Utapeli wa biashara ya kuwekeza unaofanywa na kampuni ya FX Fire iliyopo mkoani Mwanza

Naomba watanzania muwe makini sana na kijana anaitwa Peter Kasanga aliyeko mkoani mwanza mwenye kampuni ya fx fire, anafanya biashara ya uwekezaji yaani unawekeza pesa na mwisho wa mwezi unalipwa 60% ya kiasi cha pesa ulicho wekeza, alikuwa akifanya hii biashara ya uewekezaji tangu mwaka jana mwanzoni, alikusanya pesa za watu zaidi ya 300, huu ni mwezi wa 5 ajatoa pesa kwa wawekezaji waliowekeza.

Cha kushangaza anazidi kupokea pesa kwa wawekezaji wapya wakati ajalipa pesa kwa wawekezaji wa muda mrefu ajawalipa huu mwezi wa 5, naomba watanzania ambao mtakutana na matangazo ya uwekezaji toka kampuni inaitwa fx fire ambayo mmiliki ni peter kasanga mwenye namba hizi za simu 0744951631, 0626215507, 0742725683 bado anaendela kukusanya pesa za watu kwa kuwa akikishia kuwa baada mwezi watapokea 60%, mwezi ukifika anatoka visingizio kuwa pesa zimefungiwa benki.

Naomba mkuu wa takukuru mkoa wa mwanza, OCD mkoa wa mwanza, DSO na RSO fikeni jengo la Rock City Mall iliyopo ofisi ya fx fire muone namna ya kuwasaidia watanzania ambao wametapeliwa na huyu peter kasanga
Watu hawakomagi jamani😎😎😎
 
"Mang'ombe hayaishi mjini hapa."
Sijui hata inakuaje nafikiria hivi huyo mtu anamshawishije mtu hadi anakubali aisee! Pesa ilivo ngumu hivi mtu aje aniambie nimpe anipe 60% dah inabidi tukae chini week zima akinielezea ataizalishaje with vivid examples.🤔 watu wajue tu hamna shortcuts
 
Uyo sio tapeli mkuu
Naweza kumuita Baharia aliehitimu mafunzo kikamilifu kabisa kila siku tunapiga kelele bongo hii "ukiona unaitwa kwenye fursa basi jua wewe ndo fursa" Ila jitu bado HALISIKII kila siku mada ni zilezile Q-net,Smile we care wanaongelewa wanavyotapeli watu ila Jitu bado HALISIKII amakweli wajinga kila siku wanazaliwa wapya

"WAJINGA NDIO WALI WAO"

5 AGAIN
 
Duh poleni wahanga! Ila jamani bado tu hamshtuki na hizi biashara! Mtu anakuahidi kukupa 60% kwa biashara gani hasa hushtuki mtu kukushikia pesa yako?🤷‍♂️ hizi shortcuts zinatukucost.
Watu wanapenda fedha za chapchap zisizofuata kanuni ya utafutaji kiuhalisia matokeo yake ndio hayo wakati soko la hisa lipo ajabu hawajitokezi kuwekeza...kwahiyo hii itakuwa kama KUKU POA hivyo kama ni kweli wazee wataibuka na kuja na kufanya shughuli za upatu na kutaifisha kisha waliowekezwa wataambulia patupu kwa kuwa hela zao wamekeza kwenye shughuli haramu
 
Hivi hao mnaowaita matapeli na mpaka namba zao za simu mnaziweka humu kwa nini hamuwaripoti mahali husika ama hamtaki kumfaidisha DPP ambae amekuwa ndio mnufaika mkuu wa pesaza wapenda vitonga
Wengi sio matapeli. Sheria ya makampuni inasema ukiwekeza faida mnagawana ila na hasara mnagawa pia. Sasa kama kachoka account mnataka mgawane nini kama sio majivu.
Tatizo watu hawaambiwi kama kuna hasara, na ikitokea hakuna ushahidi kama hasara imetokea. Ndio hapo mambo ya subiri nitawatumia baadae inaanza.
 
Sijui hata inakuaje nafikiria hivi huyo mtu anamshawishije mtu hadi anakubali aisee! Pesa ilivo ngumu hivi mtu aje aniambie nimpe anipe 60% dah inabidi tukae chini week zima akinielezea ataizalishaje with vivid examples. watu wajue tu hamna shortcuts
Hatua ya kwanza kutapeliwa ni tamaa ya kupenda vitu rahisi(shortcut) pili binadamu tumetofautiana vingi, hasa akili, hivyo mang'ombe wanakamulika vizuri tu maziwa yao kwa kutaka shortcut na kicjwani empty set.
 
Ontario akamatwe afungwe jiwe kubwa sana shingoni atupwe baharini tena kati kati ya bahari...
 
Yani uweke pesa halafu akupe 60% hujiulizi ataizalisha vipi?

Mimi nasisitiza wapumbafu wapigwe maana hakuna namna ya kuwasaidi.
 
Uyo sio tapeli mkuu
Naweza kumuita Baharia aliehitimu mafunzo kikamilifu kabisa kila siku tunapiga kelele bongo hii "ukiona unaitwa kwenye fursa basi jua wewe ndo fursa" Ila jitu bado HALISIKII kila siku mada ni zilezile Q-net,Smile we care wanaongelewa wanavyotapeli watu ila Jitu bado HALISIKII amakweli wajinga kila siku wanazaliwa wapya

"WAJINGA NDIO WALI WAO"

5 AGAIN
Yeah.... though bado sio jambo la kukubalika lakn pia shortcuts sio nzuri wabongo tuelewee
 
Back
Top Bottom