Utaratibu huu ni wa kuigwa Kwa viongozi waadilifu!!

Pope

Senior Member
Dec 3, 2007
117
0
Kuala Lumpur - Malaysia.
Waziri Mkuu ambaye ndio kiongozi wa shughuli za kiserikali nchini Malaysia ameamuru mawaziri wote waliteuliwa hivi karibuni kuzitaja mali zao na zoezi hilo linatakiwa kukamilika kabla ya kikao cha kwanza cha Bunge Jumanne wiki ijayo 24 March 2008.Katika taarifa iliyotolewa na ofisi ya waziri mkuu Datook Badawi inasema kuwa, Katika form hizo za ku Declare mali mawaziri hao pamoja na mambo mengine wanatakiwa kusema Account walizonazo na yule mwenye Kima kinachozidi Ringit 150,000 (50,000 USD) anatakiwa aseme pia. Pamoja nao wake na waume wa mawaziri hao, watoto na wanafamilia wote wa karibu yao (immediate family members) nao pia wanatakiw mali zao zionyeshwe.

"Zoezi hili si la hiari, hii ni sheria na ni lazima ifuatwe ili kulinda imani ya wananchi kwa serikali yao...", alisema Badawi.

Zoezi hili haliishii kwa MAwaziri tuu bali ni utaratibu ambao viongozi wote wanaotumikia jamaa hutakiwa kufanywa na baada ya Jumanne, Ripoti ya mali za vigogo hao zitapatikana kwenye mtandao wa serikali kwa wananchi kujua na zitakaa hapo hadi baraza litakapovunjwa. Pia wananchi wanaruhusiwa kuhoji na kuperusi viambatanisho vya kila kiongozi katika office ya serikali, iliongeza taarifa hiyo.

Katika sheria hii, kiongozi akibainika kusema uongo au kuficha mali yake basi atafutwa kazi na kushitakiwa na ikiwezekana mali aliyoificha itataifishwa na serikali.

Baraza la mawaziri la Malaysia linaundwa kutokana na Vyama mbali mbali vya upinzani ikiwa ni kutoka chama Tawala na Upinzani (coalition).

Malaysia ni nchi yenye kufuata mfumo wa Vyama vyingi vya kisiasa na katika chaguzi iliyopita (wiki mbili zilizopita) Chama tawala kilipoteza baadhi ya Majimbo likiwamo jimbo la Penang ambako kuna wachina wengi.


Je mnaonaje utaratibu huu ukitumiwa na kwetu?
 
HATA HAPA KWETU HOJA HIYO ILILETWA......MLETA HOJA ALITANGAZA MALI ZAKE WAKATI ANAINGIA(mr.clean) WAKATI ANATOKA NA MPAKA SASA YUPO/WAPO KIMYA PAMOJA NA KELELE WANAZOPIGIWA.....!
NA HUKO MALAYSIA WASIJE WAKAIGA MFUMO WA WALIOWATANGULIA KTK MFUMO HUO(tz).........!
 
Ni kweli lakini kwa wenzetu naona Demokrasia iko mbali kidogo hasa kwenye suala la Utaifa,
Mfano ni suala la mawaziri kujiuzulu ni kitu cha kawaida endapo anakumbwa na Kashfa na wa mwisho ni aliyekuwa Waziri wa Afya Datuk Chua Soi Lek lipopata Sex Scandal na kuamua ku resign post zake zoote ikiwa ni pamoja na mjumbe wa NEC na Ubunge pia, angalia hapa
[media]http://www.youtube.com/watch?v=VC4oGayyKt4&feature=related[/media]
Nyingine ni hapa juzi tuu mawaziri wa wili walipokataa uteuzi na mmoja wao alisema bayana anataka kuwatumikia wananchi wake akiwa nje ya Madaraka ili aweze kuikosoa Serikali zaidi.
 
Ni kweli lakini kwa wenzetu naona Demokrasia iko mbali kidogo hasa kwenye suala la Utaifa,
Mfano ni suala la mawaziri kujiuzulu ni kitu cha kawaida endapo anakumbwa na Kashfa na wa mwisho ni aliyekuwa Waziri wa Afya Datuk Chua Soi Lek lipopata Sex Scandal na kuamua ku resign post zake zoote ikiwa ni pamoja na mjumbe wa NEC na Ubunge pia, angalia hapa
[media]http://www.youtube.com/watch?v=VC4oGayyKt4&feature=related[/media]
Nyingine ni hapa juzi tuu mawaziri wa wili walipokataa uteuzi na mmoja wao alisema bayana anataka kuwatumikia wananchi wake akiwa nje ya Madaraka ili aweze kuikosoa Serikali zaidi.
inataka kufanana na alivyofanya MREMA those days alipokuwa 'mrema'
 
Utaratibu huu upo ata Tanzania hasa pale inapoelekea Uchaguzi kuna fomu za wagombea wote kuorodhesha mali walizonazo.Isipokuwa Malaysia wao wameenda mbali zaidi kwa kuinclude immediate relatives.

Sual la msingi sio kwa kiasi gani fomu zinajazwa je kile kinachojazwa ni sahihi na kwa kiasi gani wananchi wana access taarifa hizi.

Mmoja wa Wachangiaji amesema ata baada ya mwisho wa madaraka ni bora viongozi wakaonyesha mali walizopata baaada ya uongozi ili vikawa wazi.

Kujaza kama kujaza si shida ila kwa kiasi gani taarifa iliyopo inafanyiwa kazi ndipo penye mushikiri.
Kwa Tanzania sehemu kubwa ya Watanzania hawapati habari au access yao kwa vyombo vya habari ni finyu sasa iko post kwenye web ya Bunge nayo ni mashaka lakini ni Bora zikawa ktk kila ofisi ya Jimbo na kuwekwa ktk mbao za matangazo.

Nawasilisha.
 
Watangaze mali zao wakati wanatoka, huku wakinukuu wakati wanaingia....
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom