Utapeli wa kwenye simu, tujifunze wote

lembu

JF-Expert Member
Dec 31, 2009
16,374
21,831
Tuusome na kama na wewe ulishatumiwa au kama bado jiandae na ujifunze, usikurupuke kutuma pesa
_______________________________________________________________________

Habari ya kazi,
ile hela inabidi uitume kwenye namba hii 0753515775 jina litatoka HADIJA MELIMELI,usitume kwenye namba yangu imefungwa,simu hazingii wala kutoka

Hawa watu ni kina nani hawa walio na uwezo wa kupata namba karibia ya kila mteja wa vodacom na kumtumia ujumbe wa kutuma pesa, mbona wanajiamini kiasi hiki!
_______________________________________________________________________
TCRA wao wako bussy na mambo mengine huku wananchi wakitapeliwa na kufanyiwa crime za kwenye mitandao, hata ukiripoti no impact
 
Hao mi nadhani wana buni buni namba tu then wanatuma msg. alafu mbona ziko nyingi acha hiyo kuna zile za kukutamanisha utajir, kwahiyo wazoee . sema kuna hawa wanaitwa BIKO hahaha ndo hatari kwa vishawishi.
 
Hata mimi kama TCRA nisingelishughulikia suala ilo. Yaani mtu una akili timamu unaambiwa tuma pesa kwenye namba hii wakati hukuwa na miadi ya kumtumia pesa akishe unatuma? Jiongeze!
 
Hata mimi kama TCRA nisingelishughulikia suala ilo. Yaani mtu una akili timamu unaambiwa tuma pesa kwenye namba hii wakati hukuwa na miadi ya kumtumia pesa akishe unatuma? Jiongeze!
Ukiwa huna mpango wa kumtumia mtu pesa ni sawa lakini kama ulikuwa kwenye harakati za kumtumia mtu wako pesa unaweza kwa haraka ukapanic ukajikuta umetuma. Na nafikiri wanapata ndio maana inashika kasi
 
Hao wezi hupata namba kwenye nyumba za wageni, Watoa wahudumu wa Mpesa, TIGO, halo na,Airtel Pesa, kwenye mahudhurio ya semina nk. Wabaya zaidi ni wahudumu wa Mpesa, Wao huwatumia no Mara uingizapo fedha naye humtumia Mwizi wake ili aanze kukufuatilia.
 
Hao wezi hupata namba kwenye nyumba za wageni, Watoa wahudumu wa Mpesa, TIGO, halo na,Airtel Pesa, kwenye mahudhurio ya semina nk. Wabaya zaidi ni wahudumu wa Mpesa, Wao huwatumia no Mara uingizapo fedha naye humtumia Mwizi wake ili aanze kukufuatilia.


Nakubaliana na wewe kabisa simu ikiwa haina hata mia hizo msg huwezi ziona subiri iingie hata mia utazima mpk uchoke. juzi nilikuwa na mgeni internationa anatumia line ya voda .... Tumekaa ile tunabadilishana mawazo mara msg hiyo ile hela tuma kwenye no ................... naangalia ni mgeni no yake haina hata week mbili. kusoma kiswahili hajui. akaniuliza ikabidi nimwambie ni Spam alichoka kabisa
 
hili ni genge la wahuni tu waganga njaa!Ila nina uhakika wanabahatisha katika watu 500 lazima upate mmoja
 
Hata mimi kama TCRA nisingelishughulikia suala ilo. Yaani mtu una akili timamu unaambiwa tuma pesa kwenye namba hii wakati hukuwa na miadi ya kumtumia pesa akishe unatuma? Jiongeze!
Swala hapa siyo akili bali usumbufu,ila nawasiwasi ni mpango wa kuongeza mapato kwa serikali na mitandao ya simu ndiyo maana wako kimya tu
 
Nakubaliana na wewe kabisa simu ikiwa haina hata mia hizo msg huwezi ziona subiri iingie hata mia utazima mpk uchoke. juzi nilikuwa na mgeni internationa anatumia line ya voda .... Tumekaa ile tunabadilishana mawazo mara msg hiyo ile hela tuma kwenye no ................... naangalia ni mgeni no yake haina hata week mbili. kusoma kiswahili hajui. akaniuliza ikabidi nimwambie ni Spam alichoka kabisa
Hata wakisikia unaongelea maswala ya hela, au umepata hela ndio hatari.
 
Ukiwa huna mpango wa kumtumia mtu pesa ni sawa lakini kama ulikuwa kwenye harakati za kumtumia mtu wako pesa unaweza kwa haraka ukapanic ukajikuta umetuma. Na nafikiri wanapata ndio maana inashika kasi
Mkuu huwezi kupanic kwenye kutuma hela tu ivi ivi... cha kwanza kama ulikuwa upo kwenye harakati za kumtumia mtu wako pesa, utashangazwa kuona ujumbe umetoka kwenye namba ya mtu mwengine, it is a common sense kumpigia kwanza kuhakikisha ndie.
 
Swala hapa siyo akili bali usumbufu,ila nawasiwasi ni mpango wa kuongeza mapato kwa serikali na mitandao ya simu ndiyo maana wako kimya tu
Filtering such message itakuwa vigumu, TCRA hawawezi wakaacha kazi na kuanza kuzifilter hizo pamoja na zile za waganga. Kwa sababu, ikiwa wana filter message kama hizo, vipi pale mtu kweli amekutumia huo ujumbe na ikawa ni kweli yeye huyo mtu? lakini hujauona kwa sababu TCRA wamefilter? Apo cha kufanya ni kuzirepoti polisi tu! Usumbufu ni zile meseji za mitandao na simu za mitandao kama Tigo wanakupigia simu unapokea kumbe tangazo au story.
 
Filtering such message itakuwa vigumu, TCRA hawawezi wakaacha kazi na kuanza kuzifilter hizo pamoja na zile za waganga. Kwa sababu, ikiwa wana filter message kama hizo, vipi pale mtu kweli amekutumia huo ujumbe na ikawa ni kweli yeye huyo mtu? lakini hujauona kwa sababu TCRA wamefilter? Apo cha kufanya ni kuzirepoti polisi tu! Usumbufu ni zile meseji za mitandao na simu za mitandao kama Tigo wanakupigia simu unapokea kumbe tangazo au story.
Unasupport ujinga na kutosupport ujinga hapa!!
 
Hata kama umetoka Nanjilinji au Makongolosi leo huwezi ibiwa kifala hivyo
Hata mimi na wewe hatuwezi ibiwa kifala namna hii, LAKINI wapo wanaoibiwa tena wengi. Hata hivyo akili zetu hazifanani
 
Mkuu huwezi kupanic kwenye kutuma hela tu ivi ivi... cha kwanza kama ulikuwa upo kwenye harakati za kumtumia mtu wako pesa, utashangazwa kuona ujumbe umetoka kwenye namba ya mtu mwengine, it is a common sense kumpigia kwanza kuhakikisha ndie.
Mimi sitapanic lakini wapo wanaojua kupanic tena wapo mijini, an wengine wamo humu humu. TUELIMISHANE ndio jambo muhimu
 
Back
Top Bottom