Utapeli mpya mjini | Mawakala wa huduma za kifedha kuweni makini sana

Hii kuna jamaa angu amepigwa laki 6 wiki iliyopita.

Kuna jamaa alikuja akaomba awekewe elfu 5, akaweka ila kabla hajaondoka akaja mtu mwingine akaomba atume/kuweka elfu 50, sasa huyu wa kwanza akawa anampigisha story yule mtoa huduma tena kuhusu mambo ya Corona na story zilikuwa tamu sana, basi mtoa huduma akampa simu yule mteja wa pili ili aweke namba za simu. Alichokifanya jamaa ni kwenda 'inbox' akajitumia sms na kisha akasave namba yake kama TIGOPESA kwenye simu ya mtoa huduma. Jamaa akarudisha simu na kumuambia muamala umekatika.

Mtoa huduma akafanya tena muamala na kufanikisha kutuma hela kwa mteja. Yule jamaa wa kwanza akachukua simu kwa jamaa wa pili na kumuambia mtoa huduma anatoa laki 6, kumbe aliedit ile sms ya salio la mwisho akaongeza laki 6 na kwa kuwa kule hii namba ikiseviwa kwa jina la TIGOPESA basi jamaa akatuma sms ya kawaida lakini kule kwa mtoa huduma likatokea jina la TIGOPESA kuwa amepokea laki 6 na salio jipya ni kadhaa, mtoa huduma si akaingia king akampa laki 6.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huu ni uzembe wa hali ya juu sana huwezi kumpa mteja ajaze namba mwenyewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekuwa nasoma visa vya kuibiwa kwenye hizo mobile money transactions na nimegundua wizi mwingi hutokea kwa sababu biashara hizi huendeshwa ki-local, kimazoea na kizembe sana. Kwa nini watu wasiwe organized jamani watanzania tuna laana gani? Kwa nini mtu asiwe na counter book ambayo mteja atarekodi details zake kabla ya kuhudumiwa? Vitu kama namba anayotuma fedha kweli unampa aandike mwenyewe? Kwa nini kusiwe na karatasi akaandika namba halafu mhudumu akaingiza mwenyewe kwenye simu?
Utahudumia wateja wangapi kwa siku kwa staili hiyo ? Imagine uko na wateja wa5 kwa wakati mmoja, kila mtu ukisema uanze kuandika taarifa zake si wengine watakukimbia.
 
Mimi kwenye biashara ni kauzu zaidi ya dagaa sicheki hata kwa bahati mbaya ukija na blablaa nikikuangalia tu mara moja unaondoka bila kuaga


Sent using IPhone X
 
Inatakiwa umakini sana matapeli wana njia nyingi sana, juzi kitaani hapa kuna dada na akiwa dukani kwake kapokea mteja, mteja aliomba soda take away dazan kadhaa akidai wana part jirani na hapo, akaomba wamsaidie kabisa na kubeba hadi katika nyumba aliodai amepanga, kule wakamkuta mdada anafua nguo na hakushtuka na ujio wa vinywaji, walipokua wanaenda kuchukua vinywaji mara ya pili jamaa akaomba atumiwe 250,000/= katika m-pesa ili wakimaliza kubeba vinywaji atoe hela yote, alipotumiwa tu akawapiga chenga na kutokomea. Walipoenda pale kuulizia yuko wapi wakaambiwa jamaa alikuja pale na kuomba aweke vinywaji kwa muda kwani anataka azunguke kutafuta mahitaji mengne ndo mana alipokuja hakuna aliekua anamshangaa. Ndo dada wa watu kujua ameshapigwa 250 fasta, akaanza kulia na kubeba soda zake dah
 
Uondoke ofisini kwangu halafu urudi na stori zako za alinacha

Utasimulia ntavyojitoa ufahamu sikujui,maana hamna ruhusa kwa wakala

kutuma pesa kwa mtu wa mbali,wakala anatakiwa kumuwekea pesa

mteja mwenye simu yake mkononi sio simu ipo kwa mtu mwingine

sasa wewe urudi ulete story zako za Ba Be Bi Bo Bu,nakuruka futi 100
 
Hii kuna jamaa angu amepigwa laki 6 wiki iliyopita.

