Utapanyaji huu wa kodi zetu kwa CCM utakoma lini?

Asha Abdala

JF-Expert Member
Mar 21, 2007
1,130
44
Nimeshika Gazeti la Uhuru la leo, mbele yangu yapo pia magazeti mengine ya hapa nyumbani ikiwemo gazeti la serikali la habari leo. Ndani ya gazeti la CCM la uhuru kuna matangazo matano ya serikali ya wizara, idara, wakala na halmashauri tofauti tofauti. Kwa mahesabu ya haraka jumla ya matangazo haya ni kati ya milioni 3 na 4 za kodi za watanzania wote bila kujali itikadi. Ndani ya gazeti la habari leo, gazeti la serikali- ukiondoa hotuba ya waziri. Hakuna hata tangazo moja la ukurasa mzima kati ya yale ambayo yametolewa na serikali katika gazeti la CCM. Huu si ufujaji wa kodi zetu? Kwanini gazeti lenye kufikia wasomaji wasiofikia elfu tano lipewe matangazo yote haya wakati magazeti yanayofikia wasomaji zaidi ya elfu 20 ikiwemo gazeti la serikali kuachwa? Je, huu si mpango kabisa wa kuendesha CCM na taasisi zake kwa kutumia fedha za walipa kodi wa itikadi mbalimbali na wasio na chama? Kuna maana gani kwa serikali kutoa matangazo katika chombo ambacho hakifikii umma wa walio wengi? Ruzuku ya takribani bilioni mbili ambayo CCM inapata kila mwezi inatumika kufanya nini kama bado wanaiba kodi zetu kwa upande wa nyuma kuendesha chama chao halafu wanaendelea kututangazia kuwa serikali haina fedha za kuwasaidia wanawake?
 
Nimeshika Gazeti la Uhuru la leo, mbele yangu yapo pia magazeti mengine ya hapa nyumbani ikiwemo gazeti la serikali la habari leo. Ndani ya gazeti la CCM la uhuru kuna matangazo matano ya serikali ya wizara, idara, wakala na halmashauri tofauti tofauti. Kwa mahesabu ya haraka jumla ya matangazo haya ni kati ya milioni 3 na 4 za kodi za watanzania wote bila kujali itikadi. Ndani ya gazeti la habari leo, gazeti la serikali- ukiondoa hotuba ya waziri. Hakuna hata tangazo moja la ukurasa mzima kati ya yale ambayo yametolewa na serikali katika gazeti la CCM. Huu si ufujaji wa kodi zetu? Kwanini gazeti lenye kufikia wasomaji wasiofikia elfu tano lipewe matangazo yote haya wakati magazeti yanayofikia wasomaji zaidi ya elfu 20 ikiwemo gazeti la serikali kuachwa? Je, huu si mpango kabisa wa kuendesha CCM na taasisi zake kwa kutumia fedha za walipa kodi wa itikadi mbalimbali na wasio na chama? Kuna maana gani kwa serikali kutoa matangazo katika chombo ambacho hakifikii umma wa walio wengi? Ruzuku ya takribani bilioni mbili ambayo CCM inapata kila mwezi inatumika kufanya nini kama bado wanaiba kodi zetu kwa upande wa nyuma kuendesha chama chao halafu wanaendelea kututangazia kuwa serikali haina fedha za kuwasaidia wanawake?

Tehe,tehe,tehe, koh,koh,kwiiiiiiiiiiiii!!! Na wewe dada Asha mtu mzima kabisa utoe pesa zako ununue gazeti la uhuru? Si uharibifu wa pesa zako binafsi? Charity begins at home!!!
 
Tehe,tehe,tehe, koh,koh,kwiiiiiiiiiiiii!!! Na wewe dada Asha mtu mzima kabisa utoe pesa zako ununue gazeti la uhuru? Si uharibifu wa pesa zako binafsi? Charity begins at home!!!

