Utaratibu wa kuonana na Rais wa nchi ukoje?

Jul 16, 2021
39
44
Naombeni kwa wenye uelewa muweze kunijuza. Hivi kwa Mimi mwananchi wa kawaida (hohehahe) nikitaka kuonana na mkuu wa nchi natakiwa kufuata taratibu zipi ili nimfikie!

Hususani Kama Nina Jambo la muhimu ambalo nataka nimfikishie yeye mwenyewe moja kwa moja?

Au kwa Hali yangu nifute kabisa mawazo hayo? Ni kama milima HAIKUTANI?
 
Kwa nchi za kidikteta kama yetu ni bora uombe kuonana na MUNGU au shetani lakini siyo mkuu wa nchi, utaambiwa upimwe akili na mengine mengi, lakini kwa Ulaya na Marekani raia ana haki ya kumuuona mkuu wa nchi na ni haraka sn unaenda na bango getini unaruhusiwa huku unaweza kufika getini na usirudi tena unapotezwa kabisa.
 
Kwa nchi za kidikteta kama yetu ni bora uombe kuonana na MUNGU au shetani lakini siyo mkuu wa nchi, utaambiwa upimwe akili na mengine mengi, lakini kwa Ulaya na Marekani raia ana haki ya kumuuona mkuu wa nchi na ni haraka sn unaenda na bango getini unaruhusiwa huku unaweza kufika getini na usirudi tena unapotezwa

Kwa nchi za kidikteta kama yetu ni bora uombe kuonana na MUNGU au shetani lakini siyo mkuu wa nchi, utaambiwa upimwe akili na mengine mengi, lakini kwa Ulaya na Marekani raia ana haki ya kumuuona mkuu wa nchi na ni haraka sn unaenda na bango getini unaruhusiwa huku unaweza kufika getini na usirudi tena unapotezwa kabisa.
Ok ahsante kwa ufafanuzi na ushauri. Japooo dahhh!!!!
 
Kwa nchi za kidikteta kama yetu ni bora uombe kuonana na MUNGU au shetani lakini siyo mkuu wa nchi, utaambiwa upimwe akili na mengine mengi, lakini kwa Ulaya na Marekani raia ana haki ya kumuuona mkuu wa nchi na ni haraka sn unaenda na bango getini unaruhusiwa huku unaweza kufika getini na usirudi tena unapotezwa kabisa.
So sad,Africa umungu mtu umetamaraki Sana,unaweza zuiwa hata kumuona mwenyekiti wa mtaa.

Juzi mke wangu alifika katika ofisi za psssf na kutaka kuonana na mkurugenzi ,duh bwana wewe watu wake wachini walitahamaki Sana,na kuanza kumuuliza maswali mengi sana ,mwisho wa siku walimzuia asionane naye.

Sasa nikabaki kijuiuliza ,je huyu mkurugenzi yupo hapo ofisini ili kumhudumia Nani ikiwa wenye shida ya kumuona wanazuliiwa wasimuone.


Mungu aturehemu Sana,sijui na Mimi ikiwa siku moja nikiwa kwenye nafasi ya kuhudumia watu kwa namna hiyo nitakuwa mungu mtu Kama Hawa viongozi wetu!!

Mungu tusaidie!!
 
So sad,Africa umungu mtu umetamaraki Sana,unaweza zuiwa hata kumuona mwenyekiti wa mtaa.

Juzi mke wangu alifika katika ofisi za psssf na kutaka kuonana na mkurugenzi ,duh bwana wewe watu wake wachini walitahamaki Sana,na kuanza kumuuliza maswali mengi sana ,mwisho wa siku walimzuia asionane naye.

Sasa nikabaki kijuiuliza ,je huyu mkurugenzi yupo hapo ofisini ili kumhudumia Nani ikiwa wenye shida ya kumuona wanazuliiwa wasimuone.


Mungu aturehemu Sana,sijui na Mimi ikiwa siku moja nikiwa kwenye nafasi ya kuhudumia watu kwa namna hiyo nitakuwa mungu mtu Kama Hawa viongozi wetu!!

Mungu tusaidie!!
Futa hayo maneno hawa siyo viongozi ni watawala tupu
 
Mwenzako aliruka geti magogoni,akaingia akakata UA,walinzi kuja kushtuka,akawaambia nilikua napima ulinzi wa Rais ,nimeingia na nikachukua ua,jamaa kilaini kabisa alionana na mkulu,ila cha moto alikipata
Labda siyo ikulu ninayoijua mimi ambayo kuta zote zimezungukwa na askari wenye silaha za moto pamoja na CCTV Camera
 
Naombeni kwa wenye uelewa muweze kunijuza. Hivi kwa Mimi mwananchi wa kawaida (hohehahe) nikitaka kuonana na mkuu wa nchi natakiwa kufuata taratibu zipi ili nimfikie! Hususani Kama Nina Jambo la muhimu ambalo nataka nimfikishie yeye mwenyewe moja kwa moja? Au kwa Hali yangu nifute kabisa mawazo hayo? Ni kama milima HAIKUTANI????
Anzia pale Magogoni, mtafute mlinzi mmoja getini msonnye na umzabe kibao. Watakuingiza ndani ya Mjengo na utamuona Mkuu. Ukitoka hapo elekea Chamwino na urudie zoezi hilo. Asante.
 
Rais huyu anatembea na magari ya makombora kwenye msafara kama tuko vitani.

Yaani viongozi wakishapewa zile v8 kumfikia itakua vigumu kama huna connection.
 
Mvizie siku akiwa na Mabeberu and mkimbilie kwa speed ya mshale, hawata kufanya chochote maana watawaonea aibu mabeberu, ila jipange baada ya kutoka hapo
😁😁😁😁😅 Umenikumbusha nikiwa mdogo nilikuwa naishi na Bibi yangu. Sasa Bibi yangu alikuwa akipewa maziwa na mapdre wazungu. Lakini yale maziwa tulikuwa hatuyatumii kila siku, yalikuwa yakitumika kwa siku maalumu tuu. Sasa ilikuwa wakifika wageni mie ndo nilikuwa nikiitumia fursa hiyo kukataa chai ya rangi na kutaka chai ya maziwa. Bibi alikuwa analazimika kutekeleza matakwa yangu hayo. Duh kilichokuwa kinanipata baada ya wageni kutoka Ni SIRI YANGU YA TAIFA 🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kwa nchi za kidikteta kama yetu ni bora uombe kuonana na MUNGU au shetani lakini siyo mkuu wa nchi, utaambiwa upimwe akili na mengine mengi, lakini kwa Ulaya na Marekani raia ana haki ya kumuuona mkuu wa nchi na ni haraka sn unaenda na bango getini unaruhusiwa huku unaweza kufika getini na usirudi tena unapotezwa kabisa.
Huku kwenye bara la giza ukitaka kumuona rais kirahisi ni kutumia uchawi. Hapo aaah, unampapasa rais popote unapotaka. Lkn ktk Ulimwengu wa nyama na mwili, sahau.
 
Back
Top Bottom