wakatanta
JF-Expert Member
- Feb 5, 2018
- 2,593
- 3,148
Mada hapa sio vyombo vya dola ,bali ni shujaa wa Taifa ,hayati Magufuli,hatatoka vinywani mwetu daima ,na alisema mtamkubuka,ndio kumkumbuka kwenyewe huku,hutaki achaWadau nawasalimu wote Kila mmoja kwa imani na itikadi yake.
Baada ya salamu napenda kujikita katika kufafanua mada Kama kichwa Cha uzi kinavyojieleza.
Wote Ni mashahidi katika awamu ya tano tuliona jinsi vyombo vya Dola hasa tiss na polisi vilivyotumika kumlinda RAISI magufuli hasa chama Cha ccm ili kibaki madarakani kwa nguvu kubwa mno.
Tulishuhudia wakuu wa mikoa na wilaya wengi wakiteuliwa kutokea upande huo yaani teeth, na wanajeshi Jambo hili si baya ila nia na malengo ya Mamlaka pengine ndiyo iliyoleta maswali mengi.
Tulishuhudia wanajeshi wakisombeshwa korosho kusini na matokeo yake tumeyaona wote, tulishuhudia jinsi ccm ikiongozwa na katibu mkuu wa kipindi hicho bwana BASHIRU alivyovitumia vyombo hivyo vya Dola hasa polisi na teeth kujibakisha madarakani na mengine Kama hayo.
Ni ukweli kwamba kiongozi au Chama chochote Cha siasa kinapokosa uhalali na ushawishi kwa wananchi hujigeuza chama Dola ili angalau kisalie kwa kitambo kidogo TU
Ni ukweli kwamba ccm kwa Sasa Ni chama Dola na raisi yeyote atakayekuwa Ni kivuli TU. Chama na viongozi wake hufikiri kwamba kujiunganisha na Dola ndio salama yao kumbe hali hii huwa tofauti kabisa, historia inayoonyesha hivyo.
Ni ukweli kwamba viongozi wengi wa kuchaguliwa wanatambua wapo Hapo si kwa jeuri,uwezo, ushawishi,uhalali au nguvu zao Basi Ni vyombo vya Dola hasa polisi na hayati magufuli.
Ni ukweli kwamba viongozi wakuu vya Hivi vyombo vya Dola, serikali, ccm na wanaccm wenye kutafakari wanatambua kwamba ccm haikubaliki Tena na HAKUNA njia mbadala zaidi ya kutumia Dola
Ni ukweli kwa jeshi la polisi linatambua viongozi wengi hasa wabunge na madawani wapo kwenye nafasi hizo si kwa jasho lao Bali kwa jasho la jeshi la polisi na polisi mmoja mmoja, na hii ndio point mbaya kuliko zote kwani ukitazama mwenendo wa jeshi la polisi kwa Sasa Ni Kama umejaa kiburi jeuri na ukatili kwani wanajua viongozi wengi wapo pale kwa jasho lao polisi.
Ni ukweli kwamba huu muungano wa jeshi la polisi na ccm unakwenda kuzaa kitu kipya kwa nchi yetu Tanzania, utamu na tamaa ya madaraka inazidi kujengeka ndani ya dhamiri zao na matokeo ya tamaa hiyo wote hatukuwa salama.
Ni ukweli kwamba unapokaribia mwisho wa chama siasa hujigeuza dola na hatimaye hujigeuza watesaji kwa raia wote si upinzani TU na mwisho Hujigeuza magaidi wa kidola na mwisho kabisa makamanda wetu wananchi (JWTZ) huchukua dola kwa mda ili kuandaa mazingira ya Taifa jipya ( naona hivyo)
NA UKWELI NI KWAMBA WOTE WANAOZUIA KATIBA MPYA KWA VIJISABABU VYA AJABU NDIO WENYE UCHU WA MADARAKA, MAADUI WA TAIFA LETU NA NDIO MAGAIDI, HAWALITAKII MEMA TAIFA N.K pointi Kila mwananchi asomaye na aelewe.
Na Ni ukweli kwamba matokeo ya chama kujiungamanisha na Dolana kuwaacha wananchi upande wa pili huwa ni mapinduzi ya kijeshi au Vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Watanzania na viongozi wenye hekima wa Taifa letu pendwa tunakoipeleka tz wote tutaumia, vyama vingi tulikubali wenyewe na Kama tumeshindwa mbona mna Mamlaka kwani Nini msivifute? Kuliko kufungana, kuuana,kutesana na kumbakiana kesi, kumbukeni chama tawala vyama Hivi vimezalisha ajira nyingi Sana kwa watanzania yaani Ni sifa kwa chama Cha ccm kutengeneza hizo ajira mnataka kuvivuruga ili hata hizo ajira zipotee? Kwa wimbi la vijana wengi wasio na ajira Ni hatari kwa usalama wa Taifa.
Pole Sana mh. Rais mama yetu Samia suluhu ninajua kwa huu muungano wa chama chako na dola kunakupa wakati mgumu Sana kutimiza malengo yako najua unajua kula na vipofu bila kuwashika mikono
Nb: CHAMA+ DOLA= MAPINDUZI note that.