Utawala wa CCM Unajifunza nini kutoka Sri Lanka?

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,759
71,139
Dunia nzima inaona yanayotokea huko Sri Lanka, nasi pia kama sehemu ya dunia tunayaona.

Yaliyotokea Sri Lanka kama kudorora uchumi, kupanda bei kwa bidhaa kwa kutisha, mikopo mikubwa isiyolipika na utawala wa kindugu ulioshindwa kuongoza nchi ndiyo yaleyale yanayotokea Tanzania chini ya CCM bila kuonyesha dalili za kujali.

Je Chama cha mapinduzi kilichoko madarakani kimejifunza nini toka huko Sri Lanka kwa yanayotokea? ambako nguvu ya umma imefanya hadi Rais amekimbia makazi yake (Ikulu) na wao kuiteka.

Ukiangalia sisi KUKOPA nje tunaona ni jambo la sifa, lakini kwa Sri Lanka waliokuwa wanaamini kama sisi TZ hilo limekuwa jambo lililoleta matatizo haya.

Je, CCM inaweza kutambua sasa kuwa ukopaji huu usio tumia maarifa waweza kuitumbukiza nchi kwenye majanga makubwa kama Sri Lanka?
 
Hatua za haraka kwa wenzetu zinachukuliwa. Jee hapa inawezekana?
20220711_082002.jpg
20220711_081902.jpg
 
Hatua za haraka kwa wenzetu zinachukuliwa. Jee hapa inawezekana?View attachment 2286822View attachment 2286824
Mkuu wa Majeshi wa Srilanka "Jeshi haiwezi kuingilia kati wala kuwapiga au kuwatawanya Wananchi kwa sababu wana haki kisheria kudai haki yao kwa njia ya maandamano ya amani bila kufanya uharibufu kazi yetu sio kupambana na raia bali kazi yetu ni kulinda mipaka ya nchi na kutoa misaada kwa wananchi pale panapokuwa kuna maafa ya matetemeko mafuriko N.k..

Ningependa kuwakumbusha kwamba nchi hii ni yetu sote msifanye uharibifu na msikubali kuwapa chance vibaka wakafanya uvunjifu wa amani uporaji kuvunja maduka na magari ya watu.
FB_IMG_1657519374169.jpg
 
Mkuu wa Majeshi wa Srilanka "Jeshi haiwezi kuingilia kati wala kuwapiga au kuwatawanya Wananchi kwa sababu wana haki kisheria kudai haki yao kwa njia ya maandamano ya amani bila kufanya uharibufu kazi yetu sio kupambana na raia bali kazi yetu ni kulinda mipaka ya nchi na kutoa misaada kwa wananchi pale panapokuwa kuna maafa ya matetemeko mafuriko N.k..

Ningependa kuwakumbusha kwamba nchi hii ni yetu sote msifanye uharibifu na msikubali kuwapa chance vibaka wakafanya uvunjifu wa amani uporaji kuvunja maduka na magari ya watu.View attachment 2286867
Kumbe inawezekana! Basi na sisi tukijifunza kuwa twaweza kuandamana bila kufanya uharibifu wala uporaji jeshi laweza kutulinda dhidi ya Policcm ambao wapo kwa ajili ya chama chao!
Hizi ni salamu kwake General Nkunda
 
Dunia nzima inaona yanayotokea huko Sri Lanka, nasi pia kama sehemu ya dunia tunayaona.
Yaliyotokea Sri Lanka kama kudorora uchumi, kupanda bei kwa bidhaa kwa kutisha, mikopo mikubwa isiyolipika na utawala wa kindugu ulioshindwa kuongoza nchi ndiyo yaleyale yanayotokea Tanzania chini ya CCM bila kuonyesha dalili za kujali.
Jee Chama cha mapinduzi kilichoko madarakani kimejifunza nini toka huko Sri Lanka kwa yanayotokea? ambako nguvu ya umma imefanya hadi Rais amekimbia makazi yake (Ikulu) na wao kuiteka.
Ukiangalia sisi KUKOPA nje tunaona ni jambo la sifa, lakini kwa Sri Lanka waliokuwa wanaamini kama sisi TZ hilo limekuwa jambo lililoleta matatizo haya.
Jee CCM inaweza kutambua sasa kuwa ukopaji huu usio tumia maarifa waweza kuitumbukiza nchi kwenye majanga makubwa kama Sri Lanka?
Katiba yetu inawalinda. Hakuna kitu wanaweza jifunza
 
Ikitokea bongo, basi vi poli si si emu vyetu vitajisikia raha kweli! Maana vitapiga watu virungu na kuua hovyo hovyo ili kukidhi tu matakwa ya mabwana zao si si emu.
 
Watanzania tuchukue hatua.wasiri lanka wametuonyesha njia kuwa umma ukiamua hakuna wa kuzuia.polisi watatupiga lakini mwisho wake tutawazidi nguvu na hapo tutakuwa tumeushinda huu unyonyaji wa nchi yetu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
..Jeshi la Srilanka lilipigana vita na waasi wa Tamil kwa muda wa miaka 26.

..Sasa nini kimepelekea jeshi lenye historia na rekodi ya mapambano lisiilinde serikali na kuiacha ianguke?
 
Sioni haja ya ku Comment humu maana tunafananisha vitu viwili tofauti sana.
 
Back
Top Bottom