GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,546
- 108,877
Umeshasema kuwa mwisho wa Wamachinga kuwa maeneo wasiyotakiwa ni tarehe 18 Oktoba, 2021 kwanini tena msogeze Siku mpaka tarehe 30 au 31 Oktoba, 2021?
GENTAMYCINE nachukia Watu (hasa Watawala) wasio na 'Misimamo' na wanakuwa 'Kigeugeu' katika ama Matamko au Mwamuzi yao.
Kama mnadhani hii 'Huruma' yenu ya 'Kinafiki' dhidi ya Wamachinga kwa Kuwaongezea Siku zaidi za Kuhama imewapa 'Credits' za Kisiasa na Kiutawala bali nawataarifu kuwa sasa ndiyo imewafanya 'Mdharaulike' na muonekane Wapuuzi na Waswahili.
Serikali makini haipendwi wala haisifiwi na Wananchi kwa kuwaonea Huruma Kinafiki bali ni kwa kuwa na Msimamo huku ikisimamia taratibu, nidhamu na Misingi iliyopo au iliyowekwa.
Nina uhakika Serikali juzi ile ile (ya Ukomo wao waliouweka) wangeamua 'Kubomoa' na Kuwaondoa Wamachinga maeneo wasiyotakiwa ingeheshimika, ingeogopeka na isingeoneka ni Lege Lege (Ndembe Ndembe) na iliyojaa 'Undumilakuwili' mwingi.
Upuuzi huu huwezi Kuukuta kwa Mataifa yaliyo 'Serious' kama ya Israel, Korea Kaskazini, Rwanda, Urusi, Cuba na China. Serikali haitakiwi izoeleke hovyo na Wananchi bali isimamie Kanuni na Miongozo iliyopo Kikatiba au Kisheria.
Subirini GENTAMYCINE ndoto yangu ya kuja kuwa Rais wa Tanzania itimie mbona mtanitambua na mtanyooka Wenyewe. Sitokuwa na Huruma Wala Upendeleo kwa Watu, Ndugu zangu na Marafiki bali nitafuata Katiba na Utaratibu wa Kiutawala / Kiuongozi.
Mkidharauliwa mnatusema tunatumika.
GENTAMYCINE nachukia Watu (hasa Watawala) wasio na 'Misimamo' na wanakuwa 'Kigeugeu' katika ama Matamko au Mwamuzi yao.
Kama mnadhani hii 'Huruma' yenu ya 'Kinafiki' dhidi ya Wamachinga kwa Kuwaongezea Siku zaidi za Kuhama imewapa 'Credits' za Kisiasa na Kiutawala bali nawataarifu kuwa sasa ndiyo imewafanya 'Mdharaulike' na muonekane Wapuuzi na Waswahili.
Serikali makini haipendwi wala haisifiwi na Wananchi kwa kuwaonea Huruma Kinafiki bali ni kwa kuwa na Msimamo huku ikisimamia taratibu, nidhamu na Misingi iliyopo au iliyowekwa.
Nina uhakika Serikali juzi ile ile (ya Ukomo wao waliouweka) wangeamua 'Kubomoa' na Kuwaondoa Wamachinga maeneo wasiyotakiwa ingeheshimika, ingeogopeka na isingeoneka ni Lege Lege (Ndembe Ndembe) na iliyojaa 'Undumilakuwili' mwingi.
Upuuzi huu huwezi Kuukuta kwa Mataifa yaliyo 'Serious' kama ya Israel, Korea Kaskazini, Rwanda, Urusi, Cuba na China. Serikali haitakiwi izoeleke hovyo na Wananchi bali isimamie Kanuni na Miongozo iliyopo Kikatiba au Kisheria.
Subirini GENTAMYCINE ndoto yangu ya kuja kuwa Rais wa Tanzania itimie mbona mtanitambua na mtanyooka Wenyewe. Sitokuwa na Huruma Wala Upendeleo kwa Watu, Ndugu zangu na Marafiki bali nitafuata Katiba na Utaratibu wa Kiutawala / Kiuongozi.
Mkidharauliwa mnatusema tunatumika.