Utaratibu wa pande nyingi unaotetewa na China unahakikisha Afrika inapata haki katika sekta ya afya

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,000
1,019
1eab10137d50a9a8200e5a2712a0cc32_1054_585.jpg


Tarehe 17, Juni mwaka 2020, mkutano wa kilele wa mshikamano dhidi ya COVID-19 kati ya China na Afrika ulifanyika, ambapo rais Xi Jinping wa China alitoa pendekezo la “kujenga jumuiya yenye hatma ya pamoja katika sekta ya afya kati ya China na Afrika”. Katika mwaka mmoja uliopita, China imekuwa ikizisaidia nchi za Afrika kupambana na COVID-19 chini ya msingi wa utaratibu wa pande nyingi, kusaidia Afrika kupata maendeleo ya kudumu na kutimiza haki katika sekta ya afya.

Ni kweli maambukizi ya virusi vya Corona barani Afrika si mabaya kama ilivyotarajiwa, lakini uchumi wake dhaifu, miundombinu mibovu ya sekta ya afya na matatizo mengine yameongeza mizigo ya watu na ukosefu wa haki kwenye jamii. Hivi sasa mabadiliko ya virusi vya Corona na upatikanaji usio wa haki wa chanjo vimeongeza sintofahamu kwa Afrika kupambana na janga hilo, kitu ambacho kinahitaji ushirikiano mpana wa kimataifa. Lakini kwa sababu ya uhaba wa rasilimali za afya duniani na baadhi ya nchi kuhodhi chanjo, utaratibu wa jadi wa kutoa msaada hauwezi kutatua mahitaji ya Afrika.

Pengine China ambayo imetuliza hali ya ugonjwa huo ndani ya nchi inaweza kutatua tatizo hilo. Historia ya ushirikiano wa matibabu na afya uliodumu kwa miaka 60 kati ya China na nchi za Afrika umeweka msingi kwa pande hizo mbili kukabiliana na janga hilo kwa pamoja. Mbali na utoaji misaada, China imeshirikiana na mashirika ya kikanda na kimataifa na kutumia ipasavyo rasilimali za pande mbalimbali ili kuimarisha jumuiya yenye hatma ya pamoja kati ya China na Afrika katika sekta ya afya.

Ili kutoa msaada utakaotumika mara moja, China ilitoa shehena tatu ya vitu kwa Umoja wa Afrika na Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa cha Afrika CDC, na mashirika hayo yakisaidia kuvisambaza. Mwezi Machi mwaka 2021, ujumbe wa China kwenye Umoja wa Afrika ulitoa misaada zaidi kwa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa ya uchumi barani Afrika, UNECA ili kusaidia Afrika kupambana na COVID-19. Katika kuijengea Afrika uwezo wa kudumu, Wizara ya Biashara ya China na kamati ya Umoja wa Afrika mwezi Julai mwaka 2020 zilisaini makubaliano ya kujenga makao makuu ya Afrika CDC, mjini Addis Ababa, Ethiopia, ikiwa ni hatua ya kwanza ya “kuanza ujenzi wa mradi huo ndani ya mwaka 2020 kabla ya mpango uliowekwa”, ahadi iliyotolewa kwenye mkutano wa kilele wa mshikamano dhidi ya COVID-19 kati ya China na Afrika uliofanyika mwezi Juni mwaka jana. Hivi sasa mradi huo unaendelea kujengwa, na kutarajiwa kumalizika ndani ya miezi 25.

Kimataifa, China inazingatia zaidi kufanya ushirikiano kwa utaratibu wa pande nyingi na nchi za Afrika katika kupambana na COVID-19. Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Ofisi ya Masuala ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa OCHA, mwaka 2020, asilimia 74 ya ufadhili ulio wa utaratibu wa pande nyingi wa kupambana na COVID-19 umeelekezwa kwenye nchi moja moja, kati yao asilimia 93.72 ikienda katika nchi za Afrika. Mbali na msaada wa fedha na vitu, China pia imejiunga na “Mpango wa Kimataifa wa Kutoa Chanjo ya COVID-19” COVAX ili kutoa chanjo kwa nchi zinazoendelea haswa nchi za Afrika, ambazo COVAX inaweza kuwa ni njia pekee ya kuzisaidia kuondokana na janga hilo. Hivi sasa chanjo mbili za Sinopharm na Sinovac za China zimeidhinishwa na Shirika la Afya Duniani WHO kwa “matumizi ya dharura”, na zinatolewa rasmi kwa COVAX.

Wakati huohuo, China pia imesaidia nchi za Afrika kukabiliana na athari mbaya kupitia ushirikiano wa pande nyingi. Kwa mfano, China imeshirikiana na nchi nyingine za kundi la G20 kutekeleza kwa pamoja “pendekezo la kuahirisha kulipa madeni kwa nchi maskini”. Kwa kupitia Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC, China imesamahe mikopo isiyo na riba ya nchi husika za Afrika iliyopangwa kulipwa hadi mwishoni mwa mwaka jana.

Ukweli ni kuwa China imekuwa na mustakbali na mahitaji yanayofanana na yale ya nchi za Afrika katika sekta ya afya katika historia. Kwa mfano, kwa kupitia msaada wa jamii ya kimataifa na juhudi yake yenyewe, China imepata mafanikio makubwa katika kupambana na malaria, na iliomba hati ya kutokomeza malaria kutoka kWHO baada ya kutoshuhudia ripoti hata moja ya ugonjwa huo. Katika juhudi yake ya muda mrefu ya kupambana na malaria, China imegundua na kutoa Artemisinin inayotokana na mtishamba, kupata uzoefu mkubwa na njia bora, na kufanya ushirikiano wa pande tatu na nchi za Afrika, nchi zilizoendelea na mashirika ya kikanda na kimataifa. Aidha, katika kipindi cha kuanzia mwaka 2014 hadi mwaka 2016 ambapo ugonjwa wa Ebola ulilipuka Afrika magharibi, China imeboresha ushirikiano wake na nchi za Afrika katika sekta ya afya kutoka kutibu magonjwa hadi kuangalia afya ya umma, ili kujihusisha zaidi kwenye ushirikiano wa pande nyingi katika kupambana na magonjwa ya kuambukiza. Wakati ule, China ilitoa pesa taslimu dola za kimarekani milioni 2 kwa WHO na Umoja wa Afrika kwa mtawalia, na pia kufadhili dola za kimarekani milioni 6 ilipozinduwa mfuko wa kimataifa wa dhamana wa Umoja wa Mataifa wa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola. Na likiwa shirika kuu la mfuko wa kupambana na ugonjwa huo, shirika hilo limepata jumla ya ufadhili wa dola za kimarekani milioni 160 kutoka pande 46, na fedha zilizochangiwa na China zilikuwa ni dola milioni 11, ikizifuata Uingereza, Sweden na Ujerumani.

Utaratibu wa pande nyingi ni njia pekee ya kupambana na COVID-19, lakini ni kweli kuwa maambukizi ya COVID-19 yamefichua tatizo kuwa baadhi ya wakati haufanyi kazi. Mbali na kuunga mkono Umoja wa Mataifa na WHO, China inajitahidi kuongeza taratibu za kufanya ushirikiano wa pande nyingi ili kusaidia nchi za Afrika katika sekta ya afya kupitia taratibu hizo, na kukidhi mahitaji mbalimbali katika ushirikiano wa kiafya. Kwa mfano, kwa kawaida, serikali ya China inaongoza katika ushirikiano wake na nchi za Afrika katika sekta ya afya, lakini safari hii, baadhi ya kampuni za China pia zimefanya kazi kubwa katika kutoa msaada utakaotumika mara moja na kujenga uwezo wa muda mrefu. Mabadiliko hayo kwa kiasi kikubwa yameimarisha ushirikiano wa pande nyingi wa China na Afrika katika sekta ya afya.

Nchi za Afrika zinakabiliwa na mizigo ya magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza. Utaratibu wa pande nyingi unaotetewa na China unaweza kuangalia kwa pande zote hali ya afya ya nchi za Afrika, na kufanya ushirikiano wake na Afrika katika sekta ya afya uwe na ufanisi zaidi, kuzisaidia nchi za Afrika kupata haki katika sekta hiyo, kulinda usalama wa afya ya umma duniani na kutoa mchango mkubwa kwa amani na maendeleo ya dunia.
 
Tarehe 17, Juni mwaka 2020, mkutano wa kilele wa mshikamano dhidi ya COVID-19 kati ya China na Afrika ulifanyika, ambapo rais Xi Jinping wa China alitoa pendekezo la “kujenga jumuiya yenye hatma ya pamoja katika sekta ya afya kati ya China na Afrika”. Katika mwaka mmoja uliopita, China imekuwa ikizisaidia nchi za Afrika kupambana na COVID-19 chini ya msingi wa utaratibu wa pande nyingi, kusaidia Afrika kupata maendeleo ya kudumu na kutimiza haki katika sekta ya afya.
Watu weupe wana mitego mingi sana, China na Afrika, jirani zao palepale wanasemaje?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom