Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,900
- 21,988
Ndugu mkuu wa mkoa Paul Makonda, Rejea kichwa cha habari hapo juu wananchi wa Kimara mwisho wakishirikiana na Kibo na Korogwe hatujui huko kwingine, tangu meya wa manispaa achaguliwe kumezuka vituko ambavyo havijawahi tokea wananchi wa Kimara wamekuwa wakilipa usafi kwa sh 3,000 kila kaya
Zoezi limekuwa likienenda bila utoaji wa risiti yoyote na pale unapotaka kujua zaidi wanakuhangaisha.
Sasa kumezuka hili zoezi hapa Kimara mwisho wanamgambo wakishirikiana na diwani wa CHADEMA wanapita nyumba kwa nyumba kila Alhamis kuomba fedha.
Katika hilo wapo wamama hapa Kimara mwisho wanalia kwasababu...
Hakuna utaratibu wa aina yoyote nani atoe ngapi madiwani wanasema huyu 40,000.
Unatakiwa kutoa usipotoa wanagari wanakutishia kukuweka ndani. Je, huu ndio ustaarabu wa manispaaa?
Nani anapanga bei za malipoo ya usafi? Je, vipi wengine wanapewa risiti wengine hawapewi, je ndio ustaarabu wa malipo?
Toka lini mgambo akapita anakusanya fedha za usafi bila serikali za mitaa kibaya zaidi wanaongea kwenye simu na mtu anawambia nyie andika pesa yoyote wakitaka risiti watoleeni wasipotaka msiwape hakikisheni tunakusanya mamilioni. Je, ndio ustaarabu wa malipo ya usafi?
Makonda njoo Kimara na Korogwe pita na vijana wako uone watu wanavyonyanyaswa na mabwana afya akishirikiana na diwani. Huu sio ustaarabu wa serikali ya Magufuli hata kidogo.
Tunaombaaa Makonda uanze kuzichunguza na zile risiti zote huku Kimara mwisho tumewagomea na baadhi wamelipishwa mpaka laki moja, huu ni uhuni.
Na kwanini kila gari la usafi liikipita wapite na mabwana afya wakiomba hela bila risiti huu ni uchafu wa zamani sio sasa kwa enzi za Magufuli.
Tunaomba msaada wako tunaamini watu wa serikali za mitaa nao watakuwa wanajua kinachoendelea.
Makonda hata mkataba wa magari ya usafi ni malipo ya kitapeli tupu tunaomba uongozi wa Meya Jacob msimamie haya na watu wajue haki zao na sio watu wachache kutengeneza matumbo yao migongo ya wananchi.
Huu wakati wa uwazi na ukweli.
Zoezi limekuwa likienenda bila utoaji wa risiti yoyote na pale unapotaka kujua zaidi wanakuhangaisha.
Sasa kumezuka hili zoezi hapa Kimara mwisho wanamgambo wakishirikiana na diwani wa CHADEMA wanapita nyumba kwa nyumba kila Alhamis kuomba fedha.
Katika hilo wapo wamama hapa Kimara mwisho wanalia kwasababu...
Hakuna utaratibu wa aina yoyote nani atoe ngapi madiwani wanasema huyu 40,000.
Unatakiwa kutoa usipotoa wanagari wanakutishia kukuweka ndani. Je, huu ndio ustaarabu wa manispaaa?
Nani anapanga bei za malipoo ya usafi? Je, vipi wengine wanapewa risiti wengine hawapewi, je ndio ustaarabu wa malipo?
Toka lini mgambo akapita anakusanya fedha za usafi bila serikali za mitaa kibaya zaidi wanaongea kwenye simu na mtu anawambia nyie andika pesa yoyote wakitaka risiti watoleeni wasipotaka msiwape hakikisheni tunakusanya mamilioni. Je, ndio ustaarabu wa malipo ya usafi?
Makonda njoo Kimara na Korogwe pita na vijana wako uone watu wanavyonyanyaswa na mabwana afya akishirikiana na diwani. Huu sio ustaarabu wa serikali ya Magufuli hata kidogo.
Tunaombaaa Makonda uanze kuzichunguza na zile risiti zote huku Kimara mwisho tumewagomea na baadhi wamelipishwa mpaka laki moja, huu ni uhuni.
Na kwanini kila gari la usafi liikipita wapite na mabwana afya wakiomba hela bila risiti huu ni uchafu wa zamani sio sasa kwa enzi za Magufuli.
Tunaomba msaada wako tunaamini watu wa serikali za mitaa nao watakuwa wanajua kinachoendelea.
Makonda hata mkataba wa magari ya usafi ni malipo ya kitapeli tupu tunaomba uongozi wa Meya Jacob msimamie haya na watu wajue haki zao na sio watu wachache kutengeneza matumbo yao migongo ya wananchi.
Huu wakati wa uwazi na ukweli.