Utawala wa Taliban umetangaza wanafunzi wa kike wataruhusiwa kuhudhuria masomo endapo tu watatenganishwa na wa kiume

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,499
9,279
Baadhi ya vyuo vikuu vya umma nchini Afghanistan vimenguliwa tena kwa mara ya kwanza tangu kundi la Taliban lilipochokua madarakani mwezi Agosti.

Utawala wa Taliban umetangaza kuwa wanafunzi wa kike wataruhusiwa kuhudhuria masomo. Lakini endapo tu watatenganishwa na wanafunzi wa kiume na mtaala utafuata kanuni za Kiislamu. Nchi mbalimbali duniani zilishinikiza Taliban kuruhusu elimu kwa watoto wa kike, kama sharti la kupewa misaada ya kiutu.

Jumuiya ya kimataifa imekuwa ikifuatilia kwa karibu endapo utawala huo mpya ungeanzisha sheria kali kama ilivyokuwa wakati wa utawala wake katika miaka ya 90. Sheria hizo ziliwazuia wasichana kupata elimu na wanawake kufanya kazi.

Chini ya utawala wa Taliban, wanafunzi wa kiume watahudhuria masomo asubuhi na wa kike mchana ili kuendana na mfumo wa kutenganisha jinsia.
 
Kibinyo Cha kiuchumi ambacho Taaliban imewekewa na Marekani ni kikali Sana,Si URUS Wala China ambaye Yuko tayari kusaidia. Mwisho wa Siku wataachana na misimamo yao TU.

Hakuna mwenye njaa mwenye msimamo,siku njaa ikimkaba lazima ataukana msimamo wake.

Taaliban wako GENEVA kwenye Mazungumzo na Marekani ili walegezewe kibano. Bila Kibano Nani angelijaribu hata kuthubutu kuwaita Taaliban waje kwenye meza ya Mazungumzo? Leo njaa ipo kooni wao wenyewe wanaomba Mazungumzo. TIME WILL TELL.

Kinachofuta Taaliban watapewa masharti ya kuandaa uchaguzi wa Kidemokrasia ili walegezewe vikwazo na Marekani.
 
Kibinyo Cha kiuchumi ambacho Taaliban imewekewa na Marekani ni kikali Sana,Si URUS Wala China ambaye Yuko tayari kusaidia. Mwisho wa Siku wataachana na misimamo yao TU...
Lakini hiyo haiondoi ukweli kwamba last year kila mtu alishuhudia Wamarekani wakifurumshwa huko Middle East. Usilisahau hilo.
 
Lakini hiyo haiondoi ukweli kwamba last year kila mtu alishuhudia Wamarekani wakifurumshwa huko Middle East. Usilisahau hilo.
Labda wewe ndio nikukumbushe kuwa Kila rais wa Marekani kwenye kampeni zake alikuwa anajichukulia point za kisiasa kwa kusema atawarejesha nyumbani Wanajeshi wa Marekani walioko Syria na Afghanistan. Alianza Obama mwaka 2013 lakini akakosolewa na wabunge wa Republican mwishowe akaacha. Alikuja Trump ndio akaweka mkataba wa jinsi ya kuyaondoa Majeshi ya Marekani na Serikali ya Afghanistan. Trump aliahidi kuwaondoa Wanajeshi wa Marekani nchini Afghanistan katika kipindi chake Cha PILI Madarakani. Bahati mbaya Trump hakushinda,alipokuja Biden akaendelea na ule mkataba na HATIMAYE akayaondoa Majeshi ya Marekani tarehe 31 mwezi wa 8 mwaka 2021.

Sasa unaposema Marekani alifurushwa na Taliban nashindwa kuelewa wewe ni mtu wa Aina gani. Kwamba ULIKUWA haufuatilii Siasa za Marekani kutaka kujiondoa Afghanistan au?
 
Labda wewe ndio nikukumbushe kuwa Kila rais wa Marekani kwenye kampeni zake alikuwa anajichukulia point za kisiasa kwa kusema atawarejesha nyumbani Wanajeshi wa Marekani walioko Syria na Afghanistan. Alianza Obama mwaka 2013 lakini akakosolewa na wabunge wa Republican mwishowe akaacha. Alikuja Trump ndio akaweka mkataba wa jinsi ya kuyaondoa Majeshi ya Marekani na Serikali ya Afghanistan. Trump aliahidi kuwaondoa Wanajeshi wa Marekani nchini Afghanistan katika kipindi chake Cha PILI Madarakani. Bahati mbaya Trump hakushinda,alipokuja Biden akaendelea na ule mkataba na HATIMAYE akayaondoa Majeshi ya Marekani tarehe 31 mwezi wa 8 mwaka 2021.

