Utakiona cha mtema kuni!, Kama ni hadithi , ilikuwa kwenye kitabu gani? Mtunzi alikuwa nani...na mengineyo....

Mzizi wa Mbuyu

JF-Expert Member
May 15, 2009
7,320
6,806
Nimekuwa nalitumia, kusikia sana msemo huu "CHAMTEMA KUNI" kwa muda mrefu sasa katika maisha yangu ya kila siku. Najua kuna maneno yanatumika kwa maana hiyo hiyo kama vile; kilichomtoa kanga manyoya ya shingo, kijinga cha moto, kilicho mfanya chura ashinde mtoni n.k haya maelezo yake yako wazi.

Ila ukweli ndugu zanguni nimejaribu kuulizia chanzo cha matumizi ya neno hili, nimeishawahi kusikia kuwa ni msemo wa wahenga tu..., wengine wanasema ni hadithi ya kimapokeo, wengine wanasema ni hadithi ya kwenye kitabu. Lakinipamoja na yoote hayo sina uhakia hasa nini chanzo cha neno.
Please, naomba ufafanuzi, kwa yeyote anaejua msemo huu "CHAMTEMA KUNI" ulitokana na nini. Cha mtema kuni! kipi! kiatu?, kisa?! ,kiuno?! nk kilifanya nini hadi kiogopwe namna hii??!!

Kama ni hadithi , ilikuwa kwenye kitabu gani? Mtunzi alikuwa nani...na mengineyo....

Maoni ya watu mbalimbali kutokana na swali hili...

X-PASTER said:
Hii methali inatokana na hadithi au simulizi ya mkata kuni (Mtema kuni... Hiki ni kiswahili cha zamani). Kwa ufupi inasimuliwa kwamba mkata kuni alikwenda porini kwa nia ya kutema kuni (kukata kuni) kutokana na sababu anazo zijuwa yeye au kwa kuzidiwa na mawazo alipofika porini akapitiwa na usingizi (kama bado nakumbuka vizuri) ndio kwanza ulikuwa muda wa Mawio yaani jua linachomoza).

Alipokurupuka... kuangaza huku na huku shoka halioni, na hali anakumbuka vizuri kulichukuwa...

Yeye hakahisi labda limedondoka mahali... akaanza kulitafuta kuanzia Mawio mpaka Machweo (Kuzama kwa jua Wakati wa Magharibi) Mwisowe akajikuta amechoka na shoka halionekani.

Akaamua kukaa chini ya mti ili apumzishe akili na kutafakari upya wapi alipolidondosha shoka lake. Wakati anajiandaa kukaa chini kuangalia begani kwake analiona shoka lake... kumbe alikuwa amesahau kuwa shoka lilikuwa amelining'iniza begani kwake...

Hapo ndipo palipo patikana huo msemo wa "Utakiona cha mtema kuni... Kutafuta shoka wakati lipo begani."

Hii kidogo inataka kufanana ule msemo wa "Utakiona kilicho vunja shoka mpini ukabaki... msemo huu umetokana na simulizi za Sir H. Rider Haggard kwenye moja ya simulizi zake zinazo elezea visa vya mwindaji Tembo hodari Bwana Allan Quatermain (Makumazan or Macumazahn)... Na msaidizi wake Msolopaganzi (Umslopogaas) na shoka lake Nkosi kazi (Inkosi-kaas)... Bwana Henry Curtis, na rafikie Kapiteni Good, (Bwana Mzuri).

Kwenye liwaya hii ndipo pia lilipo patikana jina Gagula... Kibibi kilichokuwa kichwawi (Kigagula)

Vitabu hivi ni miongoni mwa vitabu ambavyo vinaonyesha au kusimulia ujasiri wa hali ya juu sana... Pia kwenye ile riwaya ya Machimbo ya Mfalme Suleiman na nchi ya Wakukuana... Na vile vingine ambavyo havikuwahi kutafsiriwa kwa kiswahili kama vile SHE & Ayesha (Tibet)

Wale walio wahi kusoma watamkumbuka sana Bwana Msolopaganzi (Umslopogaas) na majigambo yake a.k.a Mikwara mizito aliyokuwa akiwatishia maadui zake...

Nakumbua mwisho wa riwaya Umsolopaganzi alipomaliza kazi ya kulinda ngazi kuu... Alikuwa amepata majeraha mengi mwilini... akajua kuwa mwisho wa uhai wake umekaribia ndipo alipoamua kufa na shoka lake (Bibi msemi).... alilizungusha shoka lake kiasi ya kuonekana kama mwali wa moto... kisha kwa pigo moja... pigo lililo takatifu... Pigo lililo nyooka... akalishusha shoka lake kwa kasi ya ajabu na kulipasuwa jiwe lile na huku shoka lake likitawanyika vipande vipande na kubakia akiwa ameshikilia mpini wa shoka ukiwa mzima.... Mzee wa kizuru akaanguka chini akakata roho...

Soma baadhi ya vipande toka Riwaya ya Allan Quatermain...

Umslopogaas... Straight up the hall he went, leaving
behind him a track of blood on the marble pavement, till at last
he reached the sacred stone, which stood in the centre of it,
and here his strength seemed to fail him, for he stopped and
leaned upon his axe. Then suddenly he lifted up his voice and
cried aloud...

'I die, I die... but it was a kingly fray. Where are they who
came up the great stair? I see them not. Art thou there, Macumazahn,
or art thou gone before to wait for me in the dark whither I
go? The blood blinds me... the place turns round... I hear the
voice of waters.'

Next, as though a new thought had struck him, he lifted the red
axe and kissed the blade.

'Farewell, Inkosi-kaas,' he cried. 'Nay, nay, we will go together;
we cannot part, thou and I. We have lived too long one with
another, thou and I.

'One more stroke, only one! A good stroke! a straight stroke!
a strong stroke!' and, drawing himself to his full height, with
a wild heart-shaking shout, he with both hands began to whirl
the axe round his head till it looked like a circle of flaming steel.
Then, suddenly, with awful force he brought it down straight
on to the crown of the mass of sacred stone. A shower of sparks
flew up, and such was the almost superhuman strength of the blow,
that the massive marble split with a rending sound into a score
of pieces, whilst of Inkosi-kaas there remained but some fragments
of steel and a fibrous rope of shattered horn that had been the
handle. Down with a crash on to the pavement fell the fragments
of the holy stone, and down with a crash on to them, still grasping
the knob of Inkosi-kaas, fell the brave old Zulu... dead.

And thus the hero died.

A gasp of wonder and astonishment rose from all those who witnessed
the extraordinary sight, and then somebody cried, '_The prophecy!
the prophecy!_ He has shattered the sacred stone!' and at once
a murmuring arose .

Soma majigambo (Mikwara ya mzee wa Kizuru)
'...Ah, Macumazahn,' he said, 'I suppose it is because I am getting
old, but I don't think that I shall ever learn to understand
the ways of you white people. Look there now, I pray thee, they
are a pretty pair of doves, but what is all the fuss about, Macumazahn?
He wants a wife, and she wants a husband, then why does he not
pay his cows down... like a man and have done with
it? It would save a deal of trouble, and we should have had
our night's sleep. But there they go, talk, talk, talk, and
kiss, kiss, kiss, like mad things. Eugh!'

'Thou shalt stand against me man to man, be not afraid,' replied
Umslopogaas, still in the same ominous voice. 'Thou shalt stand
face to face with Umslopogaas, of the blood of Chaka, of the
people of the Amazulu, a captain in the regiment of the Nkomabakosi,
as many have done before, and bow thyself to Inkosi-kaas, as
many have done before. Ay, laugh on, laugh on! tomorrow night
shall the jackals laugh as they crunch thy ribs.'

'What, comest thou too?' laughed out the old warrior. 'Welcome
....a welcome to thee, brave heart! Ow! for the man who can die
like a man; ow! for the death grip and the ringing of steel.
Ow! we are ready. We wet our beaks like eagles, our spears
flash in the sun; we shake our assegais, and are hungry to fight.
Who comes to give greeting to the Chieftainess (Inkosi-kaas)?
Who would taste her kiss, whereof the fruit is death? I, the
Woodpecker, I, the Slaughterer, I the Swiftfooted! I, Umslopogaas,
of the tribe of the Maquilisini, of the people of Amazulu, a
captain of the regiment of the Nkomabakosi: I, Umslopogaas, the
son of Indabazimbi, the son of Arpi the son of Mosilikaatze,
I of the royal blood of T'Chaka, I of the King's House, I the
Ringed Man, I the Induna, I call to them as a buck calls, I challenge
them, I await them. Ow! it is thou, it is thou!'
 
Lugha ninayojua ni "akifanya hivyo atakiona cha mtemakuni". Ninaelewa ni kama tishio au onyo: akifanya kitu kisicho halali ataona matokeo yake yaani atapata adhabu.

Mtemakuni (pia: mtema-kuni au mtema kuni) ni mtu anayepasua miti kuwa kuni. Kwa hiyo ana kazi nzitonzito pia ni watu wenye nguvu ya kimwili. Maana neno "kutema" hupatikana kwa maana mawili moja ni "kutema mate" mengine ni "kupasua kitu" kama ubao, miwa n.k.

Sina uhakika juu ya asili ya usemi lakini nimeielewa hivyo:

Hawa watemakuni ni watu wenye nguvu wanajua kuadhibu. Ukitaka kuiba kwao utaona jinsi gani wanavyoweza kujitetea. -
au labda pia: Watemakuni ni watu wanaoishi katika mazingira magumu msituni wakifanya kazi hii nzito heri usijaribu kucheza nao...

Sijui wenzangu wanaonaje?
 
Nashukuru sana ndugu yangu, si haba, iatabidi niende BAKITA pia kujiridhisha.
Hapa inaoneka wengi wetu huwa tuna tumia misemo tusiyojua asili yake!
 
BAKITA unataka kuuliza namna gani? Je wanao ukurasa mtandaoni unapoandika maswali?
 
BAKITA unataka kuuliza namna gani? Je wanao ukurasa mtandaoni unapoandika maswali?

Ntakwenda mzimamzima ofisini kwao, ninashida sana na hii kitu ndugu yangu nina kazi nayo. Sidhani kama watakosa ufafanuzi juu ya msemo huu. Kama unakingine cha kunisaidia, sema ndugu yangu.
 
Mzizi wa Mbuyu nimekupata mkuu ngoja nichangie kidogo; Mimi hili nilipata simulizi toka kwa jamaa mmoja wa Kenya ambae anasema kuna mwalimu aliwasimulia shule ya msingi juu ya kisa cha mtema kuni. Hiyo hadithi inasema hivi:

Siku moja jamaa mtema (mkata) kuni alienda porini kukata kuni. Sasa akakuta mti mkubwa umeanguka na umekauka vizuri, ambao wenyeji wanaupenda sana kwa kutumia kwa vile kuni zake hazitoi moshi n.k. Sasa huyo mtema kuni akaanza kukata kuni na kurundika mzigo mkubwa tu.

Jua lilipozidi kuwa kali jamaa akavua nguo akabaki uchi (hakutarajia mtu kutokea maeneo hayo kwa vile ni mbali na makazi ya watu) huku akiendelea na kupasua kuni toka kwenye lile gogo. Ikatokea jamaa akawa amechoka na pia jua kali, kwa hivyo akaamua kukaa juu ya lile gogo kupumzika.

Sasa lile gogo lilikuwa lina ufa (kutokana na kutanuka kwa jua kali), kwa hivyo nyanya zikawa zimening'inia kwenye huo ufa. Baada ya kitambo kirefu kupita, jua nalo likawa linazama; kwa hivyo jamaa akaamua kunyanyuka ili ajitayarishe kuondoka. Sasa kumbe lile gogo lilikuwa limeshaanza ku-contract (kusinyaa); kwa hiyo nyanya zikashindwa kutoka.

Jamaa wakati anakukuruka, huku contraction ya gogo inaendelea taratibu; jamaa akajikuta immediate options zimekauka kwa vile hakuweza kujinasua na shoka lilikuwa mbali hivyo hawezi kuzikata nyanya ili atoke. So, jamaa ndio akafia pale juu ya gogo baada ya mateso ya muda mrefu, kwani hata kelele alizopiga hazikuweza kusikika kijijini ambako palikuwa mbali. Kwa hivyo, ndugu, jamaa na marafiki walipomtafuta ndio wakamkuta jamaa amejifia juu ya gogo na nyanya zimenasa ndani ya gogo....! Kwa hivyo ikaonekana ni mateso makubwa mno mtu anayoweza kuyapata, so watu wakawa wanafanya reference kwamba ukifanya jambo baya/ukaidi n.k then utakiona cha mtema kuni

Poa mkuu nipe thanks....
 
Last edited:
Mtemakuni hakika ni mpasuaji au mkataji wa kuni kama wengine walivyosema. Hadithi ya mkatakuni wengine wanasema wakati akikata kuni alikosea mahesabu (umakini)shoka likatua kwenye mguu likampasua na kumjeruhi sana. Kwa hiyo, kukiona cha mtemakuni ina maana ya kujiingiza kwenye shida ya kujitakia, ni kukosa umakini katika kutenda jambo ambapo baadaye mtu anakuja kujuta kutokana na shida atakayoipata. Kumbe, ni msemo wa onyo, wa kumtaka mtu awe mwangalifu ili mabaya yasimkute. Ni msemo unaotaka seriousness ya mtu katika kutenda ili kujiepusha na matokeo mabaya.
 
Mzizi wa Mbuyu nimekupata mkuu ngoja nichangie kidogo; Mimi hili nilipata simulizi toka kwa jamaa mmoja wa Kenya ambae anasema kuna mwalimu aliwasimulia shule ya msingi juu ya kisa cha mtema kuni. Hiyo hadithi inasema hivi:


Siku moja jamaa mtema (mkata) kuni alienda porini kukata kuni. Sasa akakuta mti mkubwa umeanguka na umekauka vizuri, ambao wenyeji wanaupenda sana kwa kutumia kwa vile kuni zake hazitoi moshi n.k. Sasa huyo mtema kuni akaanza kukata kuni na kurundika mzigo mkubwa tu.


Jua lilipozidi kuwa kali jamaa akavua nguo akabaki uchi (hakutarajia mtu kutokea maeneo hayo kwa vile ni mbali na makazi ya watu) huku akiendelea na kupasua kuni toka kwenye lile gogo. Ikatokea jamaa akawa amechoka na pia jua kali, kwa hivyo akaamua kukaa juu ya lile gogo kupumzika.


Sasa lile gogo lilikuwa lina ufa (kutokana na kutanuka kwa jua kali), kwa hivyo nyanya zikawa zimening'inia kwenye huo ufa. Baada ya kitambo kirefu kupita, jua nalo likawa linazama; kwa hivyo jamaa akaamua kunyanyuka ili ajitayarishe kuondoka. Sasa kumbe lile gogo lilikuwa limeshaanza ku-contract (kusinyaa); kwa hiyo nyanya zikashindwa kutoka.


Jamaa wakati anakukuruka, huku contraction ya gogo inaendelea taratibu; jamaa akajikuta immediate options zimekauka kwa vile hakuweza kujinasua na shoka lilikuwa mbali hivyo hawezi kuzikata nyanya ili atoke. So, jamaa ndio akafia pale juu ya gogo baada ya mateso ya muda mrefu, kwani hata kelele alizopiga hazikuweza kusikika kijijini ambako palikuwa mbali. Kwa hivyo, ndugu, jamaa na marafiki walipomtafuta ndio wakamkuta jamaa amejifia juu ya gogo na nyanya zimenasa ndani ya gogo....! Kwa hivyo ikaonekana ni mateso makubwa mno mtu anayoweza kuyapata, so watu wakawa wanafanya reference kwamba ukifanya jambo baya/ukaidi n.k then utakiona cha mtema kuni


Poa mkuu nipe thanks....

