Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,597
Kwa wale ambao wako kwenye ndoa au mahusiano, kuna wakati mwenzi wako anakusimulia kuwa mtu fulani (ama unamfahamu au la) amemchokoza kwa kutaka wawe na mahusiano ya kimapenzi (amemtongoza). Kuna watu wanadhani kwamba kuambiwa kitu cha namna hiyo inaonesha kuwa mwenzi wako ni mwaminifu na kutoambiwa ni kinyume chake. Binafsi sipendi kuambiwa ila kuna wakati natamani (kama binadamu) kujua kama hayo yanamkuta mwenzangu na akina nani wanamtokea, ingawa kiukweli najua yanatokea. Je wewe unapenda kuambiwa?