Utata waibuka TRA Arusha, Meneja aliyehamishwa agoma kuondoka

buswelu moja mdada ameshamaliza kujaribu kuficha madudu yake hapo Arusha au? Ni kidogo hajieoeei.. akivhunguzwa au lawama zikimjia asijiulize kwa kuonyesha kuna majambo.
 
hii mikazi ya serikali kuna mijitu ina wivu balaa, sasa dume zima unahangaika na mwana mama anayeshughulikia ishu zake binafsi za uhamisho ... Hebu acha majungu na roho za kutu na inaonekana kabisa mnafanya nae kazi ofisi moja
 
Hizi changamoto za kiutumishi ikiwemo maswala ya uhamisho zinawakumba watumishi wengi, kwa nini mnakomaa kumrusha huyo dada!? wana taratibu zao za kiutumishi za kushughulikia changamoto kama hizo zinapojitokeza
 
Walifanya sherehe kwa sababu ipi kati ya hizi?
1.aliwabana sana
2.alikuwa hajui kazi
3.alikuwa na makando kando
4.alikuwa na majungu
5.alikuwa mkali kazini
6.hakuwa na ushirikiano kazini
7.alikuwa anaendekeza mapenzi kazini
8.mshirikina kazini
9.mchelewaji kazini
10.mjivuni
11.mbaguzi
12.hana elimu
14.mla rushwa
15.mfujaji wa fedha
16. hazingatii maagizo toka juu
18.anawakandamiza walipa kodi
19.ana sura mbaya
20.anasura nzuri
21.anamiliki mali tofauti na kipato chake
au ni wivu wivu wivu tu nk,nk,nk.

Povu ruksa.
kuna wafanyakazi wamefanya sherehe huyu dada kuhamishwa
 
Mkuu,kila sifa mbaya wanampa Makonda tu?Na nzuri zote apewe.

Uhusiano binafsi wao ni juu yao na hauna tija kwa Taifa kama hauna maingiliano na maslahi ya Taifa.

Suala hili mamlaka italishughulikia kama kuna taratibu zilikiukwa kwa pande.

Hahahahaha.
Mbona uzi wa kuhusu huyo dada ulitoka tangia juzi.

Inademekana huyo dada ni chakula cha Bashite.
Bashite kamwqmbia atulie kwanza kwa sababu bashite alimiahidi kumleta DSM
 
Kama kweli anagoma naona mkuu anamchora tu. ..asome alama za nyakati. anaweza fanyiwa surprise...
 
Arusha watu wana hela zaid ya Kahama Mkuu,, na kuna mzunguko wa hela tofauti na kahama ,


Kahama ipo vizuri Mkuu lakini tukubali haifiki kwa Arusha jiji .
Soma takwimu za makusanyo ya kodi kiwilaya utaipata Kahama...
 
Yani kwa uzi huu natumai uyo Dada sasa hivi anaenda petrol station kujaza mafuta anaondoka arushakesho saa moja na nusu mkienda TRA kahama mtamkuta

Anabahati arusha kahama siyo mbali angetupwa songea uko alafu huu Uzi ukaja mda huu mungu wangu leo angeshinda anajihalishia tu
Hahahaaaaa sio songea tu pale mjini mbona angefurahi ila.ingesoma lituhi huko manda ndio ange isoma.gps vizuri
 
Why mnamuandama huyu dada???
Kiukweli tunamchoma hivihivi lakini MUNGU atamwokoa na uchochezi huu wa vidole vyetu! kapige kazi dogo kahama kuko vizuri tu! usiogope usijidanganye kuacha kazi kwa kutegemea labda vimiradi vya kuku inaweza kula kwako nenda kwanza kaa hata baada ya miezi sita ndo utafute alternative kwa amani na usalama zaidi.
 
Mwandishi wetu,Arusha

Sakata la aliyekuwa meneja msaidizi wa mamlaka ya mapato nchini(TRA) mkoani Arusha kitengo cha madeni ,Irene Hance kukataa uhamisho wa kwenda wilayani Kahama limechukua sura mpya mara baada ya mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi,Richard Kayombo kutamka ya kwamba taasisi hiyo inafuatilia suala hilo.

Kayombo,ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku chache mara baada ya mamlaka hiyo kuwabadilisha vigogo 34 wa mamlaka hiyo kwenye vituo vyao vya kazi nchi nzima muda mfupi baada ya Rais John Magufuli kumtumbua aliyekuwa kamishna mkuu wa mamlaka hiyo,Charles Kicheere.
View attachment 1143971View attachment 1143972View attachment 1143973View attachment 1143973View attachment 1143974View attachment 1143974
Takribani uhamisho huo ulipotoka wiki mbili zilizopoita Hance amekuwa akiendelea na kazi zake kama kawaida katika kituo chake cha Arusha huku wenzake wakiwa wamesharipoti katika vituo vyao vipya jambo ambalo limeibua utata ndani ya taasisi hiyo nyeti nchini.

Akihojiwa na waandishi wa habari hivi karibuni Kayombo alitamka kwamba suala la uhamisho wa watumishi wa TRA ni suala la ndani ya taasisi hiyo na sio mahali pengine.

“Suala hilo ni suala la kiutawala na wala sio mahali popote ,suala la uhamisho ni suala la ndani kama kuna ukiukwaji wowote tofauti na kinachotakiwa kufanyika basi tutaifahamisha jamii”alisema Kayombo

Hatahivyo,alisisitiza kwamba yeye binafsi anashindwa kuelewa ni kwanini suala la uhamisho wa watumishi wa TRA hususani mkoani Arusha limekuwa jambo zito kuliko mikoa mbalimbali nchini.

Wiki iliyopita meneja wa TRA mkoani Arusha,Faustine Mdesa alikaririwa na vyombo vya habari akitamka ya kwamba Hance sio mtumishi wake na tayari alishampatia barua ya uhamisho kwenda Kahama.

“Ninachotambua huyo sio mtumishi wangu kwani nilishampatia barua ya kwenda kwenye kituo chake kipya cha kazi ambacho ni Kahama siwezi kumzungumzia mtu ambaye sio mtumishi wangu”alikaririwa Mdesa

Suala la uhamisho wa Hance limeibua mkanganyiko ambapo mara kwa mara amekaririwa na vyombo vya habari akitamka ya kwamba tayari amesharipoti kwenye kituo chake kipya cha kazi wilayani Kahama tangu Juni 26 mwaka huu na anaendelea na majukumu yake ya kazi huku akionekana katika kituo chake cha zamani akiendelea na majukumu.

“Mwandishi nimesharipoti tangu Juni 26 mwaka huu kwenye kituo change kipya cha kazi na ninaendelea na majukumu yangu ya kazi Kahama”alikaririwa Hance

Kuhusu suala la kutamba mbele ya wafanyakazi wake kuwa hawezi kwenda Kahama kwa kuwa ana mahusiano mazuri na baadhi ya vigogo wa taasisi hiyo makao makuu Hance alisema kwamba hayo ni masuala ya kiofisi na kwamba hawezi kujibu chochote.

Hatahivyo,taarifa ambazo hazijathibitishwa rasmi zinadai kwamba leo Julai Mosi mwaka huu Hance hajaonekana ofisini na taarifa zinadai kwamba amefunga safari kuelekea makao makuu ya TRA kwa lengo la kutengeneza mazingira ya yeye kuendelea kubaki katika kituo chake cha kazi mkoani Arusha.

Mwisho.

Akihama au asipohama wewe mshahara utaongezeka? Kuna watu mmekaa kiumbea kufatilia maisha ya watu wengine tu
 
Je haki za wafanyakazi zinazingatiwa?.Mfanyakazi ni binadamu anaponyimwa haki zake zinashusha hari yake kufanya kazi.Kwa mfano unamuhamisha mfanyakazi huku akiacha familia inayomutegemea nyuma.Wafanyakazi wana haki zao tusizipuuze kwa kuwakomoa, kuwafokea,kuwatumbua bila kuwa na ushaidi wa kutosha nk
 
Kama kweli anagoma naona mkuu anamchora tu. ..asome alama za nyakati. anaweza fanyiwa surprise...
Acheni kumtisha....wengi humu hatujui exactly nini kimetokea...hata hivyo ana uhuru wa kuamua kwani hiyo kazi ni lazima?.......hata akiamua kuacha aache tu
 
Back
Top Bottom