Wadau, mimi nina duka la jumla na rejareja.
Jana walikuja jamaa watatu na gari ndogo nyeupe aina ya Mark II, ''Plate Number nimehifadhi''. Wakanunua bidhaa za jumla ya kama 945,000/- na kumlipa kijana kabla ya kupakia mzigo. Kijana alizihesabu na kuhakiksha zimetimia kabisa kisha kuzihifadhi sehemu iliyofungwa. Wakaendelea kupakia mizigo, hatimaye wakamaliza. Baada hapo wakaanza kuondoka, kijana akawaomba mawasiliano kama wateja wazuri ila wakakataa kabisa kabisa. Punde alivyorudi kucheki zile pesa ghafla akakuta zimepungua sana, kabla ya kuhakiki ni kiasi gani ndipo akakimbia kunakili namba za gari. Wakati huo anadai alikuwa na kizungu zungu. Sasa baada ya kutulia, katika hesabu akakuta imebaki 201,000/- pekee. Yaani 744,000/- ilikuwa imepotea katika mazingira hayo ya kutatanisha.
Wadau naomba ushauri, je nifanye nini? Kuna aliyewahi kupitia au kusikia jambo kama hili?
Jana walikuja jamaa watatu na gari ndogo nyeupe aina ya Mark II, ''Plate Number nimehifadhi''. Wakanunua bidhaa za jumla ya kama 945,000/- na kumlipa kijana kabla ya kupakia mzigo. Kijana alizihesabu na kuhakiksha zimetimia kabisa kisha kuzihifadhi sehemu iliyofungwa. Wakaendelea kupakia mizigo, hatimaye wakamaliza. Baada hapo wakaanza kuondoka, kijana akawaomba mawasiliano kama wateja wazuri ila wakakataa kabisa kabisa. Punde alivyorudi kucheki zile pesa ghafla akakuta zimepungua sana, kabla ya kuhakiki ni kiasi gani ndipo akakimbia kunakili namba za gari. Wakati huo anadai alikuwa na kizungu zungu. Sasa baada ya kutulia, katika hesabu akakuta imebaki 201,000/- pekee. Yaani 744,000/- ilikuwa imepotea katika mazingira hayo ya kutatanisha.
Wadau naomba ushauri, je nifanye nini? Kuna aliyewahi kupitia au kusikia jambo kama hili?