Kuna jamaa alikuja akaomba awekewe elfu 5, akaweka ila kabla hajaondoka akaja mtu mwingine akaomba atume/kuweka elfu 50, sasa huyu wa kwanza akawa anampigisha story yule mtoa huduma tena kuhusu mambo ya Corona na story zilikuwa tamu sana, basi mtoa huduma akampa simu yule mteja wa pili ili aweke namba za simu. Alichokifanya jamaa ni kwenda 'inbox' akajitumia sms na kisha akasave namba yake kama TIGOPESA kwenye simu ya mtoa huduma. Jamaa akarudisha simu na kumuambia muamala umekatika.

Mtoa huduma akafanya tena muamala na kufanikisha kutuma hela kwa mteja. Yule jamaa wa kwanza akachukua simu kwa jamaa wa pili na kumuambia mtoa huduma anatoa laki 6, kumbe aliedit ile sms ya salio la mwisho akaongeza laki 6 na kwa kuwa kule hii namba ikiseviwa kwa jina la TIGOPESA basi jamaa akatuma sms ya kawaida lakini kule kwa mtoa huduma likatokea jina la TIGOPESA kuwa amepokea laki 6 na salio jipya ni kadhaa, mtoa huduma si akaingia king akampa laki 6.

Sent using Jamii Forums mobile app

Huyo atakuwa mgeni kwenye biashara au alikuwa na mambo mengi kichwani. Yaani mtu unatoa laki sita bila kuangalia salio? Mimi ule muda nakuhesabia hela huku natuma voda sms ya kuangalia salio i.e narequest kuona salio kabla sijatoa hela.
 
Ukiwa wakala wa huduma za kipesa unakua unafanya miamala mingi sana kwa siku kiasi kwamba huenda mingine usiikumbuke kama hukuandika kwenye daftari.

Airtel Money wao hawana log book kwa kumbukumbu za mteja. Matapeli wanapitia humu humu sababu wanajua hukuandika.

Alikuja mteja kama siku ya jana akaomba kuwekewa mfano 5000 ukamwekea vizuri na kuondoka zake sababu ya shughuli nyingi huwezi kufika kesho ukakumbuka wateja wote na kiasi ambacho uliwawekea.

Kesho anarudi mida ya mchana anadai alikupa 50,000 hesabu ya bosi wake kwenye boda boda ukamwekea 5,000 tu. Hapo hakuna mwenye uhakika na madai ya mwengine wewe unaweza kusema niliweka yote. Anadai bosi wake anamsumbua anataka hesabu yake kamili ambayo alileta jana.

Haraka haraka utapiga simu Airtel ili kuthibitisha madai ya mteja huyo. Utajibiwa kuwa ni kweli jana muda fulani ulimuwekea kiasi cha 5,000 tu huyo mteja. Mpaka hapo kama kichwa kibovu unapigwa sababu utalazimika kummaliza 45,000 yake iliyobaki.

Jambo muhimu la kuzingatia na kufanya:

WAKALA HAKIKISHA HESABU YAKO YA MZUNGUKO UNAIJUA KIKAMILIFU NA IKIWEZEKANA UMEIANDIKA SEHEMU

1. Mwambie huyo mteja kuwa kwa sababu unajua jumla ya kiasi chako cha pesa kinachozunguka ngoja upige hesabu.

2. Piga hesabu zako uone kama kuna kiasi halisi kwenye mzunguko wako.

3. Mwambie kiasi kilichopo kwenye mzunguko wangu hakijaongezeka kwahiyo jana alitoa kiasi hicho hicho alichowekewa. Yeye mwenyewe ataondoka kwa kisingizio cha kwenda kumuita boss wake ili aje na simu na ujumbe wa muamala.

Kama hakubaliani na unachomwambia achukue hatua zaidi kwa sababu biashara ni siri huwezi kumwambia una jumla ya shilingi ngapi kwenye mzunguko wako. Labda kwa usaidizi wa polisi kama itahitajika.

Kama una tabia ya kuchanganya pesa za miamala na pesa za biashara nyingine huenda ukashindwa kwenye utapeli huo kama mtu atakomaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Daaah,huu ni ushauri mzuri sana.
 
Utahudumia wateja wangapi kwa siku kwa staili hiyo ? Imagine uko na wateja wa5 kwa wakati mmoja, kila mtu ukisema uanze kuandika taarifa zake si wengine watakukimbia.
Ndugu yangu wee. Ulikimbia umande nini. Usiniambie watu watano ni vigumu kuwahudumia huku ukichukuwa details zao! Kwani unapowahudumia unahudumia wote kwa wakati mmoja? Unahudimia wa kwanza huku wengine wanaandika Ukimalizana naye wengine wanakuwa tayari
 
kuna ile unakuta unampa mteja simu aandike namba, yeya anaingia kwenye sms anaangalia sms ya mwisho ya muamala anaituma kwenye no yake then anaisave no yake kwnye cm ya wakala M-PESA akimaliza anakurudushia cm anajifanya ameahurisha kuweka ela,

mfano kulikwa na balance ya sh 50000 anaedit ile sms kuwa ametia sh 40000 salio lako jipya ni sh 10000, alafu anaituma hiyo sms kwenye ile cm ya wakala ambayo alisave no yake jina ni M-PESA
duhh, ukae na simu ya wakala muda wote huo asipokushtukia basi yeye ni mzembe
 
Huna hata haja ya kupiga hesabu hapo, kwa kawaida mteja anatakiwa apate confirmation sms kabla hajamalizana na wakala. Kama ulimwekea nae akathibitisha kuwa tayari imeingia ndio imeisha hivyo.
Huo ndio ukweli, maelezo mengi ya mleta mada hayana msingi. Mteja haondoki mpaka taarifa ya sms ionekane kwake. Akisha kupa kisogo biashara imekwisha. Wakala anaehadaiwa kiasi cha kudiriki kupiga simu huduma kwa wateja ujue ama ni mgeni ktk biashara, au akili imeanza kuingia kutu au Corona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu yangu wee. Ulikimbia umande nini. Usiniambie watu watano ni vigumu kuwahudumia huku ukichukuwa details zao! Kwani unapowahudumia unahudumia wote kwa wakati mmoja? Unahudimia wa kwanza huku wengine wanaandika Ukimalizana naye wengine wanakuwa tayari
Unayazungumza hayo kwa kuufikiria ulimwengu wa ushindani ? Unajua sifa za wateja ? Nani anayependa kusubirishwa ilihali pembeni kuna huduma kama hiyo ambayo inatolewa pasipo hizo interview za kukusafanya details ?
 
Ukiwa wakala wa huduma za kipesa unakua unafanya miamala mingi sana kwa siku kiasi kwamba huenda mingine usiikumbuke kama hukuandika kwenye daftari.

Airtel Money wao hawana log book kwa kumbukumbu za mteja. Matapeli wanapitia humu humu sababu wanajua hukuandika.

Alikuja mteja kama siku ya jana akaomba kuwekewa mfano 5000 ukamwekea vizuri na kuondoka zake sababu ya shughuli nyingi huwezi kufika kesho ukakumbuka wateja wote na kiasi ambacho uliwawekea.

Kesho anarudi mida ya mchana anadai alikupa 50,000 hesabu ya bosi wake kwenye boda boda ukamwekea 5,000 tu. Hapo hakuna mwenye uhakika na madai ya mwengine wewe unaweza kusema niliweka yote. Anadai bosi wake anamsumbua anataka hesabu yake kamili ambayo alileta jana.

Haraka haraka utapiga simu Airtel ili kuthibitisha madai ya mteja huyo. Utajibiwa kuwa ni kweli jana muda fulani ulimuwekea kiasi cha 5,000 tu huyo mteja. Mpaka hapo kama kichwa kibovu unapigwa sababu utalazimika kummaliza 45,000 yake iliyobaki.

Jambo muhimu la kuzingatia na kufanya:

WAKALA HAKIKISHA HESABU YAKO YA MZUNGUKO UNAIJUA KIKAMILIFU NA IKIWEZEKANA UMEIANDIKA SEHEMU

1. Mwambie huyo mteja kuwa kwa sababu unajua jumla ya kiasi chako cha pesa kinachozunguka ngoja upige hesabu.

2. Piga hesabu zako uone kama kuna kiasi halisi kwenye mzunguko wako.

3. Mwambie kiasi kilichopo kwenye mzunguko wangu hakijaongezeka kwahiyo jana alitoa kiasi hicho hicho alichowekewa. Yeye mwenyewe ataondoka kwa kisingizio cha kwenda kumuita boss wake ili aje na simu na ujumbe wa muamala.

Kama hakubaliani na unachomwambia achukue hatua zaidi kwa sababu biashara ni siri huwezi kumwambia una jumla ya shilingi ngapi kwenye mzunguko wako. Labda kwa usaidizi wa polisi kama itahitajika.

