Utajuaje umefanya maamuzi magumu?

madeinmusoma

JF-Expert Member
Jan 7, 2014
322
386
1. Unatoa mimba halafu unalala na midoli kitandani..
- Ni maamuzi magumu.

2. Huna hata kitanda na unaamua kuoa -
-Hayo pia ni maamuzi magumu.

3. Huna uwezo wa kumlisha mkeo kazi yako ni kumjaza ujauzito -
-Ni maamuzi magumu.

4. Shule haina waalimu unampeleka mwanao -
- Pia ni maamuzi magumu....

5. Daladala imejaa mpaka mlangoni na unaamua kupanda
-Ni maamuzi magumu.

6. Unalipwa laki mbili unamhonga binti laki moja -
- Hayo ni maamuzi magumu.

7. Kama utasoma hapa na kushindwa kuweka maamuzi magumu unayoyajua -
-Utakuwa unamaamuzi magumu mnoo...!

8. Mdada unavaa nguo ya laki saba mshahara laki tu-
-Hayo ni maamuzi magumu

9.Binti unamwacha kijana mwenzio wa rika moja unaamua kuolewa na babu umri kama wa baba yako -
-hayo ni maamuzi magumu

10.Unapanga nyumba ya milioni saba kwa mwaka huku mshahara ni laki tano kwa mwezi -
-Hayo nayo ni maamuzi magumu

11.Unamfumania mkeo au mkeo anakuzalia watoto wanne nje ya ndoa na bado unaendelea kumwamini-
-Hayo nayo ni maamuzi magumu kupitiliza

12. Unamuadi mtu utamchangia ela katika sendoff au harusi yake wakati unajua hata kuwalipia Ada ya shule kuwalipia watoto Hakuna. hayo ni maamuzi magumu sana

13. Unambembeleza mwanamke kuwa unataka kumuoa na unajua kwamba unataka tu kumchezea na kumuacha
- Hayo ni maamuzi ya kishetani

BADILIKA.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom