Utawala wa Rais Magufuli ni kiboko, bado wiki mbili mwaka wa fedha kuisha, mwendo ni uleule

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
8,708
5,711
Unaweza ukasema labda ni miujiza maana hii sio kawaida kwa serikali nyingi za Kiafrika. Maana pale bunge la bajeti linapoanza kukaa serikali nyingi huwa zimeishiwa pesa na nyingi huwa zimesimamisha shughuli za kimaendeleo ili kusubiri mwaka mpya wa fedha uanze.

Lakini kwa John Pombe Magufuli hili ni habari nyingine. Tayari alikuwa ameshajenga hospitali za wilaya 67 na zimeshakamilika. Sasa tayari ameshatoa pesa kwa ajili ya ujenzi wa hospital zingine 31 za wilaya ili zianze kujengwa. Moja ya wilaya zilizonufaika na mgao huo wa pesa ni wilaya ya Misungwi na Sengerema.

Kwa wapinzani hii ni dhahiri kuwa CCM na serikali yake chini ya JPM wamejipanga kuwatumikia wananchi. Na mnatakiwa mkubali kuwa rushwa na ubadhilifu vimedhibitiwa ndio maana serikali inakuwa na pesa za kutekeleza miradi hata kama tunaelekea ukingoni mwa mwaka wa fedha.

Na kwa mantiki hii, nawasihi wapinzani muache maigizo ya kutangaza nia ya kugombea urais. Ubunge na udiwani jaribuni japokuwa ni kijani tu ndio wengi watarudi.
 
Alivyowafanyia watumishi hakika Mungu yupo. Miaka yote 5 ni kapa huku wakidhalilika kwa hali ngumu ya maisha huko mtaani. Poleni walimu, madaktari, wauguzi etc.
 
Hivi nyongeza ya kila mwaka hakuna? Mbona watu wanapandishwa madaraja kila mwaka. Au unazungumzia nyongeza ya kima cha chini?
Madaraka ambayo mishahara yake hailipwi ni sawa na hujapanda daraja! Just imagine mtumishi amepanda daraja tangu 2017 na hajarekebishiwa mshahara Hadi leo, Hilo daraja Lina maana kwake?.

Kwa wachache waliobadilishiwa mishahara mwaka 2019 hawajalipwa arrears zao Hadi leo! Kisha ccm mnajisifu hapa kwa kujaza vifusi mabarabarani na kujenga dispensaries ambazo hazitakuwa na waganga.

Wala wauguzi kwani hamjawaajiri! Hakuna mtanzania mjinga kwa Sasa mkae mkijua hivyo!
Na huduma za kijamii ni haki ya wananchi na sio zawadi!.
 
Umaskini umeongezeka, unemployment rate ipo juu, biashara nyingi zmekufa, kahamisha mapato kutoka Local Gvt kapeleka Central Gvt then mnapiga makofi waaaa waaaa waaa mapato yameongezeka,

Miradi mikubwaaa pesa za mkopo tena mikopo ya kibiashara mnapiga makofi waaa waaa waaa,

Bajeti haijawahi fikiwa hata 80% mnapiga makofi pwaaa pwaaa pwaaa tupo vizuri,
Unashindana huku mpinzani wako umemfunga minyororo na pingu, unashinda then mnapiga makofi pwaaa pwaaa pwaaa tumeshinda kwa kishindo.

Pesa za walipa kodi zinatumiwa hovyo bila hata kupangiwa bajeti na zingne zinayeyuka tu, mnapiga makofi pwaaa pwaa pwaa ufisadi umeisha awamu hii mafisadi wote tumefyekelea mbali.

Watu wasiojulikana wanateka na kuua wapinzani wenu mnapiga makofi waaa waaa waaa usalama umeimarika awamu hii toka tupate uhuru.

Mtu anavunja katiba wazi wazi anavyojisikia mnapiga makofi pwaaa pwaa pwaaaa awamu hii ni ya utawala bora haijawahi kutokea.

Mnaminya vyombo vya habari mnataka muwe mnasifiwa na kusikika nyie tu mnapiga makofi pwaaa pwaa pwaaa sisi tunapendwa wananchi wanatupenda sana.

Kuna kiazi anawaza tutafika uchumi wa kati na Tanzania ya viwanda ifikapo 2022. Ndoto Nyevu hizi..
 
Madaraka ambayo mishahara yake hailipwi ni sawa na hujapanda daraja! Just imagine mtumishi amepanda daraja tangu 2017 na hajarekebishiwa mshahara Hadi leo, Hilo daraja Lina maana kwake? Kwa wachache waliobadilishiwa mishahara mwaka 2019 hawajalipwa arrears zao Hadi leo! Kisha ccm mnajisifu hapa kwa kujaza vifusi mabarabarani na kujenga dispensaries ambazo hazitakuwa na waganga Wala wauguzi kwani hamjawaajiri! Hakuna mtanzania mjinga kwa Sasa mkae mkijua hivyo!
Na huduma za kijamii ni haki ya wananchi na sio zawadi!
Mimi naongelea ukweli tu. Kuna jamaa yangu anasema kweli zilichelewa. Ila baada ya zoezi la vyeti feki na wafanyakazi hewa kuisha walilipwa. Na hazina ilitoa orodha ya watumishi wote wanaostahili kulipwa. Sasa labda system inabagua?
 
Mimi naongelea ukweli tu. Kuna jamaa yangu anasema kweli zilichelewa. Ila baada ya zoezi la vyeti feki na wafanyakazi hewa kuisha walilipwa. Na hazina ilitoa orodha ya watumishi wote wanaostahili kulipwa. Sasa labda system inabagua?
Ondoa labda ili statement yako iwe valid! Vinginevyo utakuwa sawa na mwenye kijiwe Cha kahawa asiyeweza kuzithibitisha hoja zake kwa kuwa na ushahidi maridhawa! Na kwanini wabague? Au wanaoliopwa ni wa CCM?
 
Umaskini umeongezeka, unemployment rate ipo juu, biashara nyingi zimekufa, kahamisha mapato kutoka Local Gvt kapeleka Central Gvt then mnapiga makofi waaaa waaaa waaa mapato yameongezeka.

Miradi mikubwaaa pesa za mkopo tena mikopo ya kibiashara mnapiga makofi waaa waaa waaa.

Bajeti haijawahi fikiwa hata 80% mnapiga makofi pwaaa pwaaa pwaaa tupo vizuri.
Unashindana huku mpinzani wako umemfunga minyororo na pingu, unashinda then mnapiga makofi pwaaa pwaaa pwaaa tumeshinda kwa kishindo.

Pesa za walipa kodi zinatumiwa hovyo bila hata kupangiwa bajeti na zingne zinayeyuka tu, mnapiga makofi pwaaa pwaa pwaa ufisadi umeisha awamu hii mafisadi wote tumefyekelea mbali

Watu wasiojulikana wanateka na kuua wapinzani wenu mnapiga makofi waaa waaa waaa usalama umeimarika awamu hii toka tupate uhuru.

Mtu anavunja katiba wazi wazi anavyojisikia mnapiga makofi pwaaa pwaa pwaaaa awamu hii ni ya utawala bora haijawahi kutokea.

Mnaminya vyombo vya habari mnataka muwe mnasifiwa na kusikika nyie tu mnapiga makofi pwaaa pwaa pwaaa sisi tunapendwa wananchi wanatupenda sana.

Kuna kiazi anawaza tutafika uchumi wa kati na Tanzania ya viwanda ifikapo 2022. Ndoto Nyevu hizi..
Hizi hoja ni lazima ang'ang'anie maisha, maana hawezi ishi bila kuabudiwa
 
Back
Top Bottom