Kama una tabia ya kuchanganya pesa za miamala na pesa za biashara nyingine huenda ukashindwa kwenye utapeli huo kama mtu atakomaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
wamekuonamo tu unashindwa kumtandika ngumi moja takatifu kabisa uyo jamaa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii kuna jamaa angu amepigwa laki 6 wiki iliyopita.

Kuna jamaa alikuja akaomba awekewe elfu 5, akaweka ila kabla hajaondoka akaja mtu mwingine akaomba atume/kuweka elfu 50, sasa huyu wa kwanza akawa anampigisha story yule mtoa huduma tena kuhusu mambo ya Corona na story zilikuwa tamu sana, basi mtoa huduma akampa simu yule mteja wa pili ili aweke namba za simu. Alichokifanya jamaa ni kwenda 'inbox' akajitumia sms na kisha akasave namba yake kama TIGOPESA kwenye simu ya mtoa huduma. Jamaa akarudisha simu na kumuambia muamala umekatika.

Mtoa huduma akafanya tena muamala na kufanikisha kutuma hela kwa mteja. Yule jamaa wa kwanza akachukua simu kwa jamaa wa pili na kumuambia mtoa huduma anatoa laki 6, kumbe aliedit ile sms ya salio la mwisho akaongeza laki 6 na kwa kuwa kule hii namba ikiseviwa kwa jina la TIGOPESA basi jamaa akatuma sms ya kawaida lakini kule kwa mtoa huduma likatokea jina la TIGOPESA kuwa amepokea laki 6 na salio jipya ni kadhaa, mtoa huduma si akaingia king akampa laki 6.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hao matapeli wanajuana,izo mbinu za matapeli kila cku zinakuja mpyaa...
 
Ukiwa wakala wa huduma za kipesa unakua unafanya miamala mingi sana kwa siku kiasi kwamba huenda mingine usiikumbuke kama hukuandika kwenye daftari.

Airtel Money wao hawana log book kwa kumbukumbu za mteja. Matapeli wanapitia humu humu sababu wanajua hukuandika.

Alikuja mteja kama siku ya jana akaomba kuwekewa mfano 5000 ukamwekea vizuri na kuondoka zake sababu ya shughuli nyingi huwezi kufika kesho ukakumbuka wateja wote na kiasi ambacho uliwawekea.

Kesho anarudi mida ya mchana anadai alikupa 50,000 hesabu ya bosi wake kwenye boda boda ukamwekea 5,000 tu. Hapo hakuna mwenye uhakika na madai ya mwengine wewe unaweza kusema niliweka yote. Anadai bosi wake anamsumbua anataka hesabu yake kamili ambayo alileta jana.

Haraka haraka utapiga simu Airtel ili kuthibitisha madai ya mteja huyo. Utajibiwa kuwa ni kweli jana muda fulani ulimuwekea kiasi cha 5,000 tu huyo mteja. Mpaka hapo kama kichwa kibovu unapigwa sababu utalazimika kummaliza 45,000 yake iliyobaki.

Jambo muhimu la kuzingatia na kufanya:

WAKALA HAKIKISHA HESABU YAKO YA MZUNGUKO UNAIJUA KIKAMILIFU NA IKIWEZEKANA UMEIANDIKA SEHEMU

1. Mwambie huyo mteja kuwa kwa sababu unajua jumla ya kiasi chako cha pesa kinachozunguka ngoja upige hesabu.

2. Piga hesabu zako uone kama kuna kiasi halisi kwenye mzunguko wako.

3. Mwambie kiasi kilichopo kwenye mzunguko wangu hakijaongezeka kwahiyo jana alitoa kiasi hicho hicho alichowekewa. Yeye mwenyewe ataondoka kwa kisingizio cha kwenda kumuita boss wake ili aje na simu na ujumbe wa muamala.

Kama hakubaliani na unachomwambia achukue hatua zaidi kwa sababu biashara ni siri huwezi kumwambia una jumla ya shilingi ngapi kwenye mzunguko wako. Labda kwa usaidizi wa polisi kama itahitajika.

Kama una tabia ya kuchanganya pesa za miamala na pesa za biashara nyingine huenda ukashindwa kwenye utapeli huo kama mtu atakomaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbona unaonesha wewe wakala hauna uhakika! Unapoamua kithibisha toka Airtel ni kwamba hauna uhakika na kazi yako, ulichokifanya usithubutu kumuuliza mtu mwingine kama ulikifanya unajifunga, kataa.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom