Uteketezaji huu wa vifaranga ni unyama uliopitiliza

ibanezafrica

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,261
6,543
Kupitia taarifa ya habari jana Jumatatu saa mbili usiku Azam TV imeripoti habari ya kiwanda kimoja cha kuzalisha vifaranga cha mjini Moshi kuteketeza mamia ya vifaranga kwa kuwatosa kwenye moto mkaili eti kisa tu vifaranga hao wamekosa soko!

Kweli japo kuku wanaliwa kila siku lakini kitendo kilichofanywa na uongozi wa kiwanda hicho ni cha kinyama tena kinyama mno.

Kwa kweli nimepigwa na butwaa baada ya kusikiliza habari ile na kumshuhudia mmoja wa wafanyakazi akitupia box moja baada ya jingine juu ya moto mkali huku vifaranga vikilia kwa uchungu! Aisee imeniuma mno.

Sababu za mkurugenzi:

~ Walivisafirisha vifaranga hivyo hadi Dar ili viuzwe kwa tsh 1000, biashara ikawa ngumu kwa sababu ati kuna watu wengi sasa hivi wana ingiza vifaranga toka nje hivyo soko limetibuka.

Wakaamua washushe bei hadi Tsh 900, bado hawakupata soko. Wakaamua mzigo urudi kiwandani Moshi huko nako wakatangaza bei ya Tsh 900 ikashindikana, uamuzi wao wa mwisho ukawa ni kuwateketeza kwa moto mkali!

Tuiombe serikali kitengo cha watu wa mifugo au kama bado ipo taasisi ya kutetea wanyama iwafuatilie wamiliki wa kiwanda hiki na ikibidi wachukuliwe hatua kali ili iwe onyo kwa wengine watakaofikiria kufanya upuuzi huu.

Maana Mkurugenzi wao ameshasema kuwa vifaranga wengine laki nane na nusu wanatarajiwa hivi karibuni na hajui pa kuwapeleka.

Nimejiuliza kwanini basi hata huku Dar na Moshi wasivigawe kwa mtu yeyote atakayeweza kutunza? Hata kama mtu angechukua 20 mwingine box 4, mwenye vifaranga 60 n.k, wangetangaza tu hadharani, au kuwatangazia hata majeshini, vyuoni pengine wangejaribu kuwakuza vifaranga hao wa nyama na mayai.

Nimalizie kwa kusema kitendo kile ni cha kishetani na hakina budi kulaaniwa na serikali ichukue hatua stahiki na hili lisijirudie.

 
hapo pana utata inawezekana hata wao hawajapenda ila mazingira yalikuwa ni limited kwao! Maana ilikuwa inatakiwa kuvilisha na kuvitibu kila siku, so kuliko kubiacha vife na njaa wameona bora vichomwe tu
Kwa hiyo mfanya biashara anaweza kuona ni heri avichime kuliko kushusha bei akauza japo 500tsh akapata nusu bei? Hivyo vifaranga vina corona.

Walete sababu nyingine ila hizo ngonjela wadangaye wajinga
 
Kwa hiyo mfanya biashara anaweza kuona ni heri avichime kuliko kushusha bei akauza japo 500tsh akapata nusu bei? Hivyo vifaranga vina corona.

Walete sababu nyingine ila hizo ngonjela wadangaye wajinga
Sidhani kama hali iko hivyo inawezekana walikuwa hawana njia kabisa! All in all Ukiwa unatetea mambo kama haya huku unamla samaki, kuku, Ng'ombe au kiumbe chochote kile ni yale yale
 
Kwanza naomba niseme hao siyo vifaranga original walioumbwa na Mungu or Allah, hao ni matokeo ya utundu wa mwanaadam.

Pili wangekuwa Og ambao wangeweza kujilisha wenyewe nadhani hata staff wa kiwanda wangebeba na kwenda kuwamwaga kwenye cage sababu wanatafuta na kufukua chakula popote.

Pamoja na yote kuku wa machine hana haki wala sheria ya kumlinda, kuku gani ukimuweka stendi ya daladala aondoki wala ageuki!.
 
Kwanza naomba niseme hao siyo vifaranga original walioumbwa na Mungu or Allah, hao ni matokeo ya utundubwa mwanaadam.

Pili wangekuwa Og ambao wangeweza kujilisha wenyewe nadhani hata staff wa kiwanda wangebeba na kwenda kuwamwaga kwenye cage sababu wanatafuta na kufukua chakula popote.

Pamoja na yote kuku wa machine hana haki wala sheria ya kumlinda, kuku gani ukimuweka stendi ya daladala aondoki wala ageuki!.
Vifaranga haviwezi kujileo vyenyewe viwe vifaranga vya kiswahili au vya kizungu ni sawa na mtoto mchanga hawezi kujilea mwenyewe ukishasikia kifaranga ni sawa na mtoto mchanga, vifaranga vinahitaji malezi makubwa we chunguza vifaranga vya kiswahili vikiwa na mama yao wanavyo pewa malezi usiku au wakati wabaridi mama yao uwapatia joto kwa kuwakumbatia na wakati wa chakula mama uwatafutia chakula tena hii ni kwa ndege wote, sasa itakuwa kwa vifaranga vya kizungu visivyo kuwa na Mama mtu tu wakawaida havichukue akavifuge kienyeji hata siku mbili havifiki bora ata kuku wa kiswahili wanaweza kutoboa, Kuku wa kisasa kwanza wanakula masaa 24hrs na wanatakiwa wawekewe taa na majiko ya kuwaletea joto usiku na maisha yao yote ni kuwanywesha madawa bila madawa hawa wezi kuishi na bandani kwao lazima ukiingia ujisafishe na maji ya dawa na utenge viatu vya kuingia navyo bandani mwao.
 
Kupitia taarifa ya habari jana jumatatu saa mbili usiku azam tv imeripoti habari ya kiwanda kimoja cha kuzalisha vifaranga cha mjini Moshi kuteketeza mamia ya vifaranga kwa kuwatosa kwenye moto mkaili eti kisa tu vifaranga hao wamekosa soko!

Kweli japo kuku wanaliwa kila siku lakini kitendo kilichofanywa na uongozi wa kiwanda hicho ni cha kinyama tena kinyama mno,
Kwa kweli nimepigwa na butwaa baada ya kusikiliza habari ile na kumshuhudia mmoja wa wafanyakazi akitupia box moja baada ya jingine juu ya moto mkali huku vifaranga vikilia kwa uchungu!..aisee imeniuma mno.

Sababu za mkurugenzi:

Walivisafirisha vifaranga hivyo hadi Dar ili viuzwe kwa tsh 1000@..biashara ikawa ngumu kwa sababu ati kuna watu wengi sasa hivi wana ingiza vifaranga toka nje hivyo soko limetibuka..wakaamua washushe bei hadi tsh 900...bado hawakupata soko..wakaamua mzigo urudi kiwandani Moshi huko nako wakatangaza bei ya tsh 900 ikashindikana..uamuzi wao wa mwisho ukawa ni kuwateketeza kwa moto mkali!

Tuiombe serikali kitengo cha watu wa mifugo au kama bado ipo taasisi ya kutetea wanyama iwafuatilie wamiliki wa kiwanda hiki na ikibidi wachukuliwe hatua kali ili iwe onyo kwa wengine watakaofikiria kufanya upuuzi huu.maana mkurugenzi wao ameshasema kuwa vifaranga wengine laki nane na nusu wanatarajiwa hivi karibuni na hajui pa kuwapeleka.

Nimejiuliza kwanini basi hata huku Dar na Moshi wasivigawe kwa mtu yeyote atakayeweza kutunza?hata kama mtu angechukua 20 mwingine box 4,mwenye vifaranga 60 nk wangetangaza tu hadharani..au kuwatangazia hata majeshini,vyuoni pengine wangejaribu kuwakuza vifaranga hao wa nyama na mayai.

Nimalizie kwa kusema kitendo kile ni cha kishetani na hakina budi kulaaniwa na serikali ichukue hatua stahiki na hili lisijirudie.

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Hivyo viwanda ni wapumbavu kuliko vifranga wenyewe. Wakati wa Magu waliamua kutototolesha vifaranga wakisema mayai ni adimu. Karibu nchi nzima kupata vifaranga ilikuwa taabu. Unatoa oda inachukua miezi zaidi ya minne kupata tena kwa mbinde haswaa

Niliacha kufuga kwa sababu nina rafiki yangu anafanyakazi kwenye mojawapo ya hivi viwanda na akaniambia Msanii usihangaike na kufuga kwa sababu viwanda wanalipwa na makampuni ya nje kusitisha utotoleshaji na ikatumika mbinu ya kuongeza bei ya vyakula vya kuku..... kisa kilikuwa ni yale matukio ya kuchoma vifaranga kutoka nje. Waliamua kumkomesha Magu wakidhani yeye ndo anafuga


Last week jirani yangu wakala wa vifaranga na yeye anafuga ameniambia, Msanii hali sasa ni ngumu kuku hawwna soko na bei imeshuka hadi Tshs 1,300. Yeye ana kuku wa mwezi na nusu bandani sasa.

Nimeishauri sana serikali hapo awali kuwa na kurugenzi kamili ya ujasusi wa kibiashara kwa faida ya nchi lakini serikali imewekeza kwenye mitambo ya kuwadukua raia wake wanaowakosoa viongozi.

Nchi hii inahitaji kukombolewa kutoka makucha ya CCM

Hao watotoleshaji waendelee kuisoma namba kwa sababu dhambi ya usaliti itawatafuna hadi wajute.

Walishindwa nini kuwagawa bure hao vifaranga badala ya kuwachoma?
 
Mtu anashangaa kifaranga kuchomwa moto, wakati mtu huyo huyo anachinja kuku amle nyama...

Vyote ni kuua kuku, utofauti ni kuku kauawa akiwa na umri gani...

Anyway, uamuzi wa kiwanda umekaa kikanjanja hivi
 
Kwa hiyo mfanya biashara anaweza kuona ni heri avichime kuliko kushusha bei akauza japo 500tsh akapata nusu bei? Hivyo vifaranga vina corona.

Walete sababu nyingine ila hizo ngonjela wadangaye wajinga
Hata hiyo jero hakuna atakae nunua. Watu wengi wameacha kufuga maana gharana za chakula Cha mifugo Iko juu sana huku kuku sokoni hawana bei
 
Kupitia taarifa ya habari jana jumatatu saa mbili usiku azam tv imeripoti habari ya kiwanda kimoja cha kuzalisha vifaranga cha mjini Moshi kuteketeza mamia ya vifaranga kwa kuwatosa kwenye moto mkaili eti kisa tu vifaranga hao wamekosa soko!

Kweli japo kuku wanaliwa kila siku lakini kitendo kilichofanywa na uongozi wa kiwanda hicho ni cha kinyama tena kinyama mno,
Kwa kweli nimepigwa na butwaa baada ya kusikiliza habari ile na kumshuhudia mmoja wa wafanyakazi akitupia box moja baada ya jingine juu ya moto mkali huku vifaranga vikilia kwa uchungu!..aisee imeniuma mno.

Sababu za mkurugenzi:

Walivisafirisha vifaranga hivyo hadi Dar ili viuzwe kwa tsh 1000@..biashara ikawa ngumu kwa sababu ati kuna watu wengi sasa hivi wana ingiza vifaranga toka nje hivyo soko limetibuka..wakaamua washushe bei hadi tsh 900...bado hawakupata soko..wakaamua mzigo urudi kiwandani Moshi huko nako wakatangaza bei ya tsh 900 ikashindikana..uamuzi wao wa mwisho ukawa ni kuwateketeza kwa moto mkali!

Tuiombe serikali kitengo cha watu wa mifugo au kama bado ipo taasisi ya kutetea wanyama iwafuatilie wamiliki wa kiwanda hiki na ikibidi wachukuliwe hatua kali ili iwe onyo kwa wengine watakaofikiria kufanya upuuzi huu.maana mkurugenzi wao ameshasema kuwa vifaranga wengine laki nane na nusu wanatarajiwa hivi karibuni na hajui pa kuwapeleka.

Nimejiuliza kwanini basi hata huku Dar na Moshi wasivigawe kwa mtu yeyote atakayeweza kutunza?hata kama mtu angechukua 20 mwingine box 4,mwenye vifaranga 60 nk wangetangaza tu hadharani..au kuwatangazia hata majeshini,vyuoni pengine wangejaribu kuwakuza vifaranga hao wa nyama na mayai.

Nimalizie kwa kusema kitendo kile ni cha kishetani na hakina budi kulaaniwa na serikali ichukue hatua stahiki na hili lisijirudie.

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Wapumbavu wa CHADEMA NA TEAM SAMIA wanasema ni marehemu Magufuli ndiyo kachoma hata hao vifaranga mbona uchomaji wa vifaranga umekuwepo tz awamu zote za maraisi isipokuwa nyerere hata kipindi cha mwinyi vifaranga vinatupwa kwa kuchomwa kwa sababu mbalimbali ikiwemo magonjwa. Ndiyo maana mimi nikimsikia huyu juwa wa kizanzibar anapo ponda kuchomwa vifaranga kipindi cha JPM mimi namwona ni mpumbavu as usual.maana kwenye viwanda vya kuzalisha vifaranga uchomaji ni jambo la kawaida kabisa hsta hapa interchick vinachomwagwa sana tu.
 
Back
Top Bottom