Indume Yene
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 2,950
- 711
Imenishangaza sana kukutana na habari moja katika gazeti la Mtanzania Daima (7 Janauari, 2009). Katika habari hiyo yenye kichwa cha habari kisemacho "Bashe Awashukia Wanaomtuhumu Mkapa" Hussein Bashe ambaye ni MJUMBE wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), anadai watu wanaomhusisha Rais mstaafu, Benjamin Mkapa na ubadhirifu wamefilisika kisiasa. Hivi kweli huu ndo uhondo wa Ukada, ukereketwa au UTAJO!!Huyu mkereketwa wa SISIEMU anaendelea kudai kuwa wote wanaomuandama Mkapa ni wanasiasa wavivu wa kufikiri na wanajitafutia umaarufu wa kisiasa. Akifunga Mkutano wa Baraza Kuu la Vijana wa Chama cha SISIEMU wilayani Kinondoni kada huyo alidai nanukuu Muacheni Mkapa apumzike, mengi ameyafanya kwa nchi hii watu wanalalamika tu kila kukicha, inashangaza kusikia kauli ya Spika kuwa atapokea hoja binafsi kuhusu Kumjadili Mkapa bungeni, hivi kuna mangapi ya msingi ya kuzumgumziwa bungeni badala ya kufikiria kumjadili Mkapa"
Yaani kumjadili Mkapa Bungeni si muhimu kwa mujibu wa huyu Bashe. Mie siamini kama huyu Bashe sijui Basha ni mvivu wa kufikiri kama anavyodhani watanzania wako hivyo, bali MAJI ya BENDERA anayokunywa ni MATAMU kuliko taabu wanazozipata WATANZANIA kutokana na UFISADI aliofanya Mkapa na Kampuni yake.
Sitaki kusikia wala kuambiwa kuwa Mkapa hakujua lolote jinsi Yona au Mramba walipokuwa wakitoa misamaha ya kodi kwa wafanyabiashara mbalimbali na kupotezea Taifa mapato. Ni Rais gani hujui kuwa nchi yako inapoteza mali kiasi gani kutokana na uzembe. That means you're not a good Manager.
Sitaki kuambiwa kuwa Mkapa alipokuwa anajizolea Kiwira alikuwa hajui kama anakiuka Katiba. CONSTITUION IS SUPREME LAW OF THE LAND. Hawezi kuachiwa afanye anavyotaka kinyume na Katiba. Alikula kiapo kuwa atailinda na kuitetea KATIBA ya JMT. Sasa iweje aachiwe wakati kaivunja katiba?
Sitaki kuamini kuwa Bashe or Basha whatever anaweza kumpa Pressure Spika Sitta hasisikilize hoja ya kumchukulia hatua za kinidhamu Fisadi Mkapa. Haya Maji ya Bendera especially ya SISIEMU yasiwagawe watu kwenye makundi ya walio juu na chini ya sheria. Basha Bashe kumbuka kuwa uchaguzi Mkuu unakuja, na watanzania si wale wa miaka ya 1922 wa kudanganywa kwa sufuria la pilau.
Kama wewe umeneemeka jitahidi kwa kutumia nafasi yako uneemeshe watanzania wengine ambao wanaishi kwa TAABU. Ufisadi wa Mkapa na fisadiz wenzake wamechangia kwa kiasi kikubwa Matazizo ya wananchi. Wanafunzi vyuo vikuu wanakosa udhamini, kisa serikali haina pesa, kila kitu serikali haina pesa. Lakini kwenye sherehe za kumfunda binti wa JK magari kibao ya serikali hayo Bagamoyo. Hizi pesa zinatoka wapi??
Mkapa ni fisadi na ni busara afikishwe kwenye vyombo husika.
Yaani kumjadili Mkapa Bungeni si muhimu kwa mujibu wa huyu Bashe. Mie siamini kama huyu Bashe sijui Basha ni mvivu wa kufikiri kama anavyodhani watanzania wako hivyo, bali MAJI ya BENDERA anayokunywa ni MATAMU kuliko taabu wanazozipata WATANZANIA kutokana na UFISADI aliofanya Mkapa na Kampuni yake.
Sitaki kusikia wala kuambiwa kuwa Mkapa hakujua lolote jinsi Yona au Mramba walipokuwa wakitoa misamaha ya kodi kwa wafanyabiashara mbalimbali na kupotezea Taifa mapato. Ni Rais gani hujui kuwa nchi yako inapoteza mali kiasi gani kutokana na uzembe. That means you're not a good Manager.
Sitaki kuambiwa kuwa Mkapa alipokuwa anajizolea Kiwira alikuwa hajui kama anakiuka Katiba. CONSTITUION IS SUPREME LAW OF THE LAND. Hawezi kuachiwa afanye anavyotaka kinyume na Katiba. Alikula kiapo kuwa atailinda na kuitetea KATIBA ya JMT. Sasa iweje aachiwe wakati kaivunja katiba?
Sitaki kuamini kuwa Bashe or Basha whatever anaweza kumpa Pressure Spika Sitta hasisikilize hoja ya kumchukulia hatua za kinidhamu Fisadi Mkapa. Haya Maji ya Bendera especially ya SISIEMU yasiwagawe watu kwenye makundi ya walio juu na chini ya sheria. Basha Bashe kumbuka kuwa uchaguzi Mkuu unakuja, na watanzania si wale wa miaka ya 1922 wa kudanganywa kwa sufuria la pilau.
Kama wewe umeneemeka jitahidi kwa kutumia nafasi yako uneemeshe watanzania wengine ambao wanaishi kwa TAABU. Ufisadi wa Mkapa na fisadiz wenzake wamechangia kwa kiasi kikubwa Matazizo ya wananchi. Wanafunzi vyuo vikuu wanakosa udhamini, kisa serikali haina pesa, kila kitu serikali haina pesa. Lakini kwenye sherehe za kumfunda binti wa JK magari kibao ya serikali hayo Bagamoyo. Hizi pesa zinatoka wapi??
Mkapa ni fisadi na ni busara afikishwe kwenye vyombo husika.
Last edited: