Utapeli huu hakubaliki popote

KIMATIRA

Senior Member
Dec 3, 2015
184
144
Nimemsikiliza mkuu sikumwelewa nafikiri kafanganywa. Huwezi kuzungumza uongo wenye nia mbaya ya kutapeli kiasi mile.

iliitwa kamatu ya maafa Kagera iliratibu misaada yote tena kukiwa na zuio la kupiga marufuku mtu kusaidia ndugu zake.

pesa ikapatikana ikaanza kukarabati shule ya ccm,ikafanya shughuli ambazo watoa misaada hawakulenga na leo zinakuja kauli za ghiliba kuwa serikali itainunua shule ya ccm,kwa nini iinunue?nani atapanga bei? he pesa zikipatikana zitapelekwa ccm au kwa wahanga?

Tanganyika law society mko wapi? Kibatala, lisu,safari, John mallya,rizione mko wapi?
kesi iko wazi kuna kesi ya kuaminiwa hapa. tunataka PESA tulizochanga zikawajengee mama zetu waliopatwa na maafa, ziwajengee wazee wetu waliokosa makazi ziwatibu wadogo zetu walioumia kwenye janga lile.

PESA ya serikali ni ya kujenga miundombinu hilo hàtujalikataa ila za michango ni haki ya wahanga.

Hata kama una kinyongo na watu wa Kagera huwezi kujihalalishia kuchukua haki yao kwa mabavu. Natoa changamoto kwa wanasheria kuitendea haki nchi yao na taaluma yao kuzuia utapeli huu.

Mungu ibariki Tanzania,
Mungu wabariki wahanga wa tetemeko Kagera.
 
una mantiki lakini ndio hivyo tena, kama walivyosema kila mtu atabeba msalaba wake wenyewe....!
 
kirikou-et-les-betes-sauvages.jpg
 
kubeba msalaba tumekubali lakini kuibiwa hela zetu mchana kweupe ndio hatutaki,tena na kashfa juu?kwani jina la mto ngono ni nini? mbona yeye anaitwa mataputapu?
 
Wanasheria watusaidie kama sisi tuliotoa mali na fedha kusaidia wahanga na mtu mwingine akaipangia fedha yetu matumizi mengine tunawezaje kudai vitu na pesa yetu?
 
nimesema hapa,
kama viongozi wetu wataendelea na mfumo wanaouamini wao wa kuwaingoza watanzania kwa kipindi cha miaka kumi. watatengeneza watu wenye roho mbaya na katili kukiko wanavyotegemea.
 
Wasema ukweli ndio wanaotakiwa ndio nchi itakua sawa, Babu mmoja alishasemaga mtu asiyeweza kuendesha familia yake vizuri hata Gari lake awezi kulimudu vizuri.
 
Back
Top Bottom