UJANJAUJANJA
JF-Expert Member
- Oct 14, 2012
- 226
- 122
Wana JF,
Leo nilipata bahati ya kupita karibu na kituo cha polisi cha Chang'ombe, nikaona ni heri nipeleke gari langu pale kwa ajili ya kufanyiwa ukaguzi na ikithibitika liko vizuri basi nipewe stika ya nenda kwa usalama barabarani. Baada ya kufika nilijitambulisha na kuomba gari langu lifanyiwe ukaguzi, cha kushangaza ni kwamba badala ya kwenda kufanya ukaguzi kutambua "road worthiness" ya gari, askari aliyekuwepo pale akaomba kupatiwa nakala ya kadi ya gari akaanza kuandika na baada kunikabidhi stika. Nikamuuliza, ndugu yangu siku hizi utaratibu umebadilika? Akabaki anashangaa. Nikaendelea kumuomba anifahamisha kwa sababu nilikuwa nje ya TZ miaka miwili sasa na kama utaratibu ni kuandika tu au kukagua gari kwanza. Nilichokigundua ni kwamba pamoja na kukabidhiwa majukumu yake, askari yule hajui sheria inamtaka atekeleze na afanye nini. Tuna safari ndefu kuzuia ajali ambazo zingeweza kuepukwa bila ulazima
Leo nilipata bahati ya kupita karibu na kituo cha polisi cha Chang'ombe, nikaona ni heri nipeleke gari langu pale kwa ajili ya kufanyiwa ukaguzi na ikithibitika liko vizuri basi nipewe stika ya nenda kwa usalama barabarani. Baada ya kufika nilijitambulisha na kuomba gari langu lifanyiwe ukaguzi, cha kushangaza ni kwamba badala ya kwenda kufanya ukaguzi kutambua "road worthiness" ya gari, askari aliyekuwepo pale akaomba kupatiwa nakala ya kadi ya gari akaanza kuandika na baada kunikabidhi stika. Nikamuuliza, ndugu yangu siku hizi utaratibu umebadilika? Akabaki anashangaa. Nikaendelea kumuomba anifahamisha kwa sababu nilikuwa nje ya TZ miaka miwili sasa na kama utaratibu ni kuandika tu au kukagua gari kwanza. Nilichokigundua ni kwamba pamoja na kukabidhiwa majukumu yake, askari yule hajui sheria inamtaka atekeleze na afanye nini. Tuna safari ndefu kuzuia ajali ambazo zingeweza kuepukwa bila ulazima