Sasa unaposema Marekani alifurushwa na Taliban nashindwa kuelewa wewe ni mtu wa Aina gani. Kwamba ULIKUWA haufuatilii Siasa za Marekani kutaka kujiondoa Afghanistan au?
Wamarekani eikeiei ^wababe wa vita vya kigaidi,^ hawakuwa na jinsi wala hawakuweza kufurukuta mbele ya Tajiban. They can only mess with weak nations such as Mexico and Venezuela.
 
Kibinyo Cha kiuchumi ambacho Taaliban imewekewa na Marekani ni kikali Sana,Si URUS Wala China ambaye Yuko tayari kusaidia. Mwisho wa Siku wataachana na misimamo yao TU.

Hakuna mwenye njaa mwenye msimamo,siku njaa ikimkaba lazima ataukana msimamo wake.

Taaliban wako GENEVA kwenye Mazungumzo na Marekani ili walegezewe kibano. Bila Kibano Nani angelijaribu hata kuthubutu kuwaita Taaliban waje kwenye meza ya Mazungumzo? Leo njaa ipo kooni wao wenyewe wanaomba Mazungumzo. TIME WILL TELL.

Kinachofuta Taaliban watapewa masharti ya kuandaa uchaguzi wa Kidemokrasia ili walegezewe vikwazo na Marekani.
hakuna kibinyo , taliban na USA ni kitu kimoja tu , zile zilikuwa ni ajenda za kuingia madarakani mfadhili akiwa USA ambae alijikuta rafiki wa serikali ili awe anajipatia siri za serikalin , Wangekuwa maadui wasingekaa meza moja kudiscus hizo inshu , USA ndo alililiunda hiko kundi kupigania maslai yake pale anapopishana na serikali halali
 
Wamarekani eikeiei ^wababe wa vita vya kigaidi,^ hawakuwa na jinsi wala hawakuweza kufurukuta mbele ya Tajiban. They can only mess with weak nations such as Mexico and Venezuela.
Mmarekani ndio mfadhili wa kile kikundi , hayo mengine ni miigizo tu .
 
Labda wewe ndio nikukumbushe kuwa Kila rais wa Marekani kwenye kampeni zake alikuwa anajichukulia point za kisiasa kwa kusema atawarejesha nyumbani Wanajeshi wa Marekani walioko Syria na Afghanistan. Alianza Obama mwaka 2013 lakini akakosolewa na wabunge wa Republican mwishowe akaacha. Alikuja Trump ndio akaweka mkataba wa jinsi ya kuyaondoa Majeshi ya Marekani na Serikali ya Afghanistan. Trump aliahidi kuwaondoa Wanajeshi wa Marekani nchini Afghanistan katika kipindi chake Cha PILI Madarakani. Bahati mbaya Trump hakushinda,alipokuja Biden akaendelea na ule mkataba na HATIMAYE akayaondoa Majeshi ya Marekani tarehe 31 mwezi wa 8 mwaka 2021.

Sasa unaposema Marekani alifurushwa na Taliban nashindwa kuelewa wewe ni mtu wa Aina gani. Kwamba ULIKUWA haufuatilii Siasa za Marekani kutaka kujiondoa Afghanistan au?
Elewa kwamba huyo unayemjibu ndio Isis wenyewe.
 
Mmarekani ndio mfadhili wa kile kikundi , hayo mengine ni miigizo tu .
Uko sahihi

Marekani alichokozwa na magaidi wa Afghanistan walkiongozwa na Osama wakalipua Trade center kule marekani

Marekani akaingia vitani kupigana nao akawatwanga kweli kweli akaona imetosha sasa naondoka nafadjili vikundi vya waasi waendelee kutwangana ndani na kulipuana wao kwa wao

Yeye kaondoka vita inaendelea ya wao kwa wao

Ndicho alichofanya hata Somalia

Sasa hivi wananyukana wenyewe kwa wenyewe. mnarekani aliwatwanga kipindi halafu Hugo akasema naondoka zangu watu wakasema ohhh mmarekani kashindwa vita Somalia kumbe yeye ndie mshindi hadi Leo Somalia hawajui amani in kutwangana usiku na mchana .Mission accomplished

Afghanistan watatwangana mpaka wakome wao kwa wao
 
Wamarekani eikeiei ^wababe wa vita vya kigaidi,^ hawakuwa na jinsi wala hawakuweza kufurukuta mbele ya Tajiban. They can only mess with weak nations such as Mexico and Venezuela.
Waliamua kuacha tu vinginevyo wangekua na interests pangewakaa kutokea angani
 
Back
Top Bottom