Mkogoti
TAPELI Mkubwa
- May 3, 2020
- 2,416
- 3,908
Habari wakuu Mimi mzima kabisa wa afya Natumaini nawe pia huko mzima kabisa, bado Tunaendelea na maombelezo ya Rais wetu Mpendwa Mh. William B. Mkapa R.I.P 😞🙏
Ipo hivi wakuu, nipo nawaza kitu ambacho kipo ubongoni mwangu nimekifikiria tu ghafla.
Ipo hivi Huku Maeneo ninapoishi jina (kapuni) kuna Uwanja wa ndege ulikuwa wa kitambo na ulikuwa unatumika ila sijui nini kilitokea ndege kubwa hazitui tena zinaishia mkoa jirani, bali ni ndege binafsi ndio zinaruhusiwa kutua sikujua ni kwanini.
Basi serikali imeamua tena kuutengeneza uwe mkubwa sasa kuna nyumba zipo baadhi na kiwanja na kuna mashamba pembeni watu walikuwa wanalima mpunga, viazi, na mboga mboga kwa maana hiyo wanatakiwa watoke.
Basi nikawaza hivi mtu ana nyumba yake imepigwa alama ya X yani inatolewa hiyo nyumba na serikali imeshatoa malipo kwa hao wenye nyumba! Halafu sasa huyo mwenye nyumba akafanya ujanja akatafuta mtu wa mbali sana kutoka mkoani akasema anaiuza na akaja akaiona na kuridhika na wakakubaliana bei wakauziana na kupewa hati ya nyumba.
Na siku serikali wakaja sasa kuzivunja na wewe upo humo na waliwapa siku kadhaa muwe mmeshaondoka na wanajua wameshawalipa nyie na wewe upo humo unajua umenunua nyumba ya milele kwa hela ndefu kweli, hapo wakuu msaada utapata wapi? Ukashtaki sehemu ipi! Na Aliekuuzia alishatoweka labda yupo mkoa mwingine utampata wapi?
Hapo ndio utasema "nobody can stop raggae"
Ipo hivi wakuu, nipo nawaza kitu ambacho kipo ubongoni mwangu nimekifikiria tu ghafla.
Ipo hivi Huku Maeneo ninapoishi jina (kapuni) kuna Uwanja wa ndege ulikuwa wa kitambo na ulikuwa unatumika ila sijui nini kilitokea ndege kubwa hazitui tena zinaishia mkoa jirani, bali ni ndege binafsi ndio zinaruhusiwa kutua sikujua ni kwanini.
Basi serikali imeamua tena kuutengeneza uwe mkubwa sasa kuna nyumba zipo baadhi na kiwanja na kuna mashamba pembeni watu walikuwa wanalima mpunga, viazi, na mboga mboga kwa maana hiyo wanatakiwa watoke.
Basi nikawaza hivi mtu ana nyumba yake imepigwa alama ya X yani inatolewa hiyo nyumba na serikali imeshatoa malipo kwa hao wenye nyumba! Halafu sasa huyo mwenye nyumba akafanya ujanja akatafuta mtu wa mbali sana kutoka mkoani akasema anaiuza na akaja akaiona na kuridhika na wakakubaliana bei wakauziana na kupewa hati ya nyumba.
Na siku serikali wakaja sasa kuzivunja na wewe upo humo na waliwapa siku kadhaa muwe mmeshaondoka na wanajua wameshawalipa nyie na wewe upo humo unajua umenunua nyumba ya milele kwa hela ndefu kweli, hapo wakuu msaada utapata wapi? Ukashtaki sehemu ipi! Na Aliekuuzia alishatoweka labda yupo mkoa mwingine utampata wapi?
Hapo ndio utasema "nobody can stop raggae"