issenye
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 3,781
- 5,205
kweli mambo yamebadilika. Wiki mbili zilizopita uzi kama huu usingedumu hata dakika kumi tu, ungeshafutwa.Huo ndio mtazamo wangu ukiniuliza juu ya utawala wa HayatiMagufuli.
Kaburi kilikuwa kikubwa aliogopewa na kila kiumbe Cha Tanzania alizungumzwa sirini watu waliogopa hata kuta za nyumba zao wakihisi magufuli atakuwa anawasikia.
Ufitinishi wa kina Cyprian Musiba ulifikia kiwango cha kutisha, Musiba aliweza kumfitini yeyote na wakati wowote bila woga akijua kwamba genge lao ndio lenye sheria na bosi wao ndio sheria yenyewe aliamua nani atoweshwe nani akirimiwe.
Kina Makonda waliishi kama miungu watu, kina Polepole walijirekodi mpaka video wakicheza kwa kejeli kwenye mazulia mekundu kwenye majumba ya Serikali sisi wengine tulikaa kimya tukiamini mpanda ngazi hushuka.
Spika alimnyanyasa Lissu kama jambazi yaani Lissu alilia akanyamaza Mungu wake alimfuta machozi na nyie kina Ndugai mliyekuwa mnamtetemekea kafa sasa anaitwa mwendazake subirini na nyie mlipe yale mliyoyafanya enzi zenu mkiwa miungu watu.
Mama Samia Suluhu Hassan jitenge kabisa na hawa watu
Polepole
Cyprian Musiba
Bashiru Ally
Makonda
Ayoub Ryoba - Mkurugenzi wa TBC
Nk
Imeandikwa amelaaniwa amtegemeae binadamu.