Utamkaji wa majina ya Viongozi una athari kwa watamkaji?

Tila-lila2

JF-Expert Member
Oct 20, 2019
653
1,058
Nimekuwa nikifuatilia sana namna viongozi wanavyotamka majina ya Viongozi wa juu yao: Mfano anapotamkwa Rais wa sasa:

- Makonda - Rais wetu mpendwa, Dokta John Pombe Joseph Magufuli
- Polepole - Rais na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mheshimiwa Dkt John Pombe Joseph Magufuli
- Dkt. Mpango - Rais wa wananchi, Dokta John Pombe Magufuli
- Prof Kabudi - Rais Mpendwa Daktari, Jooohn Pombe Joseeph Maghufuli
- Protabas Katambi - Rais wangu, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
- Membe - Rais wangu Pombe John Magufuli
- Rostam - Rais Ndugu Magufuli
- Lissu - Rais Magufuliii
- Musiba - Rais wa wananchi, mpendwa, kiboko ya mafisadi John Joseph Pombe Magufuli
- Lugola - Rais .......
- N.K

Hivi utamkaji wa hivi una impact kwa mtamkaji?
 
Kwa awamu hii ya mpenda sifa kila kitu kina wezekana ,imagine anafananishwa na Yesu.Kiongozi anaempamba Boss wake kwa Sifa zisizo kuwa zake akikabidhiwa Madaraka unafikiri itakuwaje kwa wapinzani wa Boss wake !!?..
 
Nimekuwa nikifuatilia sana namna viongozi wanavyotamka majina ya Viongozi wa juu yao: Mfano anapotamkwa Rais wa sasa:

- Makonda - Rais wetu mpendwa, Dokta John Pombe Joseph Magufuli
- Polepole - Rais na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mheshimiwa Dkt John Pombe Joseph Magufuli
- Dkt. Mpango - Rais wa wananchi, Dokta John Pombe Magufuli
- Prof Kabudi - Rais Mpendwa Daktari, Jooohn Pombe Joseeph Maghufuli
- Protabas Katambi - Rais wangu, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
- Membe - Rais wangu Pombe John Magufuli
- Rostam - Rais Ndugu Magufuli
- Lissu - Rais Magufuliii
- Musiba - Rais wa wananchi, mpendwa, kiboko ya mafisadi John Joseph Pombe Magufuli
- Lugola - Rais .......
- N.K

Hivi utamkaji wa hivi una impact kwa mtamkaji?
Jiwe asaidiwe manake ameshikwa pabaya na watu flani. Kuchagua mpinzani pia ni kumsaidia jiwe manake hajitambui kwasasa.
 
Sifa ya kwanza ya kiongozi anayejipendekeza hua ni lazima ataje majina manne ya kuzaliwa ya boss wake.
Unanikumbusha yule mkurugenzi wa jiji la Arusha "unachezea mapato ya serikali ya John Pombe Joseph Magufuli..." yaani ni full kujipendekeza. Inashangaza sana. Kwani mtu akisema " ..unachezea mapato ya serikali.." si inajulikana tosha hapo!?
 
Unanikumbusha yule mkurugenzi wa jiji la Arusha "unachezea mapato ya serikali ya John Pombe Joseph Magufuli..." yaani ni full kujipendekeza. Inashangaza sana. Kwani mtu akisema " ..unachezea mapato ya serikali.." si inajulikana tosha hapo!?
Hahah Mkapa aliwahi kupiga mikwara siku 1 akasema hii ni serikali ya CCM sio ya mtu,lkn naona mikwara ile haikuwaingia kabisa mkuu.
 
Back
Top Bottom