Utakiona cha mtema kuni!, Kama ni hadithi , ilikuwa kwenye kitabu gani? Mtunzi alikuwa nani...na mengineyo....

Sometimes tunatumia msemo: utakiona cha mtema kuni.
Msemo huu ulianzia wapi? Mtemakuni aliona nini?
 
ninavyojua huo msemo una asili ya Wasukuma/Wanyamwezi,,,,,,,,,na hilo neno Mtema linatokana na neno Mtemi, ,,,, na mana halisi ya neno hilo Mtemi ilikuwa ni Mkataji, mkata mashauri, mkata kesi kwa hivyo "utakiona cha mtema kuni" ina maana utakiona cha mkata kuni,,,,,,,,,,,,,,, swali lako nadhani bado halitakuwa limejibiwa sawasawa kwani hata mimi pia nina shauku ya kujua kilichompata mkata kuni
 
Sometimes tunatumia msemo: utakiona cha mtema kuni.
Msemo huu ulianzia wapi? Mtemakuni aliona nini?
Mtema kuni ndiye aliyeona kilichomng'oa kanga manyoya ya shingoni, alipokuwa msituni akikata kuni. Hadi leo mtema kuni hajisimulia ni nini haswa kilichotokea siku hiyo!
 
Hii methali inatokana na hadithi au simulizi ya mkata kuni (Mtema kuni... Hiki ni kiswahili cha zamani). Kwa ufupi inasimuliwa kwamba mkata kuni alikwenda porini kwa nia ya kutema kuni (kukata kuni) kutokana na sababu anazo zijuwa yeye au kwa kuzidiwa na mawazo alipofika porini akapitiwa na usingizi (kama bado nakumbuka vizuri) ndio kwanza ulikuwa muda wa Mawio yaani jua linachomoza).

Alipokurupuka... kuangaza huku na huku shoka halioni, na hali anakumbuka vizuri kulichukuwa...

Yeye hakahisi labda limedondoka mahali... akaanza kulitafuta kuanzia Mawio mpaka Machweo (Kuzama kwa jua Wakati wa Magharibi) Mwisowe akajikuta amechoka na shoka halionekani.

Akaamua kukaa chini ya mti ili apumzishe akili na kutafakari upya wapi alipolidondosha shoka lake. Wakati anajiandaa kukaa chini kuangalia begani kwake analiona shoka lake... kumbe alikuwa amesahau kuwa shoka lilikuwa amelining'iniza begani kwake...

Hapo ndipo palipo patikana huo msemo wa "Utakiona cha mtema kuni... Kutafuta shoka wakati lipo begani."

Hii kidogo inataka kufanana ule msemo wa "Utakiona kilicho vunja shoka mpini ukabaki... msemo huu umetokana na simulizi za Sir H. Rider Haggard kwenye moja ya simulizi zake zinazo elezea visa vya mwindaji Tembo hodari Bwana Allan Quatermain (Makumazan or Macumazahn)... Na msaidizi wake Msolopaganzi (Umslopogaas) na shoka lake Nkosi kazi (Inkosi-kaas)... Bwana Henry Curtis, na rafikie Kapiteni Good, (Bwana Mzuri).

Kwenye liwaya hii ndipo pia lilipo patikana jina Gagula... Kibibi kilichokuwa kichwawi (Kigagula)

Vitabu hivi ni miongoni mwa vitabu ambavyo vinaonyesha au kusimulia ujasiri wa hali ya juu sana... Pia kwenye ile riwaya ya Machimbo ya Mfalme Suleiman na nchi ya Wakukuana... Na vile vingine ambavyo havikuwahi kutafsiriwa kwa kiswahili kama vile SHE & Ayesha (Tibet)

Wale walio wahi kusoma watamkumbuka sana Bwana Msolopaganzi (Umslopogaas) na majigambo yake a.k.a Mikwara mizito aliyokuwa akiwatishia maadui zake...

Nakumbua mwisho wa riwaya Umsolopaganzi alipomaliza kazi ya kulinda ngazi kuu... Alikuwa amepata majeraha mengi mwilini... akajua kuwa mwisho wa uhai wake umekaribia ndipo alipoamua kufa na shoka lake (Bibi msemi).... alilizungusha shoka lake kiasi ya kuonekana kama mwali wa moto... kisha kwa pigo moja... pigo lililo takatifu... Pigo lililo nyooka... akalishusha shoka lake kwa kasi ya ajabu na kulipasuwa jiwe lile na huku shoka lake likitawanyika vipande vipande na kubakia akiwa ameshikilia mpini wa shoka ukiwa mzima.... Mzee wa kizuru akaanguka chini akakata roho...

Soma baadhi ya vipande toka Riwaya ya Allan Quatermain
...



Soma majigambo (Mikwara ya mzee wa Kizuru)

Ni thnread ya zamani kidogo ia umenifurahisha ulipo taja wahusika ktk hivyo vitabu.
 
