UNDENIABLE
JF-Expert Member
- Feb 26, 2013
- 2,326
- 1,314
Km vile magu alivyo na uhakika wa 2020 tena hahahahaNaheshimu maoni yako na naomba ukubali kutokukubiliana, mara nyingi huwa sijadili na wewe chochote maana nimekuzoea kama mzee wa kubeza beza asiyeandika chochote cha msingi. Leo nafurahi umejitutumua na kuandika aya kadhaa, ina maana upo tayari kujadili mada, tatizo nilibanwa na kazi sana leo.
Mchango wako huu wa leo naona umekua wimbo mtamu sana kwa makada wa CCM maana wao kila wakiskia katiba mpya huishia kuweweseka.
Waliobuni mifumo ya katiba dunia hii walikua na akili sana, maana kuna baadhi ya jamii bila kuendeshwa kikatiba wanaishia kuzunguka mbuyu. Husasan jamii zetu za Kiafrika, ni kweli tumeiga wenzetu kwa kila kitu ikiwemo jinsi tunakula na hata tunavyochamba lakini kwa kuiga katiba ndio kitu kizuri tulichofanya maana Mwafrika bila sheria huwa kama mnyama.
Kwa kifupi, katiba yetu mpya imetufaidi sana, nchi yetu tunaona maendeleo yakifika pembe zote za nchi, gatuzi na mikoa yote ikijiamulia vipau mbele vyao bila kupangiwa na Nairobi kama tunavyoona kwenu uwanja mkubwa wa ndege usiokua na maana unajengwa Chato wakati watu wa hapo Chato vipau mbele vyao ni tofauti sana na huo uwanja, pia tunashuhudia jinsi dola yetu inavydhibitiwa na kukwepa uongozi wa kiimla ambao tunauona kwenye nchi zote zilizotuzunguka.
Hayo ya kusema kwamba watu wanapiga kura bila kujua maana yake, sio sababu tosha yakutufanya tutelekeze mfumo huu wa katiba unaotutoa kwa kasi. Taratibu wananchi wanaendelea kupata elimu na kuanza kuhisi umuhimu wa kura zao, hamna kitu kizuri kama kutikisa dola, kuweka rais kwenye mkao wa kuogopa kutupwa nje muda wowote, anaishia kutenda na kufanya kazi kwa bidii, sio kama marais ambao wana uhakika wa kuwa madarakani hadi kifo chao.
Suala la watu kupiga kura bila kuzingatia vigezo vyenye tija ni jambo la kawaida hata kwenye nchi zilizokomaa kidemokrasia kama Marekani, kule unakuta kuna mamilioni ya Wamarekani ambao huegemea kwenye milengo yao na huwambii kitu, kama yeye Democrat hajali hata kama mtateua nguruwe igombee urais kwa tikiti ya chama hicho, na taswira ndio hiyo hiyo kwa Republicans.