Utawala wa Rais Magufuli ni dalili ya wakati muafaka kwa Vyama vya Upinzani kuungana na kuwa chama kimoja

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Kuna filosofia ya kuunganisha makundi ya watu hata wasiopatana inayoitwa "uniting to face a common enemy" ambayo hutumika sana katika mambo ya utawala.

Nina ushauri mmoja kwa Chadema na vyama vyote vya upinzani nchini, kwamba huu utawala wa Raisi Magufuli katika awamu ya tano ya uongozi na iwe kichocheo kikubwa kwenu kuweka tofauti zenu pembeni na kuwa chama kimoja cha upinzani nchini ili kukabiliana na Raisi Magufuli na chama chake cha CCM. Chadema kama chama kikuu cha upinzani lifanyeni hili kwa busara na hekima.

Raisi Magufuli na CCM wamekuwa mwiba mchungu kwenu nyote watu wa upinzani, tumieni nafasi hiyo kama factor ya kuwaunganisha pamoja. Mkiwa hamjaungana, angalieni wanavyowafanya Chadema. Angalieni wanavyowafanya ACT. Angalieni walivyowafanya CUF. Angalieni walivyowafanya TLP, nk.

Raisi Magufuli anatumia kuendelea kwenu kutokuwa kitu kimoja kuwabomoa na kuwadhoofisha, mara nyingine hata akipandikiza migongano kati yenu kwa kumsifia huyu na kumkashifu yule, na hata kuwateua baadhi yenu au kuwatia ndani bila sababu za msingi akijua hamna nguvu ya pamoja.

Angalieni kwamba mkiungana sasa mtakuwa na nguvu kubwa sana ya kukabiliana na Raisi Magufuli na chama chake CCM, na sauti yenu itakuwa kubwa zaidi ndani na nje ya nchi. Magufuli na CCM wataanza kuwaogopa. Msipoungana katika muda huu wa utawala wa Magufuli, kuna baadhi ya vyama vyenu na viongozi wenu mtadhoofika huenda hata kufa kisiasa.

Sasa ni wakati muafaka wa vyama vya upinzani nchini kuungana, angalau hata kuongea juu ya kuungana kuwa chama kimoja chenye nguvu. Sahau UKAWA, wekeni ubinafsi pembeni (self interest) unganeni na kuanzisha chama kimoja cha siasa.
 
Tatizo tofauti na Chadema hao wapinzani wengine ni akina nani,au ndo hao akina Cheyo,Mrema,Lipuuuu n.k Labda Zitto kidogo naanza kumwona kama zinamrudirudi.
Mkuu katika kuungana, sio lazima viongozi wote wa vyama vya upinzani wawe upande wa upinzani. Kuna baadhi yao, huenda hao uliowataja, itakuwa nafasi muafaka kwao pia kuonyesha true colours zao na kujiunga na CCM.

Kumbuka muungano wa vyama vya upinzani kuwa chama kimoja utatoa nafasi ya watu kuamua eidha kubaki upinzani au kwenda CCM.
 
Sheria hairuhusu kuunganisha vyama, wengi bado hamumuelewi msomi Nyalandu ni kwa nini anaitaka ile rasimu ya Warioba irudishwe tupate katiba mpya, sauti halisi ya wananchi ipo mule, hata Humfrey Polepole wa zamani analijuwa hilo vizuri sana kuliko mwenyekiti wake wa sasa.
 
Kuna filosofia ya kuunganisha makundi ya watu hata wasiopatana inayoitwa "uniting to face a common enemy" ambayo hutumika sana katika mambo ya utawala.

Nina ushauri mmoja kwa Chadema na vyama vyote vya upinzani nchini, kwamba huu utawala wa Raisi Magufuli katika awamu ya tano ya uongozi na iwe kichocheo kikubwa kwenu kuweka tofauti zenu pembeni na kuwa chama kimoja cha upinzani nchini ili kukabiliana na Raisi Magufuli na chama chake cha CCM. Chadema kama chama kikuu cha upinzani lifanyeni hili kwa busara na hekima.

Raisi Magufuli na CCM wamekuwa mwiba mchungu kwenu nyote watu wa upinzani, tumieni nafasi hiyo kama factor ya kuwaunganisha pamoja. Mkiwa hamjaungana, angalieni wanavyowafanyaChadema. Angalieni wanavyowafanya ACT. Angalieni walivyowafanya CUF. Angalieni walivyowafanya TLP, nk.

