Utamu wa Heroin- Beware

Kana-Ka-Nsungu

JF-Expert Member
Oct 4, 2007
2,257
353
Heroin, ambayo pia inajulikana pia kwa majina ya Brown, Smack and Skag kwa UK, ni dawa ambayo hutengenezwa kutoka kwenye mmea uitwao opium poppy. Hutumika kama kama dawa ya maumivu. Mitaani huuzwa kwenye vijipakti vidogo ikiwa katika hali ya ungaunga wa brauni.

Watumiaji wa heroin huivuta kama sigara au bangi kwa kutumia pipes au yale makaratasi ya jikoni ya silver, wengine hujidunga kwa kutumia sindano. Wengi wanaovuta huapa kwamba hawatathubutu kujidunga lakini mara nyingi nao huingia kwenye mchezo wa sindano kwa kuwa ndio njia bomba zaidi kwa kupata steam ya chapchap na yenye kukupa thamani halisi ya fedha zako.

Kwa wanaoanza kutumia heroin kwa mara ya kwanza husikia joto, hupata muwasho wa ngozi na kutapika kwa sana. Wengi husema inahitaji kutumia mara kadhaa kabla ya kuanza kuipenda na kunogewa. Kama nilivyosema hapo awali, heroin ni painkiller, it kills both physical and emotional pain.

Watumiaji husema kwamba unajiskia kama katoto kalikofunikwa kwenye ‘baby shoo' au pamba, unasahau matatizo yako yote na kujiona kama Bill Gates. Hii ndio sababu kubwa kwanini watu wengi wanaotumia heroin ni wale wenye matatizo makubwa na uhaba mkubwa wa furaha kwenye maisha yao.

Kama unatumia heroin mara kwa mara kuna uwezekano mkubwa ukawa addicted au teja' kama wengi tunavyosema. Ukishakuwa teja inamaanisha utahitaji kutumia kila siku vinginevyo utakua physically ill kutokana na symptoms za kuwithdraw, na hii ndio inawafanya wengi washindwe kuacha, na pia ukizingatia kwamba watumiaji wengi hawana mengi ya kuwafanya wawe na furaha kwenye maisha yao zaidi ya kutumia huo unga.

Ukishajikuta kwenye hali hii, inakua ukiamka asubuhi unakuwa unahitaji kutumia na mawazo yako yote ni juu ya namna ambavyo utapata pesa ili uweze kununua ;unga' wa siku hiyo. Na inakuwa tabu sana kwa watumiaji sugu kwa kuwa wanahitaji kiwango kikubwa zaidi ili wapate steam, hii inamaanisha pesa zaidi na kwa kuwa wengi hawana ajira au means yoyote ya kipato, wanaishia kuingia kwenye uhalifu.

Heroin inaua kama mtumiaji atatumia kiwango kikuwa ambacho mwili wake hauwezi kukihandle, hii inaitwa Overdose na mara nyingi hutokea kama mtumiaji ata inject, na kuinject kuna ambatana na hatari za maambukizi ya magonjwa kama hep C, hep B na HIV kama watumiaji watashare sindano.

Utumiaji wa madawa ya kulevya umewasababishia watu wengi matatizo makubwa, wengine wamepoteza maisha yao kabisa, njia pekee na salama ya kuyaepuka yote haya ni simple- USITUMIE. Kama unatumia heroin, jitahidi usi inject- vuta tu, its safer na usisahau kuongea na wataalamu , kama wapo
 
Hahaahaaaa hapa kunadatishwa duh

Paku- watu wenye akili zao timamu watanishukuru kwa hiyo thread, I think its very infomative, ask me anything about drugs or substance misuse in general and I will answer you.
 
......................
Kwa wanaoanza kutumia heroin kwa mara ya kwanza husikia joto, hupata muwasho wa ngozi na kutapika kwa sana. Wengi husema inahitaji kutumia mara kadhaa kabla ya kuanza kuipenda na kunogewa. Kama nilivyosema hapo awali, heroin ni painkiller, it kills both physical and emotional pain. Watumiaji husema kwamba unajiskia kama katoto kalikofunikwa kwenye ‘baby shoo’ au pamba, unasahau matatizo yako yote na kujiona kama Bill Gates.Hii ndio sababu kubwa kwanini watu wengi wanaotumia heroin ni wale wenye matatizo makubwa na uhaba mkubwa wa furaha kwenye maisha yao.

Mkuu hivi ni kwa nini inakuwa vigumu kuacha kama mtu anapata side effect kama hizo hapo juu? Kwa jinsi mimi binafsi ninavyojiskia kitu chochote kitakachonifanya nitapike siwezi kukijaribu maishani, nashindwa kupata picha ni kwa nini hao watumiaji wanavumilia mateso hayo!!?

Many thanks lakini for the informative piece!
 
Mkuu hivi ni kwa nini inakuwa vigumu kuacha kama mtu anapata side effect kama hizo hapo juu? Kwa jinsi mimi binafsi ninavyojiskia kitu chochote kitakachonifanya nitapike siwezi kukijaribu maishani, nashindwa kupata picha ni kwa nini hao watumiaji wanavumilia mateso hayo!!?

Many thanks lakini for the informative piece!

Hilo joto, muwasho wa ngozi na kutapika hufutia baada ya steam kukatika, kinachowachanganya watumiaji na kuwafanya watumie zaidi ni ule wakati ambao steam inakuwa iko mahali pake, unaambiwa ni utamu wa ajabu!
 
Hilo joto, muwasho wa ngozi na kutapika hufutia baada ya steam kukatika, kinachowachanganya watumiaji na kuwafanya watumie zaidi ni ule wakati ambao steam inakuwa iko mahali pake, unaambiwa ni utamu wa ajabu!

ooohh I see...
Kwa hiyo hii ni kama hangover sio?

Ila duh....
 
Burudani ya ibilisi haishi utamu ... the more unapata the more you want more till you lose yourself
 
Burudani ya ibilisi haishi utamu ... the more unapata the more you want more till you lose yourself

... :D

kweli tupu!

...kilicho cha ibilisi na uharamu wake kinakuwa 'kitamuuuu', yaaaani ...we acha tu dada'angu!

...ndio maana (kwa wanaoamini) Adam na Eve waliushindwa 'mtihani'!
 
Paku- watu wenye akili zao timamu watanishukuru kwa hiyo thread, I think its very infomative, ask me anything about drugs or substance misuse in general and I will answer you.

Nilisikia kuwa Raha inayowafanya watu wavute madawa ni kama vile mtu akiwa anapata ORGASM ila hii inakuwa prolonged, ukiacha ila ya sekunde chache kwenye ngono, Hii ina ukweli gani Mkuu?
 
Nilisikia kuwa Raha inayowafanya watu wavute madawa ni kama vile mtu akiwa anapata ORGASM ila hii inakuwa prolonged, ukiacha ila ya sekunde chache kwenye ngono, Hii ina ukweli gani Mkuu?
Kama una maumivu makali yanapotea, kama ilikua na hofu inakutoka, husikii njaa, husikii baridi, unakuwa umerelax na kuwa na furaha hata kama umefiwa na ndugu wa karibu. Steam yenyewe inaweza kukaa hadi masaa 6 ikitegemea na dose yenyewe unayojipiga ndo maana watumiaji wengine wanaingia tamaa na kuishia kujioverdose.
 
nilitaka kujua,ni kwa nini walio watumiaji sugu wa heroin wakikosa kupata kwa siku mmoja huwa wanaharisha na baada ya kupata huwa wanakata kuharisha
N;B KUHARISHA HUKO HUWA HAKUZUHILIKI KWA DAWA YEYOTE MPAKA APATE HEROIN
 
nilitaka kujua,ni kwa nini walio watumiaji sugu wa heroin wakikosa kupata kwa siku mmoja huwa wanaharisha na baada ya kupata huwa wanakata kuharisha
N;B KUHARISHA HUKO HUWA HAKUZUHILIKI KWA DAWA YEYOTE MPAKA APATE HEROIN

Kiroboto sina sababu ya kisayansi ya kwanini wanaharisha lakini najua hiyo ni mojawapo ya withdrawal symptoms haswa kama mtumiaji sugu ataacha kutumia bila msaada wa wataalam, dalili nyingine mara nyingi huwa ni kutapika, maumivu ya misuli na mifupa, kukosa usingizi na mafua. Inashauriwa kwa watumiaji sugu kupata ushauri wa kitaalamu kabla hawajaamua kuacha kwa kuwa wanaweza kufa kabisa. Normally ushauri unaotolewa ni kupunguza dose taratibu, au kutumia substute ambazo zinakupa steam kama ya heroin, medhadone ndo very common kwa suala hili.
 