Mzizi wa Mbuyu nimekupata mkuu ngoja nichangie kidogo; Mimi hili nilipata simulizi toka kwa jamaa mmoja wa Kenya ambae anasema kuna mwalimu aliwasimulia shule ya msingi juu ya kisa cha mtema kuni. Hiyo hadithi inasema hivi:


Siku moja jamaa mtema (mkata) kuni alienda porini kukata kuni. Sasa akakuta mti mkubwa umeanguka na umekauka vizuri, ambao wenyeji wanaupenda sana kwa kutumia kwa vile kuni zake hazitoi moshi n.k. Sasa huyo mtema kuni akaanza kukata kuni na kurundika mzigo mkubwa tu.


Jua lilipozidi kuwa kali jamaa akavua nguo akabaki uchi (hakutarajia mtu kutokea maeneo hayo kwa vile ni mbali na makazi ya watu) huku akiendelea na kupasua kuni toka kwenye lile gogo. Ikatokea jamaa akawa amechoka na pia jua kali, kwa hivyo akaamua kukaa juu ya lile gogo kupumzika.


Sasa lile gogo lilikuwa lina ufa (kutokana na kutanuka kwa jua kali), kwa hivyo nyanya zikawa zimening'inia kwenye huo ufa. Baada ya kitambo kirefu kupita, jua nalo likawa linazama; kwa hivyo jamaa akaamua kunyanyuka ili ajitayarishe kuondoka. Sasa kumbe lile gogo lilikuwa limeshaanza ku-contract (kusinyaa); kwa hiyo nyanya zikashindwa kutoka.


Jamaa wakati anakukuruka, huku contraction ya gogo inaendelea taratibu; jamaa akajikuta immediate options zimekauka kwa vile hakuweza kujinasua na shoka lilikuwa mbali hivyo hawezi kuzikata nyanya ili atoke. So, jamaa ndio akafia pale juu ya gogo baada ya mateso ya muda mrefu, kwani hata kelele alizopiga hazikuweza kusikika kijijini ambako palikuwa mbali. Kwa hivyo, ndugu, jamaa na marafiki walipomtafuta ndio wakamkuta jamaa amejifia juu ya gogo na nyanya zimenasa ndani ya gogo....! Kwa hivyo ikaonekana ni mateso makubwa mno mtu anayoweza kuyapata, so watu wakawa wanafanya reference kwamba ukifanya jambo baya/ukaidi n.k then utakiona cha mtema kuni


Poa mkuu nipe thanks....
Mmmmhhh... Hii ni kweli?
 
Last edited by a moderator:
Duh kweli kusoma kwingi ni kujua mengi,hili neno ukweli nalitumia sana lkn sijui ht sababu wala maana ila nashkuru nimepata maana ht ya mtema kuni,ikiwa na maana ya mkata kuni,big up wana jf
 
ninavyojua huo msemo una asili ya Wasukuma/Wanyamwezi,,,,,,,,,na hilo neno Mtema linatokana na neno Mtemi, ,,,, na mana halisi ya neno hilo Mtemi ilikuwa ni Mkataji, mkata mashauri, mkata kesi kwa hivyo "utakiona cha mtema kuni" ina maana utakiona cha mkata kuni,,,,,,,,,,,,,,, swali lako nadhani bado halitakuwa limejibiwa sawasawa kwani hata mimi pia nina shauku ya kujua kilichompata mkata kuni
Sasa nimegundua kuwa yooote hayo majitabu kutoka ughaibuni ni facade ,ukweli watu wana hamu ya hadthi na visa vyetu asilia!swali tunaanzia wapi kukata kiu hii?
 
Habri za asubuhi wadau!?

Naomba kuelewa chanzo hasa cha hiyo kauli "... cha mtema kuni". Je hiyo ilikuwa ni hekaya au nini hasa?

Na kama ni hekaya kama zilivyo za Abu nuwasi, je Kitabu chake kinaetwaje ili nijue ni nini hasa kilimpata huyu mtema kuni hadi leo huwa tunatishwa kukiona alichokiona mtema kuni.
 
Mtema kuni ni mkata kuni. Inahadithiwa kuwa kulikuwa na mtu mmoja aliyekwenda kukata kuni msituni. Wakati wa kukata,alijeruhiwa na kipande cha mti aliokuwa akiukata vibaya sana. Ikasemwa kuwa,kuni zimemrudi mkataji. Yaani,kuni zimelipa kisasi kwa kuwaka hasira.

Asante Petro kwa kunipa mwanga kidogo...
Nadhani hizi ni moja ya hadithi zetu za kiafrica ambazo nyingi hazijawa documented popote na matokeo yake zimeshakufa na kusahaulika!
 
Last edited by a moderator:
Mtema kuni ni mkata kuni. Inahadithiwa kuwa kulikuwa na mtu mmoja aliyekwenda kukata kuni msituni. Wakati wa kukata,alijeruhiwa na kipande cha mti aliokuwa akiukata vibaya sana. Ikasemwa kuwa,kuni zimemrudi mkataji. Yaani,kuni zimelipa kisasi kwa kuwaka hasira.
Hapo unachanganya mambo kidogo. Msemo mzima ni: utakiona cha mtema kuni kilichomng'oa kanga manyoya ya shingoni.

​Suala zima hapo ni nini haswa kilichomng'oa kanga manyoya ya shingoni? Hicho ndio alichokiona mtema kuni alipokua anakata kuni huko msituni!
 
Back
Top Bottom