Raisi Magufuli anatumia kuendelea kwenu kutokuwa kitu kimoja kuwabomoa na kuwadhoofisha, mara nyingine hata akipandikiza migongano kati yenu kwa kumsifia huyu na kumkashifu yule, na hata kuwateua baadhi yenu au kuwatia ndani bila sababu za msingi akijua hamna nguvu ya pamoja.

Angalieni kwamba mkiungana sasa mtakuwa na nguvu kubwa sana ya kukabiliana na Raisi Magufuli na chama chake CCM, na sauti yenu itakuwa kubwa zaidi ndani na nje ya nchi. Magufuli na CCM wataanza kuwaogopa. Msipoungana katika muda huu wa utawala wa Magufuli, kuna baadhi ya vyama vyenu na viongozi wenu mtadhoofika huenda hata kufa kisiasa.

Sasa ni wakati muafaka wa vyama vya upinzani nchini kuungana, angalau hata kuongea juu ya kuungana kuwa chama kimoja chenye nguvu. Sahau UKAWA, wekeni ubinafsi pembeni (self interest) unganeni na kunzisha chama kimoja cha siasa.
Mbona CHADOMO imeshapauka.....kwani USAJILI wao ni wale wale waliokuwa kule ndio wanarudi kwa njia mbadala....Nyalandu mgombea URAIS CHADEMA 2020.....
 
VYAMA VYA WAPINZANI VYA KUUNGANA VIPO WAPI.WAKIUNGANA CUF LIPUMBA, ACT ZITO UTAPATA NINI HAPO LABDA ACT BILA ZITO NA CUF BILA LIPUMBA
 
Sheria hairuhusu kuunganisha vyama, wengi bado hamumuelewi msomi Nyalandu ni kwa nini anaitaka ile rasimu ya Warioba irudishwe tupate katiba mpya, sauti halisi ya wananchi ipo mule, hata Humfrey Polepole wa zamani analijuwa hilo vizuri sana kuliko mwenyekiti wake wa sasa.
Mkuu sheria inaweza isiruhusu kuunganisha vyama moja kwa moja, lakini hilo haliwezi kuwa tatizo. Tunapoongelea vyama kuungana kimsingi tunamaanisha vyama kujiua na kuungana katika kuanzisha chama kimoja.
 
VYAMA VYA WAPINZANI VYA KUUNGANA VIPO WAPI.WAKIUNGANA CUF LIPUMBA, ACT ZITO UTAPATA NINI HAPO LABDA ACT BILA ZITO NA CUF BILA LIPUMBA
Ndipo kile nilichosema kuwa kwanza lazima wajitafakari juu ya kuweka self interest pembeni. La sivyo hawatafanikiwa hata siku moja.

Na kuweka self interest pembeni ni kujiendesha katika misingi ya demokrasia. Mkitaka mwenyekiti - amueni kwa kura. Na ijulikane Mwenyekiti atapewa nafasi ya kwanza kuwa mgombea uraisi. Ni baadhi ya mambo wanayoweza kuweka kwenye katiba ya chama.

Amini nakuambia, ni heri kuungana kuliko kufishwa na Magufuli.
 
U
Ndipo kile nilichosema kuwa kwanza lazima wajitafakari juu ya kuweka self interest pembeni. La sivyo hawatafanikiwa hata siku moja.

Na kuweka self interest pembeni ni kujiendesha katika misingi ya demokrasia. Mkitaka mwenyekiti - amueni kwa kura. Na ijulikane Mwenyekiti atapewa nafasi ya kwanza kuwa mgombea uraisi. Ni baadhi ya mambo wanayoweza kuweka kwenye katiba ya chama.

Amini nakuambia, ni heri kuungana kuliko kufishwa na Magufuli.
upo sahihi mkuu
 
Mkuu sheria inaweza isiruhusu kuunganisha vyama moja kwa moja, lakini hilo haliwezi kuwa tatizo. Tunapoongelea vyama kuungana kimsingi tunamaanisha vyama kujiua na kuungana katika kuanzisha chama kimoja.
Kwa msajili huyu tulienae unaweza anzisha chama kama kinatishia uhai wa CCM basi kamwe hakiwezi kupata usajili wa kudumu
 
Lowassa alienda CHADEMA kwa mbwembwe kwamba kuna theluthi ya CCM inamfuata bado akaambulia kura chini ya 40%.
Uzuri kwa wanaohama CCM leo hii ni kwamba Mrema bado yupo hai.
 
Back
Top Bottom