Mwadilifu Mdhulumiwa
JF-Expert Member
- Jul 22, 2021
- 418
- 630
Alafu shida ni kwamba hata ukiandika barua ni haohao wanazipokea na kuzizuia hukohuko chini ndo mana ukijitutumua kumsogelea boss wao wanakuzuia kwa nguvu kubwa wakihofia ni lazima utasema ulishaandika barua nyingi , huoni utekelezaji wala hupati majibu! Hii wakati mwingine inaudhi mno!So sad,Africa umungu mtu umetamaraki Sana,unaweza zuiwa hata kumuona mwenyekiti wa mtaa.
Juzi mke wangu alifika katika ofisi za psssf na kutaka kuonana na mkurugenzi ,duh bwana wewe watu wake wachini walitahamaki Sana,na kuanza kumuuliza maswali mengi sana ,mwisho wa siku walimzuia asionane naye.
Sasa nikabaki kijuiuliza ,je huyu mkurugenzi yupo hapo ofisini ili kumhudumia Nani ikiwa wenye shida ya kumuona wanazuliiwa wasimuone.
Mungu aturehemu Sana,sijui na Mimi ikiwa siku moja nikiwa kwenye nafasi ya kuhudumia watu kwa namna hiyo nitakuwa mungu mtu Kama Hawa viongozi wetu!!
Mungu tusaidie!!