika ofisi ya Bunge ambaye hakutaka kutajwa gazetini alilidokeza gazeti hili jana kuwa wabunge watapata mafao hayo baada ya Rais Kikwete kulivunja Bunge.
"Mimi si msemaji wa Bunge lakini, kwa kukusaidia tu fedha hizo zitalipwa baada tu ya rais kutangaza rasmi kulivunja Bunge.
Wabunge watazikuta fedha hizo kwenye akaunti zao kati ya Julai na Agosti," alisema na kuongeza:
"Malipo hayo yatafanywa kwa kuzingatia Sheria ya Mafao ya Viongozi wa Kisiasa ya mwaka 1999 iliyopo sasa, iliyoanza kutumika mwaka 2000. Sheria hiyo ilitokana na marekebisho yaliyofanywa kwa sheria ya awali, ambayo ni Sheria ya mafao ya viongozi maalum wa kitaifa ya mwaka 1986".
Katibu wa Bunge Dk Thomas Kashilillah alilithibitishia Mwananchi kuwa malipo hayo ya kiinua mgongo yatafanyika kwa kutumia sheria hiyo baada ya bunge kuvunjwa.
"Sheria iliyopo ndiyo itakayotumika na ndiyo itayoongoza kufanya malipo hayo. Sheria hiyo ni ya Mafao ya Viongozi wa Kisiasa ya mwaka 1999 iliyoanza kutumika mwaka 2000," alisema Dk Kashilillah.
Alifafanua zaidi akiasema: "Malipo yanaweza kufanyika 'at either' (wakati wowote), kabla au baada ya kuvunjwa Bunge".
Kuhusu kiinua mgongo kwa mawaziri na manaibu wao Kashilillah alisema sheria ipo wazi kuhusu viongozi hao na kueleza kuwa hawalipwi mishahara na Bunge bali serikali kupitia wizara husika.
"Kuna mafao ya Bunge na serikali, sisi hatulipi mishahara ya mawaziri, bali ya wabunge. Mawaziri wanalipwa mishahara na serikali, sheria ipo wazi, ukiisoma imeweka wazi hilo," alisema Dk Kashilillah.
Sheria hiyo imeainisha pia viwango vya malipo vya viongozi wa juu serikalini ikiwamo rais, makamu wake na waziri mkuu.
Aidha, imewajumuisha mawaziri na manaibu wao, wakuu wa mikoa, wilaya, Spika wa Bunge na Naibu wake.
Spika wa Bunge na naibu wake watapata kiinua mgongo cha kiwango sawa na rais mstaafu, lakini, watatofautiana kwenye baadhi ya mafao.
Kwa mahesabu ya viwango vya mishahara yao, mawaziri na manaibu wao watuchukua jumla ya Sh2,658,768,000 kama kiinua mgongo chao.
Mwaka uliopita serikali iliwaongezea mishahara viongozi wakuu wa nchi na viongozi wa kisiasa ambapo mishahara ya wabunge ilipanda kutoka Sh1,840,000 hadi 1,921,000 na naibu Spika kutoka Sh Sh2,080,000 hadi Sh2,172,000.
"Viwango vya mishahara kwa viongozi wa serikali vinawekwa na serikali, mimi hainihusu hivyo siwezi kuthibitisha hilo. Nimesikia tu kama mlivyosikia ninyi," Katibu wa Bunge Dk Thomas Kashilillah aliliambia gazeti hili alipotakiwa kuthibitisha ongezeko hilo la mishahara mwaka jana.
Hata hivyo, viwango hivyo vya mishahara, havijumuishi posho za vikao, mafuta ya gari na fedha za kujikimu ambapo sasa Mbunge mmoja anapata Sh135,000 kama posho kwa kikao kimoja cha Bunge ambayo pia mawaziri na manaibu hunufaika nayo.