Bill
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 8,075
- 8,108
Mbinguni Kuna utatu Mtakatifu unaofanya kazi yake kwa umoja na kupewa jina la MUNGU. Mungu Baba yupo katika kiti cha enzi, Mungu mwana anatuombea na alijidhihirisha kwa kufanyika mwili ili atuokoe, na Mungu Roho mtakatifu ambaye yupo nasi siku zote akituongoza kutenda yaliyo mema japo haonekani.
Vilevile hapa TZ kuna utatu unaofanya kazi zake kwa pamoja kila mmoja akiwa na Jukumu lake alilopewa. Huu umepewa Jina la MTANDAO. Kuna JK, EL na RA hawa kila mmoja analo jukumu lake kama ilivyo huko mbinguni kuleta ukombozi kwa nchi yetu. Lakini Huu utatu unaweza kweli kufanikisha hili.
JK yupo katika kiti cha enzi, yeye ndiye Baba wa Taifa, EL ndiye Mwana, anajidhihirisha kwetu kwa njia mbalimbali kila kukicha hakosa hata siku moja kujidhihirisha kwetu kwa njia ya redio, TV na magazeti. RA yeye haonekani ila yupo kati yetu kila siku, ni mshauri kwa njia ya vyombo vya habari especially magazeti na amekuwa akifanya kazi kubwa ya kutuongoza wananchi kuiona serikali inafanya kila lililojema katika kutuletea maisha bora kwa kila mTZ kwa kasi, nguvu na ari japo zimekuwa kuukuu sasa.
Je utatu huu utatufikisha unakotupelekea, nawauliza wana JF!!!!!
Vilevile hapa TZ kuna utatu unaofanya kazi zake kwa pamoja kila mmoja akiwa na Jukumu lake alilopewa. Huu umepewa Jina la MTANDAO. Kuna JK, EL na RA hawa kila mmoja analo jukumu lake kama ilivyo huko mbinguni kuleta ukombozi kwa nchi yetu. Lakini Huu utatu unaweza kweli kufanikisha hili.
JK yupo katika kiti cha enzi, yeye ndiye Baba wa Taifa, EL ndiye Mwana, anajidhihirisha kwetu kwa njia mbalimbali kila kukicha hakosa hata siku moja kujidhihirisha kwetu kwa njia ya redio, TV na magazeti. RA yeye haonekani ila yupo kati yetu kila siku, ni mshauri kwa njia ya vyombo vya habari especially magazeti na amekuwa akifanya kazi kubwa ya kutuongoza wananchi kuiona serikali inafanya kila lililojema katika kutuletea maisha bora kwa kila mTZ kwa kasi, nguvu na ari japo zimekuwa kuukuu sasa.
Je utatu huu utatufikisha unakotupelekea, nawauliza wana JF!!!!!