Utani na Msichana ninaye fanya naye kazi unataka kunivunjia ndoa yangu

Kwanza ulifanya kosa kuondoka nyumbani, maana yake unamwongezea machungu mke wako! maana atajua tu umeenda hukooooo.....! Kama kweli unampenda mke wako, basi rudi nyumbani kaongee naye. Hope atakuwa ametulia, atakuelewa na kukusamehe. Ila ujifunze kwa hilo lililotokea! Pole sana.
 
Kaka mi sina msaada ila chanzo wewe kwanini huwa unamruhusu mkeo kufungua msg zako? Huo ndio upumbavu wako.
Ndugu ni vigumu sana kumzuia mke kutokuperuzi kwenye simu. Mfano unaweza ukawa umelala na mama watoto jumamosi/jumapili mchana mkifurahia mapumziko ya week end. Ghafla mtoto anakuja na kuanza kulia mlangoni. Mama anakwambia kambeleze acheze na dada yake. Kwa kuwa wewe unataka kuutumia huo mchana kumbembeleza mama watoto kitandani unakwenda kucheza na mtoto mpaka analala. Huku nyuma umeiacha simu kitandani, mama anapekua sms moja baada ya nyingine. Hivyo hivyo na usiku ukiwa umelala simu ipo pembeni kitandani, mama anaamka zake wakati wewe umemzungushia mikono kiuononi unakoroma yeye anapekua simu. Its difficult to prohibit your wife from touching your phone. Stoping your wife from touching your phone rises also questions from her side.
 
Hivi huo kweli ni utani au huyo msichana anakutaka kimapenzi? kwanini atume msg ya aina hiyo tena muda huo??? Hata mimi lingekuwa varangati hapo. Hebu tujifunze jamani,utani gani unamuita mke wa mtu mpenzi, honey, sweetie, darling na mengineyo? huyo mwanamke alijua anaachokifanya ndio maana katuma msg usiku alijua fika mkeo ataiona. Yaani jioni yangu imekuwa mbaya ghafla!!!!!!! khaaaaaaaaaa
 
pole mkaka ila ww umeyataka mwenyewe na matan ya kijinga jinga na huyo bint, sasa kama kwel hana hisia zozote juu yako kwa nn
acheke cheke pia kama ni rafik yako tu mwambie aje kukusaidia kumbembeleza huyo mkeo.[/QUOTE

unalalamika nini sasa? hapo ni wote mnatamaniana. kama usingependa you should have stopped her right from the beginning. matani mengine hayana tija. sana sana ni kuharibiana ndoa tu maana vibinti siku hizi navyo viko sharp sana kutongoza waume za watu. jamani tafuteni wasiooa wakuoeni.]
 
Utalijua jiji!nani alikuambia uoe mmachame?kwa waliooa mwisho wa kupigiana na simu na meseji ni saa 10 kamili jioni!ukifika zako hm unaiweka simu sebuleni unaenda zako room raha mustarehe!amani na upendo ndani ya nyumba!

Pole kwa matatizo ila akina mama ni wepes kusamehe!wewe nenda zako hm akiuchuna poa tuu!Atauchuna atachoka atazungumza mwenyewe!
 
Kaka mi sina msaada ila chanzo wewe kwanini huwa unamruhusu mkeo kufungua msg zako? Huo ndio upumbavu wako.

mkuu hapo hajafanya kosa...mkeo ni mkeo na ana full access kwenye simu yako...Je, wewe mkeo akifungua msg zako utampiga? Kuweni watu walioelimika...mambo ya Umimi ya kizamani...
 
Kwanza ulifanya kosa kuondoka nyumbani, maana yake unamwongezea machungu mke wako! maana atajua tu umeenda hukooooo.....! Kama kweli unampenda mke wako, basi rudi nyumbani kaongee naye. Hope atakuwa ametulia, atakuelewa na kukusamehe. Ila ujifunze kwa hilo lililotokea! Pole sana.

Mama makonde yalizidi jamaa kaona bora aokoe uso wake, yaonekana huyo mama ni noma...jamaa mpaka kakimbia ULINGO...huyo atakuwa ASHA NGEDERE nini
 
hongera kwa yaliyokukuta wala siyo pole tena umeyataka mwenyewe uliweka mwanya tokea mwanzo.
 
Mkuu, una moyo!! Yaani unakimbia nyumba yako kwa ajili ya kitu ambacho unajua kiuhalisia siyo cha kweli? Mimi piga ua siondoki nyumbani kwangu. Kama yeye anaona mimi nitamuua basi aondoke aniachie nyumba na watoto wangu. Kwanza huyo mwanamke naye ni balaa, hadi anaweza kukukata kibao? Mkuu inaonekana umemdekeza huyo.
 
Utalijua jiji!nani alikuambia uoe mmachame?kwa waliooa mwisho wa kupigiana na simu na meseji ni saa 10 kamili jioni!ukifika zako hm unaiweka simu sebuleni unaenda zako room raha mustarehe!amani na upendo ndani ya nyumba!

Pole kwa matatizo ila akina mama ni wepes kusamehe!wewe nenda zako hm akiuchuna poa tuu!Atauchuna atachoka atazungumza mwenyewe!

Hivieee!?????????!
 
Utalijua jiji!nani alikuambia uoe mmachame?kwa waliooa mwisho wa kupigiana na simu na meseji ni saa 10 kamili jioni!ukifika zako hm unaiweka simu sebuleni unaenda zako room raha mustarehe!amani na upendo ndani ya nyumba!Pole kwa matatizo ila akina mama ni wepes kusamehe!wewe nenda zako hm akiuchuna poa tuu!Atauchuna atachoka atazungumza mwenyewe!
Hebu watake radhi wamachame! Mimi nimeoa mmachame na maisha ywtu shwariiiii!
 
Pole sana mkuu,
Ulipokosea wewe ni kuondoka nyumbani. Rudi nyumbani haraka na umuombe msamaha maana hilo ni kosa. Hata mimi mkuu yamesha nikumba hayo hayo na imenifanya sasa niache kabisa mizaha na watoto wa kike. hawa viumbe siku hizi hawataniwi wamekuwa kama maharage ya mbeya maji mara moja.
Pole sana mkuu,
 
1.Mkuu,samahani,akili yangu inaniambia huyu binti ni wako ila mmefumaniwa,POLE.
2.Umefanya kosa kubwa sana kuondoka nyumbani....anakwambia nenda kwa malaya wako na UNAENDA KWELI...MWE!!!!!!!
3.Hapo mke huna tena,akikusamehe basi subiri akuzalie hadi mtoto wa nje..........
4.Solution....mwache kwanza atulieeee hasira zake zikiisha sikiliza anaamua nini...lakini kila siku omba msamaha kama mara mia moja hivi.
 
Hebu watake radhi wamachame! Mimi nimeoa mmachame na maisha ywtu shwariiiii!

Mimi nimeshtuka kusikia hivyo ila kwa sababu sina facts nimebaki kuguna tu!!!
Asavali umesema...one of my investments ni mmachame sasa nlishaanza kuogopa.
 
mkuu, una moyo!! Yaani unakimbia nyumba yako kwa ajili ya kitu ambacho unajua kiuhalisia siyo cha kweli? Mimi piga ua siondoki nyumbani kwangu. Kama yeye anaona mimi nitamuua basi aondoke aniachie nyumba na watoto wangu. Kwanza huyo mwanamke naye ni balaa, hadi anaweza kukukata kibao? Mkuu inaonekana umemdekeza huyo.
ana moyo gani??? Huyu ni wake wa siku zote,baada ya kuona yamejulikana kahamia kabisa nyumba ndogo wala sio hoteli.
 
Pole sana mkuu,Ulipokosea wewe ni kuondoka nyumbani. Rudi nyumbani haraka na umuombe msamaha maana hilo ni kosa. Hata mimi mkuu yamesha nikumba hayo hayo na imenifanya sasa niache kabisa mizaha na watoto wa kike. hawa viumbe siku hizi hawataniwi wamekuwa kama maharage ya mbeya maji mara moja.Pole sana mkuu,
Unajua kilichonifanya mimi niondoke nyumbani ilikuwa ni kunusuru ule ugonvi usije ukaanza kukusanya watu pale nyumbani. Mkuu jitahidi sana masuala ya ndani kwako yasitoke nje. Kwa gharama yoyote ile. Suala la ugomvi ndani ya nyumba yako na mkeo likakusanya watu nyumbani kwako mpaka wanavunja mlango ni la aibu sana na halitakaa liwatoke hao majirani kichwani mwao. Na watalitumia kila mahali wakiwaona mna furaha. Utasikia "Unaowaona hawa sasa hivi wana furaha, usiku tunaweza tusilale kwa ugomvi wao". hapo mpo kwenye harusi na mamsap mnacheza "Embe dodo limelala mchangani" mmeshasahau ya nyuma, wenzenu wanatumia kama weak point. Ni vyema sana kuhakikisha ugomvi wa ndani kwako haswa na mkeo hautoki nje. Maana mara zote uwezekano wa kuelewana na mkeo na kurudi katika maisha ya kama zamani ni mkubwa. Majirani huwa wanachukulia huo ugomvi kama weak point ya kuwatangaza vibaya.
 
Back
Top Bottom