Mkuu, thanks umepata ila duh! kama ni kweli ilikuwa hivyo, mtema kuni aliteseka sanaa!! Yaani nanihii.. yake ilibanwa kwenye gogo!!
Poa, lakini kweli pia ntakwenda BAKITA, nikipata muda kuchunguza jambo hili.
 
Mi huwa nafahamu simulizi tofauti kuhusu ''kukiona cha mtemakuni'', sikuwahi kusikia pia hizo zilipoelezwa hapo juu.
Niliambiwa kuwa mtema kuni ni mtu anaekata kuni na alieenda kukata kuni porini na alipokuwa anataka kuzifunga kuni pamoja akawa anatafuta kamba, na bila kujua akamgusa nyoka akidhani ni kamba ili afungie kuni, loooo! kilichofuata ni mapambano... kwa hiyo hicho ndo kilikuwa ''cha mtemakuni'' nilichokifahamu.
It is so intresting kuwa kuna simulizi tofauti tofauti kuhusiana na msemo uleule. Na nafikiri mambo kama haya yangehifadhiwa vizuri (yangekuwa well documented) ingesaidia kwa vizazi vijavyo hasa ukizingatia kiswahili kinakua sana sasa hivi ktk nch nyingi za Afrika.
 
Hii methali inatokana na hadithi au simulizi ya mkata kuni (Mtema kuni... Hiki ni kiswahili cha zamani). Kwa ufupi inasimuliwa kwamba mkata kuni alikwenda porini kwa nia ya kutema kuni (kukata kuni) kutokana na sababu anazo zijuwa yeye au kwa kuzidiwa na mawazo alipofika porini akapitiwa na usingizi (kama bado nakumbuka vizuri) ndio kwanza ulikuwa muda wa Mawio yaani jua linachomoza).

Alipokurupuka... kuangaza huku na huku shoka halioni, na hali anakumbuka vizuri kulichukuwa...

Yeye hakahisi labda limedondoka mahali... akaanza kulitafuta kuanzia Mawio mpaka Machweo (Kuzama kwa jua Wakati wa Magharibi) Mwisowe akajikuta amechoka na shoka halionekani.

Akaamua kukaa chini ya mti ili apumzishe akili na kutafakari upya wapi alipolidondosha shoka lake. Wakati anajiandaa kukaa chini kuangalia begani kwake analiona shoka lake... kumbe alikuwa amesahau kuwa shoka lilikuwa amelining'iniza begani kwake...

Hapo ndipo palipo patikana huo msemo wa "Utakiona cha mtema kuni... Kutafuta shoka wakati lipo begani."

Hii kidogo inataka kufanana ule msemo wa "Utakiona kilicho vunja shoka mpini ukabaki... msemo huu umetokana na simulizi za Sir H. Rider Haggard kwenye moja ya simulizi zake zinazo elezea visa vya mwindaji Tembo hodari Bwana Allan Quatermain (Makumazan or Macumazahn)... Na msaidizi wake Msolopaganzi (Umslopogaas) na shoka lake Nkosi kazi (Inkosi-kaas)... Bwana Henry Curtis, na rafikie Kapiteni Good, (Bwana Mzuri).

Kwenye liwaya hii ndipo pia lilipo patikana jina Gagula... Kibibi kilichokuwa kichwawi (Kigagula)

Vitabu hivi ni miongoni mwa vitabu ambavyo vinaonyesha au kusimulia ujasiri wa hali ya juu sana... Pia kwenye ile riwaya ya Machimbo ya Mfalme Suleiman na nchi ya Wakukuana... Na vile vingine ambavyo havikuwahi kutafsiriwa kwa kiswahili kama vile SHE & Ayesha (Tibet)

Wale walio wahi kusoma watamkumbuka sana Bwana Msolopaganzi (Umslopogaas) na majigambo yake a.k.a Mikwara mizito aliyokuwa akiwatishia maadui zake...

