Utajisikiaje ukiwa na mdogo wako

Afrika Furaha

JF-Expert Member
Dec 16, 2010
329
9
Utajisikiaje ukiwa umeongozana na mdogo wako uliyemzidi miaka kama 8 hivi, mnaenda sehem mnakutana na watu tofauti lakin cha ajabu wakimuona dogo lako wanamwamkia SHIKAMOO Bro, anapewa na kiti akae, halafu wewe unapewa MAMBO VP MSHIKAJI halafu unaambiwa WE BADO KIJANA MDOGO SIMAMA KIDOGO ULE TIZI UKOMAE . . .?
 
Nitajisikia vizuri mno. Nitawashukuru wazazi wangu kwa kunirithisha "genes" nzuri ambazo zinanifanya nionekane bado yanki kuliko umri wangu wa kweli.

Nani anayetaka kuonekana kama ana miaka 50 wakati umri wake ni miaka 30? Si mimi...labda wengine.
 
Sorry naona kama vile mnanitania... nitawapiga ban fasta
 
Kama una ego kubwa, na unahusudu ukubwa utakasirika.

Kama unaelewa vitu kwa kina zaidi utacheka na kushukuru kwamba huonekani kuzeeka mapema.

Wakati wengine wanatumia pesa nyingi sana ili waonekane vijana bado, wengine wanakasirika kwa sababu wanaonekana vijana bado.

Ni vijimambo vya maisha tu.
 
Kama una ego kubwa, na unahusudu ukubwa utakasirika.

Kama unaelewa vitu kwa kina zaidi utacheka na kushukuru kwamba huonekani kuzeeka mapema.

Wakati wengine wanatumia pesa nyingi sana ili waonekane vijana bado, wengine wanakasirika kwa sababu wanaonekana vijana bado.

Ni vijimambo vya maisha tu.

Ikitokea mara moja unaweza kucheka, lakin ikiwa inatokea kila mara inakera bwana . . . mbali na kusema huonekani mzee lakin UNADHALILIKA MBELE YA WATU . . . ipo siku itakutokea mbele ya mkeo au mkweo . . . sijui napo utaona kawaida?
 
Ikitokea mara moja unaweza kucheka, lakin ikiwa inatokea kila mara inakera bwana . . . mbali na kusema huonekani mzee lakin UNADHALILIKA MBELE YA WATU . . . ipo siku itakutokea mbele ya mkeo au mkweo . . . sijui napo utaona kawaida?

Huenda pia hili jambo ni la tofauti za kiutamaduni maana kwenye nchi magharibi watu wanajidunga botox kuondoa makunyanzi ambayo ni alama ya uzee.
 
Ikitokea mara moja unaweza kucheka, lakin ikiwa inatokea kila mara inakera bwana . . . mbali na kusema huonekani mzee lakin UNADHALILIKA MBELE YA WATU . . . ipo siku itakutokea mbele ya mkeo au mkweo . . . sijui napo utaona kawaida?

Fikra kwamba unadhalilika mbele ya watu inatoka wapi? Au tunahalalisha kudhalilisha wadogo?

Mimi ni kaka mkubwa kwenye familia, na sina tabia ya kutaka kuabudiwa kwa sababu ya ukubwa, naongea na wadogo vizuri tu na kuwaheshimu wote sawa tu.

Tatizo kubwa linajionyesha hapa ni kwamba tunadharau wadogo. Nelewa kuhusu umuhimu wa kuthamini busara zinazokuja na umri, lakini je hili linamaanisha kwamba automatically udogo ni wa kubezwa?
 
Fikra kwamba unadhalilika mbele ya watu inatoka wapi? Au tunahalalisha kudhalilisha wadogo?

Mimi ni kaka mkubwa kwenye familia, na sina tabia ya kutaka kuabudiwa kwa sababu ya ukubwa, naongea na wadogo vizuri tu na kuwaheshimu wote sawa tu.

Tatizo kubwa linajionyesha hapa ni kwamba tunadharau wadogo. Nelewa kuhusu umuhimu wa kuthamini busara zinazokuja na umri, lakini je hili linamaanisha kwamba automatically udogo ni wa kubezwa?

nadhani umeenda mbali kidogo, udogo haubezwi ila unatakiwa upewe heshima stahiki, ukubwa nao upewe heshima stahiki. Udogo hauheshimiki kwa kuibia heshima ya wakubwa . . . udogo ukubali kuwa udogo tu
 
nadhani umeenda mbali kidogo, udogo haubezwi ila unatakiwa upewe heshima stahiki, ukubwa nao upewe heshima stahiki. Udogo hauheshimiki kwa kuibia heshima ya wakubwa . . . udogo ukubali kuwa udogo tu

Sasa kwa nini mtu ajisikie vibaya kuonwa mdogo ? Au ndiyo habari ya kupenda ukubwa niliyoitaja juu?

Hata manabii wamesema anayejikuza hushushwa, anayejishusha hukuzwa. The rejected stone is now the cornerstone, sorta like the masterbuilder when I make my way home.

You know my steez.
 
Sasa kwa nini mtu ajisikie vibaya kuonwa mdogo ? Au ndiyo habari ya kupenda ukubwa niliyoitaja juu?

Hata manabii wamesema anayejikuza hushushwa, anayejishusha hukuzwa. The rejected stone is now the cornerstone, sorta like the masterbuilder when I make my way home.

You know my steez.


Kwani kuwa mkubwa ni kujikuza? Ukubwa wa umri sio cheo cha kazin kwamba unaweza kushushwa au kupunguzwa. Unaweza ukamdharau mkubwa lakin KAMWE huwezi punguza umri wake. Pia unatakiwa ufaham kuwa hapa sio kwamba mkubwa atamchukia mdogo kwa tukio walilofanya wengine, badala yake ni challenge kwa jamii kutotambua mtu kwa kuangalia sura . . . sijui unanielewa?
 
Kwani kuwa mkubwa ni kujikuza? Ukubwa wa umri sio cheo cha kazin kwamba unaweza kushushwa au kupunguzwa. Unaweza ukamdharau mkubwa lakin KAMWE huwezi punguza umri wake. Pia unatakiwa ufaham kuwa hapa sio kwamba mkubwa atamchukia mdogo kwa tukio walilofanya wengine, badala yake ni challenge kwa jamii kutotambua mtu kwa kuangalia sura . . . sijui unanielewa?

Kama unaelewa hili tatizo liko wapi?

Jamii inaweza kuchukulia mkubwa ni mdogo na mdogo ni mkubwa kwa mujibu wa muonekano, ama sivyo itabidi tutembee na vitambulisho vyenye tarehe ya kuzaliwa na kuvionyesha kila tunapoenda ili watu wasituchanganye.

Wewe tatizo lako hasa ni nini? Unaona kuambiwa mdogo ni kudharauliwa au vipi ?
 
Kama unaelewa hili tatizo liko wapi?

Jamii inaweza kuchukulia mkubwa ni mdogo na mdogo ni mkubwa kwa mujibu wa muonekano, ama sivyo itabidi tutembee na vitambulisho vyenye tarehe ya kuzaliwa na kuvionyesha kila tunapoenda ili watu wasituchanganye.

Wewe tatizo lako hasa ni nini? Unaona kuambiwa mdogo ni kudharauliwa au vipi ?

Naona kama una JAZBA fulani hivi, au pengine una lako jambo hapa. Ulipoingiza maneno KUTEMBEA NA VITAMBULISHO VYENYE TAREHE ZA KUZALIWA ulinifanya nikufikirie mara mbili-mbili uwezo wako wa kuoanisha mambo? Na bado unaniuliza KUITWA MDOGO NI KUDHARAULIWA AU? Naona hatulingani uwezo wa kufikiria . . . iache tu mada ipite
 
Naona kama una JAZBA fulani hivi, au pengine una lako jambo hapa. Ulipoingiza maneno KUTEMBEA NA VITAMBULISHO VYENYE TAREHE ZA KUZALIWA ulinifanya nikufikirie mara mbili-mbili uwezo wako wa kuoanisha mambo? Na bado unaniuliza KUITWA MDOGO NI KUDHARAULIWA AU? Naona hatulingani uwezo wa kufikiria . . . iache tu mada ipite
toka haraka hapo umeingia choo cha kike
 
Utajisikiaje ukiwa umeongozana na mdogo wako uliyemzidi miaka kama 8 hivi, mnaenda sehem mnakutana na watu tofauti lakin cha ajabu wakimuona dogo lako wanamwamkia SHIKAMOO Bro, anapewa na kiti akae, halafu wewe unapewa MAMBO VP MSHIKAJI halafu unaambiwa WE BADO KIJANA MDOGO SIMAMA KIDOGO ULE TIZI UKOMAE . . .?
Nitafurahi....
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom