UTARATIBU WA MANUNUZI KWA SHULE ZA SERIKALI. NAOMBA TUFAHISHANE TARATIBU NA SHERIA ZILIVYO

Murashani GALACTICO

JF-Expert Member
Feb 27, 2012
2,205
4,707
Wanajukwaa la elimu. Mm ni mtumishi mwalimu katika shule ya sekondari hapa Tanzania. Naomba kufahamu namna manumuzi ya vifaa vya kujifunza na kufundishia ulivyo kwa shule za serikali. Kwa uelewa wangu mdogo wa sheria ya manunuzi ya umma PPRA na marekebisho yake ya 2016 napata wakati mgumu na kujikuta sielewi jinsi inavyopaswa vifaa na hudumu ,kandarasi na zabuni kwa shule. Mathalan najua bei za katoni ya chaki, katon za ream A4 na A3 bei za vifaa vya maabara na vifaa vingine vingi vitumikavyo mashuleni. Sasa kila nikijaribu kushauri wakubwa wangu wa kazi hapa kituo nilichopo wananiona mtu tofauti sana. Kwan vitu, huduma na vifaa hununnuliwa kwa mtindo wa cheki na zabuni kwa gharama za juu kuliko kawaida yani. Naomba tujikite kwenye hoja na sio vioja kwa maslahi ya umma
 
Umeenda kufundisha
Mambo ya ugavi waachie wagavi
Utatafuta ugomvi na wenyewe uanze kuona watu wachungu

Wewe waache,siku wakija wakaguzi wataelewana wao wenyewe
 
Umeenda kufundisha
Mambo ya ugavi waachie wagavi
Utatafuta ugomvi na wenyewe uanze kuona watu wachungu

Wewe waache,siku wakija wakaguzi wataelewana wao wenyewe
Mkuu nikukumbushe kuwa shule hizi za umma nyingi hazina wataaalam wa ugavi na uhasibu. Ni ss waalim ndo huwa tunachukua majukumu hayo. Sasa ipo siku unaweza pata uteuz wa ofisi hizo au kupokea vifaa, au hudumu ambazo zinautata juu ya malipo yake. Je utafanyeje? Kupokea tuu na kusain huku ukijua sahihi yako inahalalisha wizi wa mali ya umma. Ndo maana nimeomba msaada anaefahamu haya mambo atoe elimu
 
Bro hzo bei unazoziona zipo juu ni bei elekezi kutokana na mikataba mbalimbali hasa GPSA.. Huwa kuna viwango vya chini na vya juu vya bei; sasa mara zote wazabuni huwa wanaweka bei ile ya juu kabisa... Unaweza ukaona bei ya kifaa ni sh.elfu 3 ila mzabuni anauza elfu 5
 
Bro hzo bei unazoziona zipo juu ni bei elekezi kutokana na mikataba mbalimbali hasa GPSA.. Huwa kuna viwango vya chini na vya juu vya bei; sasa mara zote wazabuni huwa wanaweka bei ile ya juu kabisa... Unaweza ukaona bei ya kifaa ni sh.elfu 3 ila mzabuni anauza elfu 5
Mkuu mm najua katon ya chaki hizi za dobercolor ni elfu 30 chakushangaza hapa shule niliopo inanunuliwa elfu 60 hadi 70 yaan mara mbili. Boksi la kalam elfu 5 hapa tunaletewa eti kwa elfu 10. Bando ya A4 ream ni elfu 45 hapa tunaletewa kwa elfu 70 si wizii huu wa mali ya umma. Wakat huo unakuta mwalim anakosa hata kiti cha kikaa ofisini. Wanafunzi wanakaa chini hakuna viti na meza. Eti manunuzi yapo juu
 
Then ukumbuke huyo mzabuni alipwi cash...kuna kodi anakatwa...
pia kuna mda anasupply ila anakuja kulipwa hata baada ya miezi 6... Chunguza vizuri hapo ulipo je fedha inayokuja kila mwezi inaweza kufanya kila kitu na kikaenda sawa..
 
Mkuu mm najua katon ya chaki hizi za dobercolor ni elfu 30 chakushangaza hapa shule niliopo inanunuliwa elfu 60 hadi 70 yaan mara mbili. Boksi la kalam elfu 5 hapa tunaletewa eti kwa elfu 10. Bando ya A4 ream ni elfu 45 hapa tunaletewa kwa elfu 70 si wizii huu wa mali ya umma. Wakat huo unakuta mwalim anakosa hata kiti cha kikaa ofisini. Wanafunzi wanakaa chini hakuna viti na meza. Eti manunuzi yapo juu
Kwa nini msinunue moja kwa moja GPSA?
 
Then ukumbuke huyo mzabuni alipwi cash...kuna kodi anakatwa...
pia kuna mda anasupply ila anakuja kulipwa hata baada ya miezi 6... Chunguza vizuri hapo ulipo je fedha inayokuja kila mwezi inaweza kufanya kila kitu na kikaenda sawa..
Asante kwa elimu nzuri mkuu. Hii kodi imekaaje mkuu. Shule nyingine zinanunua mfano katon ya chaki elfu 30 ss shule yetu inauziwa elfu 60. Najua analipwa kwa cheki na sio cash. Emu nipe uelewa kuhusu hilo la kodi linaloleta tofauti ya bei kutoka 30 elf hadi 60 elfu. Na pia fedha ya fidia ya ada tunauopata kwa mwezi milion 2 na sehem inatosha kabisa kulipia bidhaa na huduma kwa wakato bila kuchelewa eti miez sita yote hiyo
 
Naomba nisaidiwe namna ya kupata bei elekezi za vifaa na huduma kutoka GPSA. Nimeingia kwenye tovuti yao sijaona wakuu
 
Back
Top Bottom