#COVID19 Utata wa chanjo ya UVIKO-19: Askofu Gwajima kutoa msimamo mwingine juu msimamo tarehe 1/8/2021

The Palm Tree

JF-Expert Member
Apr 13, 2013
7,951
12,535
Mtazame na msikilize mwenyewe ktk video hii. Yeye kauita huu wa kesho kuwa ni "msimamo juu ya msimamo"...

Hii ndiyo sauti ya "Jitu la Mbinguni" iliayo nyikani kusema itengenezeni njia ya Bwana maana ufalme wa Mwanakondoo upo duniani...!

Video na sauti yake itafuata.
 
hii nchi ni kama vile haina amiri jeshi mkuu, Gwajima kitendo anachokifanya hakina tofauti na muuwaji hakustahili mpaka muda huu kiwa uraiani
Toka lini maneno yakaua mtu? 😂😂😂 Huu ujinga ndio ulifanya awamu ya 5 ionekane awamu ya hovyo sana pamoja na kufungua wapinzani kila mara!
 
hii nchi ni kama vile haina amiri jeshi mkuu, Gwajima kitendo anachokifanya hakina tofauti na muuwaji hakustahili mpaka muda huu kiwa uraiani
Tanzania tumezoea kuzibwa midomo...acha aongee anachokiamini.

Btw, hujalazimishwa kuamini au kufuata anachosema, tatizo liko wapi?
 
Gwajima atumie lugha ya busara wakati wa kupinga chanjpo kuliko tuhuma za watu kughushi chanjo na kuwatisha watakufa kwa vile wanahamasisha chanjo.

Kimsingi Gwajima ana hoja nzuri na inayohitaji majibu makini ya kisayansi na siyo kejeli kama alivyo jibu Waziri Gwajima, na wala siyo majibu mepesi kama ya bosi wa waziri kwamba "chanjo tumeanza kuchanja toka tukiwa watoto kama za ndui, BCG.." .

Hizo chanjo nyingine zimechukua muda mrefu na takwimu za kutosha kuthibitisha ubora na usalama wake kwa watumiaji.

Pia hizo chanjo zimekuwa zikizuia kweli magonjwa husika yasiuwe au yasidhuru watumiaji wake, mambo ambayo chanjo za COVID19 zimeshindwa kufikia vigezo hivi.

Za COVID19 hazizuii maambukizo na vifo, bado hatujui madhara yake baada ya muda mrefu.
 
Mtazame na msikilize mwenyewe ktk video hii. Yeye kauita huu wa kesho kuwa ni "msimamo juu ya msimamo"...

Hii ndiyo sauti ya "Jitu la Mbinguni" iliayo nyikani kusema itengenezeni njia ya Bwana maana ufalme wa Mwanakondoo upo duniani...!

Video na sauti yake itafuata........
Huyu Gwajima ni wa kupigwa mawe hadi afariki
 
Back
Top Bottom