MZEE MKUBWA
JF-Expert Member
- Jun 24, 2017
- 4,094
- 11,498
Kumbe Watu wasiojulikana wako toka kitambo
Mmh kaka umenishtua kidogo, inaonekana kuna kitu unakijua hebu funguka kidogo na wengine tupate kujua.
Mmmh yule wa temeke?Harooo usin'tanie!! Ina maana Mzee Kizota long time alikuwa Mjeda yule? Sa' yale manyama manyama aliyonayo na mengine yaliyojazana sehemu ya kukalia yametoka wapi yale? Au anaumwa?
Alifariki siku ya alhamisi kama Leo, kesho yake Ijumaa niligoma kwenda shule kwa huzuni niliyokuwa nayo. Nilikuwa darasa la 3.Mkubwa nakwambia umenikumbusha kitu gani tena? Usinilize Mkubwa! Nakumbuka kabisa mvua kubwa ilinyesha pasipo kukatika takrban masaa 7 na RTD enzi hiyo ambayo leo ndiyo TBC ikitangaza moja kwa moja mazishi yake!
Nilikuwa mdogo sana kwani nilikuwa darasa la kwanza ila nilikuja barabarani kuomboleza kifo ya shujaa huyo wa Tanzania mzalendo wa Nchi yetu!
Nakumbuka kabisa wanakijiji wote wababa kwa wamama walijitokeza barabarani na huku vijana karibu wengi wa kabla lake (Maasai) Morani wakiumiza miili yao kwa mori siku hiyo ya mazishi nilikuwa mdogo lakini sitokaa nikasahau msiba huu mchungu kwa Watanzania walio wengi kwa JEMBE huyo Marehemu Edward Moringe Sokoine.
Mwenyenzi MUNGU mwingi wa Rehema na ampe pumziko la milele shambani mwake Bwana wetu!
Ameeen!
Aliemgonga alichukuliwa hatua gani?
mkuu ina maana zamani viongozi walipokua katika misafara yao gari la kiongozi husika ndo lilikua linatangulia mbele?*UNDANI KIFO CHA SOKOINE*
WAZIRI Mkuu (sasa ni marehemu) Edward Moringe Sokoine alikuwa Dodoma kwenye kikao cha Bunge akiwa ni kiongozi wa shughuli za serikali na alimaliza kikao chake Aprili 11, 1984.
Aliandaliwa usafiri wa ndege ili asafiri na ujumbe wake wakati wa kurejea Dar es Salaam kuendelea na majukumu mengine ya kitaifa lakini alikataa.
“Safari hii sitaki kurudi Dar es Salaam kwa ndege, nataka kurudi kwa gari ili nione hali ya mazao ya wakulima njiani,” alikaririwa afisa mmoja wa Ikulu akimkariri Waziri Mkuu Sokoine mara baada ya kujulishwa habari ya usafiri wa kumrejesha Dar.
Aprili 12, 1984 msafara wake ulianza akitokea Dodoma huku ukisindikizwa na magari ya polisi na wana usalama wa taifa.
Msafara wake mchana ulipofika eneo la Wami mkoani Morogoro, jirani na palipojengwa makao makuu ya sasa ya Wilaya ya Mvomero, gari yake ilipata ajali kwa kugongwa na gari lingine aina ya Toyota Land Cruiser.
Sokoine alipofikishwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, madaktari walithibitisha kifo chake.
Rais (wa wakati huo), Mwalimu Julius Kambarage Nyerere siku hiyo majira ya jioni alilitangazia taifa kifo cha waziri mkuu wao. Mwalimu Nyerere, alishindwa kuhutubia kutokana na majonzi aliyokuwa nayo.
Miaka kumi baada ya kifo chache, daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa Sokoine baada ya kifo, aliweka wazi taarifa ya chanzo cha kifo chake.
Sehemu ya taarifa hiyo ilisema kuwa baada ya ajali, Sokoine alivunjika shingo ambayo ilisababisha kubana mishipa ya fahamu (spinal cord) ambayo ilikata mawasiliano kati ya ubongo na sehemu nyingine za mwili.
Kabla ya kifo chake, Sokoine alikuwa pia Mbunge wa Jimbo la Monduli na mwili wake ulizikwa huko kwa heshima zote za kiserikali, japokuwa mila za Kimasai pia zilipewa nafasi katika mazishi hayo.
Mahali alipopatia ajali Sokoine mara baada ya ajali hiyo panaitwa Wami Sokoine na pamejengwa mnara wa kumbukumbu ya kifo chake.
Maadhimisho ya miaka 34 ya kifo cha Hayati Edward Sokoine yanatarajia kufanyika April 12 Moringe Juu, Arusha. Kutakuwa na ibada maalum pamoja na fursa ya kutembelea kaburi la Sokoine. Tuungane kwa pamoja. Karibuni sana.View attachment 741015View attachment 741016
Bla blah na stori za sokoine zimekuwa nyingiIle audio wakati mwalimu anatangaza kifo si ipo?
Kwanini isingepandishwa hapa wote tukasikiliza?
Maana watu ni wazuri kuongeza maneno hivyo kupoteza uhalisia wa tukio
Mliokuwepo wekeni audio hapa kutoka Radio Tanzania Dar es Salaam tusikie tangazo live bila chenga