Utaratibu wa ulipaji hotel levy kwenye nyumba za kulala wageni Manispaa ya dodoma

h120

JF-Expert Member
Jan 10, 2012
2,530
3,315
Kwa wasiofahamu hotel levy ni ushuru wa nyumba za kulala wageni, mlipaji ni mmiliki wa biashara husika, na Ushuru huu unalipwa kwa kufuata Sheria ya nyumba za kulala Wageni(The Hotels Act) ya mwaka 1965 sura ya 105 kifungu cha 26 (2) pamoja na Marekebisho yake ya mwaka 2002 (The Hotel Act Wap. 105) toleo la mwaka 2002.

Kwa utaratibu unaotumika dodoma mjini naona ni mbovu na usio na tija sifahamu kama mikoa mingine wanatumia utaratibu wa aina hiyo, utaratibu uliopo kwa sasa ni wafanyakazi wa manispaa kutembelea kila nyumba ya kulala wageni nyakati za usiku kwa kushtukiza na kukagua kila chumba na idadi ya vyumba vyenye wateja na huzidishwa kwa 1000/=Tshs na kuchukua chao, je hamna utaratibu unaofaa juu ya kusimamia ukusanyaji wa haya mapato kwa njia nzuri zaidi.

Angalizo sipingani na matakwa ya sheria juu ya ukusanyaji wa hotel levy bali njia itumikayo kwa manispaa hiii.
Inawezekana pia utaratibu unaotumika ni sahihi zaidi labda uelewa wangu ni finyu juu ya hili jambo. Naomba tujadili kwa kina je huu utaratibu huu ni sahihi na wenye tija au unapaswa kurekebishwa.
Karibuni.
 
Kwa staili iyo wanawakosea sana, utaratibu ambao baadhi ya mikowa kufanya ni wa kistahatabu sana, kwamba baada ya siku 30 tunampeleka mahali usika kilabu chako cha kuandikisha wageni waliokuwa wanaingia hotelini au guest house km ni manispa au jiji, basi wanakikagua na kufanya mahesabu yao na kisha kukupa viwango cha kwenda kulipa kwa mujibu wa sheria na taratibu zao.
Ivyo ndivyo tunavyofanya uku kwetu Mwaz na siyo kuvamia nyakati za usiku km wezi
 
Hao ni wajinga... Sasa kwa mtindo huo watavamia hotel/guest ngapi kwa usiku mmoja? Njia sahihi na iliyo bora ni guests register na kitabu cha receipt/EFD machines kukaguliwa na mamlaka husika then wanakokotoa hotel levy.
 
Mkurugenzi wa Manispaa ya DDM kusema kweli anaharibu sana na sijui kama kuna tija wala kitakachoendelea chini ya utawala wake. Ni ubabe tena wa kitoto kwelikweli.
 
Naona wakuu munazungumzia upande mmoja tu wa Manispaa bila upande wa Wafanyabiashara ambao wamekuwa hawatumii vitabu vya Register kwa mgeni anayelala hata Risiti hawatoi me nilishadai risiti Hotel moja hapo Dom ilibidi ikafuatwe nyumbani mtu kama huyu unamtoza vipi Ushuru wa Hotel levy kama sio kumshtukiza inatakiwa Watanzania tubadilike.
 
Back
Top Bottom