Utalii kitaifa hauhitaji vivutio vingi na matangazo; unahitaji historia, siasa, muingiliano, biashara na miondombinu

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,581
46,178
Mataifa yanayofanya vizuri na kuongoza katika utalii duniani ni pamoja na; Ufaransa, Hispania, Marekani, China, Italia, Uturuki, Mexico, Ujerumani, Uingereza. Kwa Africa ni South Africa, Misri, Morocco, Algeria, Zimbabwe, Mozambique, Ivory Coast, Kenya na Botswana.

Ukiyatazama mataifa haya kwa undani utagundua kila moja lina yote au baadhi ya mambo yafuatayo:

1. Historia kubwa, za muda mrefu na maarufu duniani kote. Ukiizungumzia hispania ni taaifa lililohusika kwa kiasi kikubwa kuwafanya binadamu wafike sehemu nyingine za dunia, US ni taifa la kwanza katika Ulimwengu wa kisasa kuanzisha Demokrasia, Misri ina historia maarufu ya mafarao na Piramidi n.k

2. Siasa zenye ushawishi mkubwa kwa mataifa mengine. Hapo utaiona Marekani, China, Uingereza, Misri, n.k

3. Muingiliano mkubwa na wa muda mrefu na Mataifa mengine. Kuna mataifa ambayo yako wazi sana kutembelewa na raia kutoka nchi nyingine na kuna mataifa ambayo ni yaliyojifungia "wanapenda kufanya mambo yao kama kisiwa cha kipekee"

4. Biashara na uchumi wa soko hurua ni kigezo kikubwa katika kupata watu wengi wanaoitembelea nchi yako. Botswana ni mzalishaji namba moja wa Almasi Africa, Kenya imekuwa taifa la kibepari tangu kuanzishwa kwake.

5. Miondombinu bora. Watalii wanapenda watembelee maeneo yenye barabara nzuri za lami, hospitali bora, miji misafi n.k

Kama tunataka kuwa na sekta kubwa ya utalii kuliko wengine barani Africa tuzingatie hayo. Kuwa na vile "tunavyofikiri" ni vivutio vingi na kuvitangaza kwa nguvu sana ni tone dogo tu katika bahari ya utalii.
 
Uko sahihi, Simba wako sehemu nyingi duniani, milima mirefu, maziwa na mito mikubwa viko sehemu nyingi duniani, watalii hawaji tu kwa sababu unavyo hivyo, wanahitaji "experience", na experience wanasikiliza wengine wanakuzungumziaje.

Tanzania tunatangaza vivutio hatutangazi experience ya vivutio. Unakuta mtu anajinasibu mbele ya watu eti Tanzania tuna Simba wengi zaidi Africa halafu kamaliza. Ndio ni kweli lakini hakuna tofauti ya kuona Simba 100 na kuona Simba 1000.
 
Uko sahihi, Simba wako sehemu nyingi duniani, milima mirefu, maziwa na mito mikubwa viko sehemu nyingi duniani, watalii hawaji tu kwa sababu unavyo hivyo, wanahitaji "experience", na experience wanasikiliza wengine wanakuzungumziaje.
Kitu ambacho wanashindwa kujua nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara vivutio vyetu vingi vinafanana vimepishana majina tu. Ila Kenya ana almost everything ya kile ambacho tunacho, Zimbabwe ana hifadhi za kutosha, Mozambique wana beaches nzuri, South Africa ana landscapes nzuri pia.... Inchotakiwa ni kumuonyesha mgeni kwa nini aje kwako na atapata kipi cha tofauti
 
Algeria ina siasa gani kushinda Tanzania? Creativity inayofanywa kutangaza utalii wa Tanzania ni ya kipekee sio lazima guiga mataifa mengine yanavyotangaza utalii wao
 
Vivutio vya utalii vya Tanzania ni vya asili na vimekuwepo miaka lukuki, mengine yanabaki kuwa maigizo tu......
 
Watanzania mpoje? Kila kitu mnapinfa tu.
Yani Raisi kutangaza utalii we unaona haina tija, kwa hio bora asitangaze eti? Kuwaelewa watanzania kazi kweli.
Kila kitu kupinga.
 
Algeria ina siasa gani kushinda Tanzania? Creativity inayofanywa kutangaza utalii wa Tanzania ni ya kipekee sio lazima guiga mataifa mengine yanavyotangaza utalii wao
Algeria ni mojawapo ya mataifa yenye miondombinu bora barani Africa na pia ni taifa lenye historia ndefu sana inayohusisha Himaya za Roma ya kale, Ottoman. Ina miji mingi ya kihistoria iliyotunzwa vizuri.

Algeria ni mshirika mkuba wa Ulaya dhidi ya siasa za msimamo mkali na ugaidi katika katika ukanda wa Sahel. Hizo ni siasa za kimataifa zinazoiweka nchi hiyo katika ramani ya dunia.
 
Watanzania mpoje? Kila kitu mnapinfa tu.
Yani Raisi kutangaza utalii we unaona haina tija, kwa hio bora asitangaze eti? Kuwaelewa watanzania kazi kweli.
Kila kitu kupinga.
Hayo mataifa yanayoongoza kwa utalii hakuna hata moja Rais wake amehusika kutangaza hivyo unavyodhani ni vivutio vya utalii.Rudia kusoma uzi.
 
Hayo mataifa yanayoongoza kwa utalii hakuna hata moja Rais wake amehusika kutangaza hivyo unavyodhani ni vivutio vya utalii.Rudia kusoma uzi.
Lwani tukanza sisi kyna ubaya gani? .kwa hio ulitaka raisi wa hizo nchi atangaze na sie tuige ?
Kwani raisi ni mungu mpaka asitangaze rasilimali za nchi?
Hata mungu Yesu alikuwa anajitangaza kuna ubaya gani raisi wetu kutangaza utalii?
 
Back
Top Bottom