Tatizo sio fedha zangu. Tatizo ni fedha za umma. Ni kwa kununua ndipo nimejua kuwa wanaweka matangazo mengi ya serikali kwenye uhuru kuliko hata gazeti la serikali. We unafurahia unadhani ni sawa? Labda mie Asha sijui. Eti jamani
 
Nimeshika Gazeti la Uhuru la leo, mbele yangu yapo pia magazeti mengine ya hapa nyumbani ikiwemo gazeti la serikali la habari leo. Ndani ya gazeti la CCM la uhuru kuna matangazo matano ya serikali ya wizara, idara, wakala na halmashauri tofauti tofauti. Kwa mahesabu ya haraka jumla ya matangazo haya ni kati ya milioni 3 na 4 za kodi za watanzania wote bila kujali itikadi. Ndani ya gazeti la habari leo, gazeti la serikali- ukiondoa hotuba ya waziri. Hakuna hata tangazo moja la ukurasa mzima kati ya yale ambayo yametolewa na serikali katika gazeti la CCM. Huu si ufujaji wa kodi zetu? Kwanini gazeti lenye kufikia wasomaji wasiofikia elfu tano lipewe matangazo yote haya wakati magazeti yanayofikia wasomaji zaidi ya elfu 20 ikiwemo gazeti la serikali kuachwa? Je, huu si mpango kabisa wa kuendesha CCM na taasisi zake kwa kutumia fedha za walipa kodi wa itikadi mbalimbali na wasio na chama? Kuna maana gani kwa serikali kutoa matangazo katika chombo ambacho hakifikii umma wa walio wengi? Ruzuku ya takribani bilioni mbili ambayo CCM inapata kila mwezi inatumika kufanya nini kama bado wanaiba kodi zetu kwa upande wa nyuma kuendesha chama chao halafu wanaendelea kututangazia kuwa serikali haina fedha za kuwasaidia wanawake?
ASHA mara nyingi nimekua nikikuaambia acha kukurupuka.Naomba ujue kua kampuni,Taasisi inapo amua kutoa matangazo inatengeneza PR plan kwa ajili ya either campaing or whetever,

Sasa withdue respect kabla hujasema kua CCM wanaiba Pesa za walipa kodi ni vizuri ungefanya jitihada kidogo kujua kwa nini hao waliotangaza wametumia GAZETI la UHURU may be hawataki tangazo liwafikie watu wengi,or kuna aina ya wasomaji ambao wame watarget.

Ni vizuri ukaacha kuongozwa na HISIA,or CHUKI, or ITIKADI unapo jenga hoja yako.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
ASHA mara nyingi nimekua nikikuaambia acha kukurupuka.Naomba ujue kua kampuni,Taasisi inapo amua kutoa matangazo inatengeneza PR plan kwa ajili ya either campaing or whetever,

Sasa withdue respect kabla hujasema kua CCM wanaiba Pesa za walipa kodi ni vizuri ungefanya jitihada kidogo kujua kwa nini hao waliotangaza wametumia GAZETI la UHURU may be hawataki tangazo liwafikie watu wengi,or kuna aina ya wasomaji ambao wame watarget.

Ni vizuri ukaacha kuongozwa na HISIA,or CHUKI, or ITIKADI unapo jenga hoja yako.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI




Talk about PR plan…..

Matangazo yaliyokuwepo siku hiyo ya Januari 7 kwenye gazeti la UHURU la CCM ambayo hayakuwepo kwenye magazeti mengine ikiwemo HABARILEO la Serikali.

BOT- mnada wa Treasury Bills; je wateja wake wanasoma UHURU la CCM? BOT ijieleze na kufafanua hiyo PR plan yao.

Kwimba district council- mahesabu yao ya mwaka. Wilaya ijieleze kwa nini imetoa tangazo hilo kwa UHURU la CCM wakati nakala za UHURU zinazouzwa Kwimba kwa siku hazizidi hamsini.

TRA- taarifa kwa umma kuhusu TIN; umma gani wakati UHURU linasomwa na watu wasiozidi elfu tano tena wengi wao wakiwa wanaCCM? TRA ijieleze hiyo PR plan.

Mahakama ya Kisutu- tangazo la kuitwa Mahakamani- wahusika watalisomaje wakati wananchi wengi hawasomi UHURU? Kuna orodha ya wanachi 132 ambao mahakama imewataja majina. Sasa kama ni watu wa itikadi nyingine hawasomi UHURU si mtawafunga?

TRA- Tangazo la mnada- tangazo ni kwa wananchi wote lakini mnalitoa kwenye gazeti la CCM? Hamuoni kama vile mnatangaza mnada kwa wanaCCM tu?

Na haya ni matangazo ya ukurasa mzima mzima. Mmewalipa bei gani UHURU kwa matangazo haya? Tukisema kwamba ni mpango tu wa kuchota fedha kuwalipa mishahara waandishi wa CCM kwa mlango wa nyuma tutakuwa tumekosea?

Tupeni hiyo PR plan yenu inayohalalisha ufujaji wakati ambapo tafiti zote zinaonyesha UHURU halisomwi na watu wengi. Nyinyi mnajua kama usingekuwa huu ufisadi wa kuwapa matangazo hili gazeti lingekufa; kwanini CCM msikubali kuendesha kwa hasara kwa kulipatia ruzuku yenu ya kila mwezi badala ya kuiba fedha za walipa kodi?

Je, ni PR plan ya serikali kujipendekeza kwa CCM?

Talk about Asha kukurupuka eeeeeehhhhh. Una laana ya CCM wewe
 
Mkurugenzi ambaye anafanya kazi kwa kutumia kanuni nzuri za kazi, huweka tangazo la kampuni au shirika lake kwenye vyombo vya habari kwa kusudi la kuwafikia watu wengi iwezekanavyo. Kwa msingi huo, atachagua magazeti yale ambavyo yanasomwa na walengwa wengi zaidi.

Sasa kuna wanaofanya kazi kwa msingi wa kujikomba. Hao ni watu hatari sana kwa makampuni na mashirika yao. Hakuna shaka hao waliomkera Asha Abdala ni wa aina hiyo. Wameweka matangazo yao kwenye gazeti la UHURU kama njia ya kujikomba kwa CCM. Wanaacha kuangalia maslahi ya mashirika au makampuni yao na kuendeleza kujikomba kwa CCM. These are cheap bootlickers, full stop.
 
hao waliotangaza wametumia GAZETI la UHURU may be hawataki tangazo liwafikie watu wengi,or kuna aina ya wasomaji ambao wame watarget.

Huyu mtu anayetangaza halafu hataki hilo tangazo liwafikie watu wengi ni kichaa au kalogwa? Sasa hapa nani anakurupuka, wewe au Asha aliyekuja na uchanganuzi makini? Nafikiria wewe ndio unatakiwa utulie kidogo kabla hujashika keyboard!
 
Dada Asha hizo namba za nakala elfu tano ni sahihi au unazitumia kufikisha ujumbe kuwa Uhuru halisomwi sana?

Nilitaka kujua digrii ya ujinga huu, ni wazi kuwa matangazo yanatolewa kwa upendeleo unaotokana na itikadi za kisiasa.
 
Huyu mtu anayetangaza halafu hataki hilo tangazo liwafikie watu wengi ni kichaa au kalogwa? Sasa hapa nani anakurupuka, wewe au Asha aliyekuja na uchanganuzi makini? Nafikiria wewe ndio unatakiwa utulie kidogo kabla hujashika keyboard!

Kabisa.
Asha ako sahihi. Wizara na idara zote za sirikali ni mali ya WATANZANIA wote sio mali ya sisi M, ndio maana wizara hizi hazihudumii watu kutokana na itikadi zao za vyama bali UTANZANIA wao. Sasa inapotokea kwamba matangazo ya wizara na idara za WATANZANIA yanapelekwa kwenye gazeti LA CHAMA lazima tuulize huu walakini. Pointi ya Asha mimi naiona katika hoja hii. Kwamba kama ni suala la kuwafikishia habari WATANZANIA lazima haya matangazo yapelekwe kwenye vyombo wakilishi vya WATANZANIA. Sasa kama unapeleka matangazo RTD peke yake wakati kuna mahali hawasikiki kabisa itakuwa ni uharamia.
 
Mie ninaona huu ni mkakati wa ku-support Gazeti la Uhuru, it has nothing to do with the readership or coverage of the newspaper.
 
Back
Top Bottom