mmmh! Kuamini hii inabidi bibie awe na kichwa cha panzi.Situation kama hizi inabidi huwe mwepesi wa kufikiri....,ungecheka saaana alafu ukasema kumbe kweli unanipenda.., yaani umeshinda mtego, tulipanga na rafiki yangu tukupime.., hivi kweli wife ningekuwa nategemea sms kama hiyo unadhani ningeacha simu chumbani.., dah kumbe mshikaji alisema kweli mi nilisema wife hawezi kukubali mtego mdogo hivi..., dah wife embu twende tukalale......
Situation kama hizi inabidi huwe mwepesi wa kufikiri....,
ungecheka saaana alafu ukasema kumbe kweli unanipenda.., yaani umeshinda mtego, tulipanga na rafiki yangu tukupime.., hivi kweli wife ningekuwa nategemea sms kama hiyo unadhani ningeacha simu chumbani.., dah kumbe mshikaji alisema kweli mi nilisema wife hawezi kukubali mtego mdogo hivi..., dah wife embu twende tukalale......
to some extent uliamua vyema kuondoka ili ugomvi usiwe wa kijiji. Rudi home atakuwa keshapoa akigomba kalete mkeka lala chini tena bila cha kujifunika,mara 2 atalainika atakufata hapo hapo chini...baba naniliuh twende kalale kitandani....hapo unatumia nafasi vizuri ktk kuleta suluhu na utani tani uachage bwana!Unajua kilichonifanya mimi niondoke nyumbani ilikuwa ni kunusuru ule ugonvi usije ukaanza kukusanya watu pale nyumbani. Mkuu jitahidi sana masuala ya ndani kwako yasitoke nje. Kwa gharama yoyote ile. Suala la ugomvi ndani ya nyumba yako na mkeo likakusanya watu nyumbani kwako mpaka wanavunja mlango ni la aibu sana na halitakaa liwatoke hao majirani kichwani mwao. Na watalitumia kila mahali wakiwaona mna furaha. Utasikia "Unaowaona hawa sasa hivi wana furaha, usiku tunaweza tusilale kwa ugomvi wao". hapo mpo kwenye harusi na mamsap mnacheza "Embe dodo limelala mchangani" mmeshasahau ya nyuma, wenzenu wanatumia kama weak point. Ni vyema sana kuhakikisha ugomvi wa ndani kwako haswa na mkeo hautoki nje. Maana mara zote uwezekano wa kuelewana na mkeo na kurudi katika maisha ya kama zamani ni mkubwa. Majirani huwa wanachukulia huo ugomvi kama weak point ya kuwatangaza vibaya.
Kuna msichana nafanya naye kazi katika kampuni moja. Sasa tumezoea kweli kutaniana na kuitana majina ya Kimahaba huku kukiwa hakuna uhusiano wowote wa Kimapenzi. Jana saa nne usiku nikiwa nafanya kazi zangu kwenye kompyuta sebuleni na simu ikiwa chumbani akanitumia ujumbe unaosomeka "Honey, its too cold today, I wish you could be beside me now, I cant Imagine how the situation could be". Aisee, mama watoto alikuwa kajipumzikia kitandani huyoo akaamka na kwenda mezani, akachukua simu na kusoma meseji. Kilichojiri hapo nilisikia mlango wa chumbani umefunguliwa, baadaye nikasikia paa, nimepigwa kofi zito la shavuni. Nilipozinduka nikamkuta analia, akaniambia haya twende chumbani ukavae uende ukampe joto huyo malaya wako. Nikasita, nikapigwa tena kofi la begani na kuambiwa nyanyukaaaa, malaya mkubwa wewe. Unataka kuniuwa niache watoto wanakula shida na malaya zako. Kwa kweli ilikuwa ni zengwe sana. na leo nimemkia hotel, baada ya kuona vurugu inataka kuanza kushirikisha majirani. Wife amekataa kabisa kunielewa, leo nimempigia simu hapokei, meseji hajibu binti nimemueleza yaliyonikuta kwa sababu ya ushenzi wake anachekacheka tu, natamani nimmeze kwa kweli. Natafakari nielekee wapi nkitoka hapa kazini.Nawasilisha kwa ushauri.
Kuna msichana nafanya naye kazi katika kampuni moja. Sasa tumezoea kweli kutaniana na kuitana majina ya Kimahaba huku kukiwa hakuna uhusiano wowote wa Kimapenzi. Jana saa nne usiku nikiwa nafanya kazi zangu kwenye kompyuta sebuleni na simu ikiwa chumbani akanitumia ujumbe unaosomeka "Honey, its too cold today, I wish you could be beside me now, I cant Imagine how the situation could be". Aisee, mama watoto alikuwa kajipumzikia kitandani huyoo akaamka na kwenda mezani, akachukua simu na kusoma meseji. Kilichojiri hapo nilisikia mlango wa chumbani umefunguliwa, baadaye nikasikia paa, nimepigwa kofi zito la shavuni. Nilipozinduka nikamkuta analia, akaniambia haya twende chumbani ukavae uende ukampe joto huyo malaya wako. Nikasita, nikapigwa tena kofi la begani na kuambiwa nyanyukaaaa, malaya mkubwa wewe. Unataka kuniuwa niache watoto wanakula shida na malaya zako. Kwa kweli ilikuwa ni zengwe sana. na leo nimemkia hotel, baada ya kuona vurugu inataka kuanza kushirikisha majirani. Wife amekataa kabisa kunielewa, leo nimempigia simu hapokei, meseji hajibu binti nimemueleza yaliyonikuta kwa sababu ya ushenzi wake anachekacheka tu, natamani nimmeze kwa kweli. Natafakari nielekee wapi nkitoka hapa kazini.Nawasilisha kwa ushauri.
Mama makonde yalizidi jamaa kaona bora aokoe uso wake, yaonekana huyo mama ni noma...jamaa mpaka kakimbia ULINGO...huyo atakuwa ASHA NGEDERE nini
Mhh kaka kumbe na wewe umekaliwa hivyo unazabwa vibao?pole kwa yaliyokukuta wenzio tukifika home huwa tunazima simu mpaka asubuhi
Halafu wewe.........Kesi yetu tafuta wakili mzungu!Khaaaa!
Wewe nae unamwona mangi kakaliwa? Mbona hata wewe umekaliwa pia? Why uzime cm kama sio unaogopa vibao? Kuzima cm ni ishara ya WOGA kwa wife, kama unajiamini acha cm on tena chumbani afu kakae sebuleni km hayajakukuta yaliyomkuta mangi.
Halafu wewe.........Kesi yetu tafuta wakili mzungu!
kesi hiyo. Umejuaje kama mkewe mwelewa.. *Najua* mkeo ni muelewa, atakuelewa tu.
Unajua sometimes ukweli unaonekana ni uongo kuliko ukweli.., kwahiyo hapo mtu inabidi ufanye kila kitu ili kuokoa ndoa, na hapo akili inabidi ifanye kazi..., kwahiyo angeanza kwa kucheka sana angekuwa anacheka huku akili inafanya kaziMhhhh!!! VoR, kama hujazoea kusema uongo sio rahisi kupata mawazo kama hayo! Labda awe ni mzoefu, kwahiyo lazima ajiandae kwa situatio kama hiyo! Otherwise utabaki unashangaa tu........