Nakumbua mwisho wa riwaya Umsolopaganzi alipomaliza kazi ya kulinda ngazi kuu... Alikuwa amepata majeraha mengi mwilini... akajua kuwa mwisho wa uhai wake umekaribia ndipo alipoamua kufa na shoka lake (Bibi msemi).... alilizungusha shoka lake kiasi ya kuonekana kama mwali wa moto... kisha kwa pigo moja... pigo lililo takatifu... Pigo lililo nyooka... akalishusha shoka lake kwa kasi ya ajabu na kulipasuwa jiwe lile na huku shoka lake likitawanyika vipande vipande na kubakia akiwa ameshikilia mpini wa shoka ukiwa mzima.... Mzee wa kizuru akaanguka chini akakata roho...

Soma baadhi ya vipande toka Riwaya ya Allan Quatermain...

Umslopogaas... Straight up the hall he went, leaving
behind him a track of blood on the marble pavement, till at last
he reached the sacred stone, which stood in the centre of it,
and here his strength seemed to fail him, for he stopped and
leaned upon his axe. Then suddenly he lifted up his voice and
cried aloud...

'I die, I die... but it was a kingly fray. Where are they who
came up the great stair? I see them not. Art thou there, Macumazahn,
or art thou gone before to wait for me in the dark whither I
go? The blood blinds me... the place turns round... I hear the
voice of waters.'

Next, as though a new thought had struck him, he lifted the red
axe and kissed the blade.

'Farewell, Inkosi-kaas,' he cried. 'Nay, nay, we will go together;
we cannot part, thou and I. We have lived too long one with
another, thou and I.

'One more stroke, only one! A good stroke! a straight stroke!
a strong stroke!' and, drawing himself to his full height, with
a wild heart-shaking shout, he with both hands began to whirl
the axe round his head till it looked like a circle of flaming steel.
Then, suddenly, with awful force he brought it down straight
on to the crown of the mass of sacred stone. A shower of sparks
flew up, and such was the almost superhuman strength of the blow,
that the massive marble split with a rending sound into a score
of pieces, whilst of Inkosi-kaas there remained but some fragments
of steel and a fibrous rope of shattered horn that had been the
handle. Down with a crash on to the pavement fell the fragments
of the holy stone, and down with a crash on to them, still grasping
the knob of Inkosi-kaas, fell the brave old Zulu... dead.

And thus the hero died.

A gasp of wonder and astonishment rose from all those who witnessed
the extraordinary sight, and then somebody cried, '_The prophecy!
the prophecy!_ He has shattered the sacred stone!' and at once
a murmuring arose .

Soma majigambo (Mikwara ya mzee wa Kizuru)
'...Ah, Macumazahn,' he said, 'I suppose it is because I am getting
old, but I don't think that I shall ever learn to understand
the ways of you white people. Look there now, I pray thee, they
are a pretty pair of doves, but what is all the fuss about, Macumazahn?
He wants a wife, and she wants a husband, then why does he not
pay his cows down... like a man and have done with
it? It would save a deal of trouble, and we should have had
our night's sleep. But there they go, talk, talk, talk, and
kiss, kiss, kiss, like mad things. Eugh!'

'Thou shalt stand against me man to man, be not afraid,' replied
Umslopogaas, still in the same ominous voice. 'Thou shalt stand
face to face with Umslopogaas, of the blood of Chaka, of the
people of the Amazulu, a captain in the regiment of the Nkomabakosi,
as many have done before, and bow thyself to Inkosi-kaas, as
many have done before. Ay, laugh on, laugh on! tomorrow night
shall the jackals laugh as they crunch thy ribs.'

'What, comest thou too?' laughed out the old warrior. 'Welcome
....a welcome to thee, brave heart! Ow! for the man who can die
like a man; ow! for the death grip and the ringing of steel.
Ow! we are ready. We wet our beaks like eagles, our spears
flash in the sun; we shake our assegais, and are hungry to fight.
Who comes to give greeting to the Chieftainess (Inkosi-kaas)?
Who would taste her kiss, whereof the fruit is death? I, the
Woodpecker, I, the Slaughterer, I the Swiftfooted! I, Umslopogaas,
of the tribe of the Maquilisini, of the people of Amazulu, a
captain of the regiment of the Nkomabakosi: I, Umslopogaas, the
son of Indabazimbi, the son of Arpi the son of Mosilikaatze,
I of the royal blood of T'Chaka, I of the King's House, I the
Ringed Man, I the Induna, I call to them as a buck calls, I challenge
them, I await them. Ow! it is thou, it is thou!'
 
Tangu nikiwa shuleni nimekua nikiusikia huu usemi,hivi ni nini hasa mtema kuni alikiona mpaka iwe hivyo..
 
Happy Valentine wana jf. Naomba kujua kisa kilichompata "Mtema Kuni" hadi huu msemo kuwa maarufu, hasa pale mtu anapoonywa asitende jambo fulani.
 
Kutema ni kukata kwa kibantu
kuni hapa jiongeze, kuni kuu ulimwenguni

zamani wanamme ndo walihesabiwa peke yao. Sasa Mzee X aliiba mke wa mfalme. Akatemwa kuni.
 
Kutema ni kukata kwa kibantu
kuni hapa jiongeze, kuni kuu ulimwenguni

zamani wanamme ndo walihesabiwa peke yao. Sasa Mzee X aliiba mke wa mfalme. Akatemwa kuni.

Asante kwa kunielewesha Kongosho, japo sijakupata vizuri hebu fafanua tena kwa lugha "rahisi"
 
Nilivamia hii Thread , nikidhani unaulizia "Ukuni" ! Kumbe "Mtema kuni"
Hii siifahamu, niwaachie watu wa Mrima, naimani watakutosheleza.
 
huyu mzee ukuni ulikatwa akabaki mwanamme shati.
Haku-qualify hata kuwa mwanamme suruali.

Ndo maana ukionywa halafu husikii wanakuambia utakiona cha mtema kuni. Huyu mzee alionywa ila hakusikia.

Nachoka kuandika kirefu.

Asante kwa kunielewesha Kongosho, japo sijakupata vizuri hebu fafanua tena kwa lugha "rahisi"
 
kaka mara zote nikiona nyuzi zako nashawishika kuzisoma
na mara zote nakosa chakuchangia ktk nyuzi zako...
duh!
ila kwa hili niliwahi kuckia japo akili imefuta, kuwa Mtema kuni ina maana ya mkata kuni. ...
Moja ya simulizi za Mtema kuni nilizosimuliwa utotoni ni pale aliporudi nyumbani bila kuni
lakini na jeraha la kuchomwa na mwiba mkali. .... and blah blah blah
 
huyu mzee ukuni ulikatwa akabaki mwanamme shati.
Haku-qualify hata kuwa mwanamme suruali.

Ndo maana ukionywa halafu husikii wanakuambia utakiona cha mtema kuni. Huyu mzee alionywa ila hakusikia.

Nachoka kuandika kirefu.

nimekupata sasa Kongosho, lakini mbona hawasemi "ukuni" bali wanasema kuni?
 
kaka mara zote nikiona nyuzi zako nashawishika kuzisoma
na mara zote nakosa chakuchangia ktk nyuzi zako...
duh!
ila kwa hili niliwahi kuckia japo akili imefuta, kuwa Mtema kuni ina maana ya mkata kuni. ...
Moja ya simulizi za Mtema kuni nilizosimuliwa utotoni ni pale aliporudi nyumbani bila kuni
lakini na jeraha la kuchomwa na mwiba mkali. .... and blah blah blah

Kwa nini huwa unakosa cha kuchangia?? Asante kwa mchango wako.
 
Back
Top Bottom