Nilisikia kuwa Raha inayowafanya watu wavute madawa ni kama vile mtu akiwa anapata ORGASM ila hii inakuwa prolonged, ukiacha ila ya sekunde chache kwenye ngono, Hii ina ukweli gani Mkuu?
Hio kitu na unga kipi zaidi? Athari za kuishi mijini hizo
 
Heroin, ambayo pia inajulikana pia kwa majina ya Brown, Smack and Skag kwa UK, ni dawa ambayo hutengenezwa kutoka kwenye mmea uitwao opium poppy. Hutumika kama kama dawa ya maumivu. Mitaani huuzwa kwenye vijipakti vidogo ikiwa katika hali ya ungaunga wa brauni.Watumiaji wa heroin huivuta kama sigara au bangi kwa kutumia pipes au yale makaratasi ya jikoni ya silver, wengine hujidunga kwa kutumia sindano. Wengi wanaovuta huapa kwamba hawatathubutu kujidunga lakini mara nyingi nao huingia kwenye mchezo wa sindano kwa kuwa ndio njia bomba zaidi kwa kupata steam ya chapchap na yenye kukupa thamani halisi ya fedha zako.

Kwa wanaoanza kutumia heroin kwa mara ya kwanza husikia joto, hupata muwasho wa ngozi na kutapika kwa sana. Wengi husema inahitaji kutumia mara kadhaa kabla ya kuanza kuipenda na kunogewa. Kama nilivyosema hapo awali, heroin ni painkiller, it kills both physical and emotional pain. Watumiaji husema kwamba unajiskia kama katoto kalikofunikwa kwenye ‘baby shoo' au pamba, unasahau matatizo yako yote na kujiona kama Bill Gates.Hii ndio sababu kubwa kwanini watu wengi wanaotumia heroin ni wale wenye matatizo makubwa na uhaba mkubwa wa furaha kwenye maisha yao.

Kama unatumia heroin mara kwa mara kuna uwezekano mkubwa ukawa addicted au ‘teja' kama wengi tunavyosema. Ukishakuwa teja inamaanisha utahitaji kutumia kila siku vinginevyo utakua physically ill kutokana na symptoms za kuwithdraw, na hii ndio inawafanya wengi washindwe kuacha, na pia ukizingatia kwamba watumiaji wengi hawana mengi ya kuwafanya wawe na furaha kwenye maisha yao zaidi ya kutumia huo unga. Ukishajikuta kwenye hali hii, inakua ukiamka asubuhi unakuwa unahitaji kutumia na mawazo yako yote ni juu ya namna ambavyo utapata pesa ili uweze kununua ‘unga' wa siku hiyo. Na inakuwa tabu sana kwa watumiaji sugu kwa kuwa wanahitaji kiwango kikubwa zaidi ili wapate steam, hii inamaanisha pesa zaidi na kwa kuwa wengi hawana ajira au means yoyote ya kipato, wanaishia kuingia kwenye uhalifu.

Heroin inaua kama mtumiaji atatumia kiwango kikuwa ambacho mwili wake hauwezi kukihandle, hii inaitwa Overdose na mara nyingi hutokea kama mtumiaji ata inject, na kuinject kuna ambatana na hatari za maambukizi ya magonjwa kama hep C, hep B na HIV kama watumiaji watashare sindano.

Utumiaji wa madawa ya kulevya umewasababishia watu wengi matatizo makubwa, wengine wamepoteza maisha yao kabisa, njia pekee na salama ya kuyaepuka yote haya ni simple- USITUMIE. Kama unatumia heroin, jitahidi usi inject- vuta tu, its safer na usisahau kuongea na wataalamu , kama wapo.
Kana,
Kwa kuongezea: matumizi ya heroin yanakupa raha ile inayopatikana unapofika katika kilele cha ngono.Tofauti yake ni kuwa ile raha ya kilele cha ngono ni in terms of seconds while kwenye heroin unapata zile hisia za kilele cha ngono in terms of minutes.
 
Hio kitu na unga kipi zaidi? Athari za kuishi mijini hizo
Naamini unaposema 'unga' unaanisha cocaine kama ambavyo wengi tumezoea kibongobongo kwa kuwa hiyo kitu inafanana na unga wa mahindi, lakini pia heroin iko kwenye form ya unga wa brown na inaweza kuwa smoked kama coke, ofcourse mtu akitaka ku inject ndo itabidi aichanganye na maji na kuichemsha kidogo kabla ya kujidunga.

Heroin ni depressants kwa maana kwamba inadepres central nervous system na kumpunguzia mtumiaji maumivu, woga na stress, yani mtumiaji anakuwa totally relaxed.

Cocaine inaangukia kwenye kundi la stimulants, inastimulate mood na kukupa ile hali ya excitement, unajiskia fresh na kutamani kupiga mayowe kwa furaha, wazungu wanasema unapata 'adrenaline rush'.
 
kuna mtu aliwahi kuniambia kuwa raha unayosikia muda ule umebwia ni sawa na ile ya kufikia wakati wa malovee,tofauti ni kuwa hiyo moja ni for some few seconds while ile ya unga ni ya
muda mreeeeefu,ndo sababu once you are in,inasumbua kuacha
 
Back
Top Bottom