Utendaji mbovu wa Shirika la TANESCO: Kwanini nisubiri zaidi ya miezi 6 kuunganishiwa umeme ulio mlangoni kwangu Gongo la Mboto?

Ahsante kwa ushuhuda wako

Tafadhali tusaidieni taarifa kamili tupo kuwahudumia
Tunashukuru vile umekuja na kujibu maswali kwa wakati.

Unatakiwa kufanya nini ili kubadilishiwa tarrif? Mimi nimeunganishiwa umeme mwezi Januari 2020 nikapigwa tariff 1 nafikiri (ile ya elfu 10 unit 28), matumizi yangu kwa mwezi ni wastani wa unit 60, ninaona ninastahili kuwa katika tarrif ya matumizi madogo (tarrif 4 nafikiri - sina uhakika, kama nakosea nirekebishwe) nipo Kiluvya.
 
Tunashukuru vile umekuja na kujibu maswali kwa wakati.

Unatakiwa kufanya nini ili kubadilishiwa tarrif? Mimi nimeunganishiwa umeme mwezi Januari 2020 nikapigwa tariff 1 nafikiri (ile ya elfu 10 unit 28), matumizi yangu kwa mwezi ni wastani wa unit 60, ninaona ninastahili kuwa katika tarrif ya matumizi madogo (tarrif 4 nafikiri - sina uhakika, kama nakosea nirekebishwe) nipo Kiluvya.
Tafadhali onyesha namba ya mita tuhakiki
 
Katika juhudi za kuboresha uchumi, upatikanaji wa nishati ni muhimu sana.

Ila kama pia usambazaji wa nishati utalega tunaweza tusipate matokeo tarajiwa.

Mimi ni mkazi wa Ukonga, Imepita miezi 6 tangu nimalize mchakato wote wa kupata umeme, yaani kufanya e/wiring kwangu, maombi, survey, wakatoa ripoti, inahitajika nguzo moja, wakanipa control number, nikalipia. Almost 600,000TSH. Tangia mwaka jana August nimekuwa nikifuatilia Gongo la Mboto mpaka kuonana na Meneja ili nijue tatizo kwa nini hawajaja kuunganisha umeme bila mafanikio, danadana nyingi, uongo uongo mwingi, mwisho nenda tutashughulikia na hawashughulikii.

Je, kwa hali hii, mtu kuunganishiwa umeme uliopita 105m kutoka kwake TANESCO inachukua zaidi ya miezi sita, uchumi wa kati tutatoboa kweli, hili kwa kweli ni swali kwa Waziri wa nishati.

Mimi nafikiri kuna umuhimu wa kulivunja hili shirika ili kuongeza ufanisi wa huduma za nishati au kuhusisha mashirika binafsi kwa kiwango kikubwa katika shughuli wanazoweza kufanya. Mfano: kwa sasa hatupati shida kwenye suala la kuunganishiwa mawasiliano ya simu kwa sababu TTCL wana washindani, ila kipindi wakiwa wenyewe walikuwa na ukiritimba mwingi kama huu wa TANESCO

Kuna harufu kubwa ya rushwa hapa, hasa hapa branch la TANESCO Gongo la Mboto, watu wanacheleweshewa huduma kwa makusudi ili waingie mfukoni kutoa rushwa, Nashauri PCCB wamulike eneo hili.

TANESCO wafanye kazi zao, kwa nini nilipe laki sita kuunganishiwa umeme na nisubiri zaidi ya miezi 6, hiyo fedha ningekuwa nimeitumia kwa biashara ningekuwa na bakaa fulani ya kunitoa mwaka 2021, kuna umuhimu wa kuwa na mkataba kwa wateja, yaani ndani ya muda gani mteja atakuwa ameunganishiwa umeme, iwapo watavuka muda huo kuwe na hatua madhubuti za kumlinda mteja kwa uonevu huo.
Pamoja na maelezo marefu.
Nikuambie tu hiyo laki 6 umepigwa gharama ya kuunganisha umeme ndani ya mita 100 haifiki laki 6. Pia tambua nguzo za Tanesco haziuzwi. Wana mtindo wanakuambia nguzo moja bure ya pili unalipia. URONGO.

AU NASEMA UONGO NDUGU YANGU TANESCO
 
tunachokifanya hapa kinaitwa whistle blowing siyo ila mtoa taarifa anapenda kujulikana hapa tumeshawapa pa kuanzia ni swala la nyie wenyewe kujifanyia tathmini kila meneja aitishe mafaili yaliyokaa muda mrefu na ahakikishe yanafanyiwa kazi na siyo unihudumie mimi kwa sababu nimepaza sauti bali badilisheni mfumo wenu wa huduma….ushaambiwa bila kuwaona wale vishoka hupati huduma unataka jina la nini sasa
Wanataka jina ili wakawaambie wenzao anaeleta chokochoko zote hizi ni pombe kali
 
Wanataka jina ili wakawaambie wenzao anaeleta chokochoko zote hizi ni pombe kali
Taarifa kamili ndio huduma mpendwa mteja wetu

Unapolalamika unalenga kuhudumiwa na unapohitaji huduma onyesha taarifa kamili maana wakati mwingine unakuta ni vishoka wanafatilia kazi za watu na hawana taarifa kamilo.hivyo kama ni mteja halali unaogopa nini kutuma taarifa hata inbox uhudumiwe
 
Vishoka tunaomaanisha ni wateja wanaojifanya wanafatilia kazi za wateja au kujifanya wafanyakazi ili wajipatia fedha isivyo kihalali

Nchi ina miaka 60 ya Uhuru lakini bado mnafanya kazi kizamaniiii. Yani hamuwahudumii watu mpaka walalamike, lipite zogo, vurugu za maongezi dah!, Mtu analipia huduma kumpa sasa haki yake ya kimsingi ya kile alicholipia mpaka lipite zogo.
Ni shirika lenye watu wavivu msio na mfano, miezi 6 toka mtu alipie mnazurura tu, Pesa yake mmekula kumpa huduma majanga.
Ningekuwa Jiwe au Waziri anaehusika na hii mamlaka yenu aisee ningeanza na wewe uliepo humu. Upo humu kila siku lakini malalamiko hayaishi, maana yake ni kwamba hata wewe ni mvivu. Uwepo wako humu ilitakiwa liwe ndio suluhisho la ucheleweshaji. Sasa kama upo humu kuwahudumia wale wanaolalamikia huduma yenu Vp wale ambao hawajajiunga humu huku wakicheleweshewa huduma, wao walalamike wapi ili kilio chao kisikike???
Tunasoma habari za shirika lenu mpaka tunasikia aibu. Mnatutia aibu kwa wageni. Kuna wageni wapo humu wanaojua Kiswahili, wanatusimanga wanaposoma malalamiko ya wateja wenu. Makazini humu na matusi kututukana huku wakitoa mifano ya shirika lenu kuwa lina mijitu mivivu.
Jirekebisheni bana.
 
Nchi ina miaka 60 ya Uhuru lakini bado mnafanya kazi kizamaniiii. Yani hamuwahudumii watu mpaka walalamike, lipite zogo, vurugu za maongezi dah!, Mtu analipia huduma kumpa sasa haki yake ya kimsingi ya kile alicholipia mpaka lipite zogo.
Ni shirika lenye watu wavivu msio na mfano, miezi 6 toka mtu alipie mnazurura tu, Pesa yake mmekula kumpa huduma majanga.
Ningekuwa Jiwe au Waziri anaehusika na hii mamlaka yenu aisee ningeanza na wewe uliepo humu. Upo humu kila siku lakini malalamiko hayaishi, maana yake ni kwamba hata wewe ni mvivu. Uwepo wako humu ilitakiwa liwe ndio suluhisho la ucheleweshaji. Sasa kama upo humu kuwahudumia wale wanaolalamikia huduma yenu Vp wale ambao hawajajiunga humu huku wakicheleweshewa huduma, wao walalamike wapi ili kilio chao kisikike???
Tunasoma habari za shirika lenu mpaka tunasikia aibu. Mnatutia aibu kwa wageni. Kuna wageni wapo humu wanaojua Kiswahili, wanatusimanga wanaposoma malalamiko ya wateja wenu. Makazini humu na matusi kututukana huku wakitoa mifano ya shirika lenu kuwa lina mijitu mivivu.
Jirekebisheni bana.
Tunashukuru sana mteja aliyelalamika hakutoa taarifa kamili tuone hicho alicholalamikia hivyo nie vema kuacha atoe ushirikiano tuone taarifa kwenye mfumo na kumuhudumia
 
Tatizo Janja Janja nyingi TANESCO dawa yenu kuwaripoti kwa mkuu, maana bila kuchangamshwa hamfanyi kazi

Hivi siku mkipata mshindani si mtafilisika nyie? Acheni hizo
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom