Utajiri wenye uchungu

NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.

Sehemu ya tisa.

Siku zikaendelea kukatika, wakati Dylan anaanza kusoma hapo ndipo bi Leticia alipogundua kwamba mtoto huyo alikuwa na uwezo mkubwa mno. Alipelekwa katika shule ya uswahilini ya Mississippi Nusery School ambapo baada ya kufika hapo, yeye ndiye alikuwa mwanafunzi wa kwanza kujua kusoma na kuandika.
Hilo lilikuwa gumu kuaminika kwa walimu lakini ndivyo hali ilivyokuwa. Aliendelea kukua kila siku, uwezo wake uliendelea kuonekana kwani kwa kipindi kifupi alichokuwa amesoma shuleni hapo, hata kwenye kuandika hakuwa na tatizo lolote lile.
Bi Leticia alipopewa taarifa kwamba mtoto wake alikuwa na uwezo mkubwa darasani, akamshukuru Mungu kwa kumpa mtoto aliyekuwa na akili kama ilivyokuwa kwa Dylan.
Huo ulikuwa mwanzo tu, uwezo wake uliendelea kuonekana kila siku huku akiwaongoza wanafunzi kila walipofanya mtihani. Katika kipindi ambacho alimaliza masomo ya elimu yake ya chini ya msingi, Dylan ndiye aliyekuwa ameongoza kwa kufaulu vizuri zaidi ya wanafunzi wote shuleni hapo.
Hakuwa msomaji, hakuwahi kuchukua daftari na kujisomea, muda wake mwingi ulikuwa ni kwenda uwanjani na mpira wa kucheza kikapu. Hicho ndicho kitu alichokipenda sana lakini lilipokuja suala la kufanya mitihani, Dylan alikuwa moto wa kuotea mbali.
“Nimebadili...”
“Umebadili nini?”
“Sitaki kuwa mchungaji...”
“Kwa nini?”
“Ninataka kuwa na fedha, niwe tajiri, niheshimike na nijulikane dunia nzima...” alisema Dylan.
“Kwa hiyo unataka kuwa nani?”
“Nataka niwe mcheza kikapu...”
“Unasemaje?”
“Ninataka kuwa mcheza kikapu mashuhuri duniani,” alisema Dylan.
Hicho ndicho alichokipata, wazo lake la kuwa mchungaji halikuwepo tena, kitu alichokifikiria kwa kipindi hicho ni kuwa mcheza kikapu hapohapo nchini Marekani. Urefu wake ulimpa moyo kwamba angefanikiwa kuwa miongoni mwa wachezaji mahiri hapo baadaye, alitaka ajulikane ila mbali na hiyo, alitaka kuwa na fedha, atajirike ili mama yake atoke katika maisha ya umasikini aliyokuwa nayo.
“Nitakuwa tajiri mama, nitakutoa hapa ulipo,” alisema Dylan huku akionekana kumaanisha alichokisema.
“Nitashukuru sana, nitafurahi kukuona ukifanikiwa,” alisema bi Leticia.
Siku ziliendelea kwenda mbele, pamoja na kusoma lakini hakuacha kucheza mpira wa kikapu. Mwili wake ulikuwa mwembamba sana hivyo akashauriwa kunyanyua vyuma, hilo wala halikuwa tatizo, akafanya hivyo kwa ajili ya kuongeza mwili.
Kutokana na kuupenda sana mchezo huo, akajikuta akisahau kabisa kusoma jambo lililomtia wasiwasi bi Leticia na walimu wengine lakini kitu cha ajabu kabisa, kwenye mitihani, namba yake ilikuwa ileile, namba moja.
Mpaka muda wa kufanya mtihani wa mwisho wa shule za sekondari ambapo kwa Tanzania ingekuwa kidato cha nne, Dylan aliingia ndani ya chumba cha mtihani kwa ajili ya kufanya mtihani huo na kuendelea na mambo yake.
Hakupenda kusoma, kitu alichokifikiria kilikuwa ni kucheza mchezo wa kikapu tu. Katika kipindi hicho ambacho mtihani ulikuwa ukifanyika ndiyo kipindi ambacho mashindano ya kikapu kitaifa kwa watu walio chini ya miaka kumi na nane yalikuwa yakifanyika.
Alifanya mitihani harakaharaka ili awahi nyumbani kucheza katika timu yake ya mitaani kwani kupitia michezo hiyo, kulikuwa na mawakala mbalimbali waliokuwa wakifika na kutafuta wachezaji kwa ajili ya kuwapeleka ligi kuu.
“Vipi? Nilisikika upo kwenye mtihani!” alisema rafiki yake.
“Ndiyo! Nimefanya harakaharaka ili niwahi...”
“Mmh!”
“Usijali, nitafanya vizuri...” alisema Dylan.
Mashindano hayo yalikuwa na umuhimu mkubwa sana kuliko masomo yake, japokuwa alikuwa na uwezo mkubwa darasani, hakupanga kuwa mwanasheria au daktari, kitu alichokitaka ni kuwa miongoni mwa wachezaji kikapu wenye majina makubwa duniani, atengeneze fedha na kuwa bilionea mkubwa, yote hiyo ilikuwa ni sababu ya umasikini mkubwa aliokuwa nao mama yake.
Mashindano hayo yaliyojulikana kama Underground Bassketball U18 yalipoanza, watu wengi wakavutiwa, wakaanza kuyafuatilia katika kila mechi iliyokuwa ikifanyika. Watu wengi walikuwa wakijaa katika viwanja vilivyokuwa vikitumika kwa ajili ya mashinano hayo na kuangalia mechi hizo.
Hapo ndipo Dylan alipoanza kupata jina, alikuwa shujaa wa timu yake ya mtaani iliyojulikana kwa jina la Cobra, alikuwa na uwezo wa kuruka juu na kufunga pointi mfululizo. Kutokana na umahiri huo.
Dylan akaanza kufagiliwa na wanawake wengi, kila timu yake ilipokuwa ikicheza, wasichana waliongezeka, walichotaka ni kumuona huyo Dylan ambaye tayari alikuwa gumzo tena huku taarifa za chini zikisema kwamba tayari wakala wa timu ya kikapu ya Chicago Bulls iliyokuwa ikishiriki Ligi ya Kikapu ya NBA nchini humo aliongea na kocha wa timu hiyo ya kina Dylan kwa ajili ya kumsajiri mchezaji huyo.
Maisha ya kimasikini yalimpiga mno, hakutaka kuendelea kuishi huko, aliwaona watu wakiwa na fedha, walitembelea magari ya kifahari na kuyabadilisha kadiri walivyotaka. Aliyapenda maisha hayo lakini hakuwa na jinsi, hakuwa na uwezo na kitu pekee alichokihitaji kwa wakati huo kilikuwa ni pesa tu hata kama umri wake ulikuwa mdogo.
Aliposikia tetesi kwamba kulikuwa na mawakala wa timu mbalimbali za kikapu ambao walifika mahali hapo, akaongeza juhudi, hakutaka kuishia hapo, alicheza kwa nguvu kubwa kwani kwake hiyo ilionekana kuwa kama nafasi ya mwisho ambayo kama angeipoteza basi asingeweza kuipata tena.
Alifunga pointi nyingi, aliruka juu, tena kwa ustadi mkubwa na kwa kumwangalia ilikuwa rahisi kugundua kwamba Dylan angekuwa mchezaji mkubwa, mwenye jina kubwa hapo baadaye.
Mashindano hayo yaliendelea kwa takribani mwezi mzima, yalipomalizika, wachezaji wakaanza kuchukuliwa na timu mbalimbali lakini kwa Dylan, kuchukuliwa ilikuwa ngumu sana.
Alishangaa, hakuelewa ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea. Alicheza vizuri na kuwa mchezaji bora tena huku akiipa ubingwa timu yake, sasa kwa nini hakupata hata nafasi ya kuchukuliwa na timu moja kama ilivyokuwa kwa wachezaji wengine.
“Tatizo?” alimuuliza kocha wake.
“Subiri, usiwe na presha...”
“Lazima niwe nayo! Nimekuwa mchezaji bora, nimeipa timu ubingwa, yaani hata kuuliziwa sijauliziwa kweli! Kuna nini?” aliuliza Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa.
Machozi yalimlenga, moyo wake uliumia mno, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea, alijitoa sana katika mashindano hayo lakini mpaka katika kipindi hicho, mambo yalikuwa kimya kabisa.
Hakutaka kubaki hivihivi, muda ulizidi kwenda, alichokifanya ni kuanza kuulizia tatizo lilikuwa nini. Jibu alilolipata ni kwamba tangu mchezo wa kwanza alioucheza, kila mtu alivutiwa naye, timu sita za Ligi Kuu ya NBA zilimwania na walichokifanya viongozi wa timu yake ya mtaani ni kuangalia yupi alikuja na fedha nzuri.
Hicho ndicho kilichokwamisha, wote walitaka kupata fedha nyingi pasipo kujua ni kwa jinsi gani kukataa kwao kusaini mkataba wa kukubali kumuuza ulimuumiza moyoni mwake.
Dylan alipogundua hilo, akashinikiza kuuzwa, kila siku alikuwa ofisini kwa kocha wake, alimwambia wazi kwamba alikuwa kijana masikini ambaye alimuahidi mama yake kwamba ni lazima apambane ili apate fedha na kuyabadilisha maisha yao na hakukuwa na kitu alichokitegemea kuyabadilisha maisha yao zaidi ya kucheza kikapu kwa nguvu zote.
“Hilo nalifahamu Dylan...” alisema kocha wake.
“Tatizo nini sasa?”
“Hii ni biashara, tunaangalia fedha...”
“Kwa hiyo sitouzika?”
“Ndiyo tunawasikilizia waongeze fedha...” alisema kocha huyo.
Moyo wa Dylan ukawaka kwa hasira, hakuona umuhimu wa kuitumikia timu hiyo na wakati ilimzuia hata kumuuza kwa kisingizio cha kuhitaji fedha zaidi. Hakutaka kubaki ofisini humo, alichokifanya ni kuondoka, aliondoka kimasihara sana, wakahisi kwamba kesho yake angerudi lakini huo ndiyo ukawa mwisho wa kurudi katika timu hiyo, akapotea na hata alipofuatwa na uongozi wa timu, aliwaambia wazi aliamua kuachana na masuala ya mchezo wa kikapu.
Yalikuwa ni maamuzi magumu, yalimuumiza lakini hakuwa na jinsi, alitaka kuyabadilisha maisha ya familia yake, aliuchukia mno umasikini, alimchukia mtu yeyote ambaye alisimama mbele yake na kumzuia kupata mafanikio aliyoyataka maishani mwake.
Wiki mbili baada ya kuondoka katika timu hiyo ndipo wakapokea barua kutoka shuleni kwamba Dylan alitakiwa kwenda katika ikulu ya Marekani kwa ajili ya kuzungumza na rais kutokana na kufaulu vizuri katika masomo yake.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumamosi.

Au unaweza kuinunua simulizi hii yote kwa sh. 4000, namba hiyo hapo juu njoo tudiscuss.
 
Hahaha umeona eh



Ahhahhahah nyemo ameshaanza
Madame asantee
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.

Sehemu ya Kumi.

Wote walibaki wakimwangalia Dylan, alifana mno na Bwana James kiasi kwamba wakaamini maneno kuwa kweli duniani kulikuwa na watu wawili-wawili. Kwa Catherine, mbali na mfanano aliokuwa nao kijana huyo, akahisi moyo wake ukianza kumpenda, kila alipomwangalia alihisi kabisa kuwa na mapenzi mazito moyoni mwake.
Hakujua kama kweli yalikuwa mapenzi ya kweli au kwa sababu mvulana huyo alikuwa na akili nyingi zaidi yake. Kila alipomwangalia, aliachia tabasamu pana.
“Ninamshukuru Mungu kwa hatua hii niliyofikia, huwa niliamini kwamba mafanikio yangu yapo kwenye mchezo wa kikapu, nikaweka tegemeo langu huko kabla ya viongozi wa timu kukataa kuniuza bila kujali ni umasikini wa aina gani unaitafuna familia yangu. Mbali na mchezo wa kikapu, kumbe kuna sehemu nyingine naweza kufanikiwa, naahidi kupambana, nitakuwa mfanyabiashara mkubwa sana hapa,” alisema Dylan, japokuwa alitoa tabasamu pana, lakini wengi waligundua kwamba tabasamu hilo halikuwa kutoka moyoni.
Akakabidhiwa zawadi yake na kuteremka. Alishindwa kuvumilia, machozi yakaanza kumtoka machoni mwake, aliumia mno, kila alipofikiria maisha aliyokuwa akipitia na mama yake, alihisi kwamba dunia haikuwa na usawa kabisa.
Sherehe iliendelea, watu walikunywa, kila mmoja mahali hapo alionekana kuwa na furaha kubwa isipokuwa watu wawili tu, Dylan na mama yake. Watu hao wawili walionekana kuwa na majonzi, leo hii walikuwa katika jumba kubwa, lililokuwa likiheshimiwa duniani lakini kila walipofikiria kwamba mara watakapotoka ndani ya jumba hilo walitakiwa kwenda kwenye nyumba yao ya kawaida, hakika mioyo yao iliumia mno.
“Habari yako...” Dylan alisikia sauti kutoka nyuma yake, alipogeuka, macho yake yakatua kwa msichana mzuri wa sura, mwenye uso wa tabasamu pana, alikuwa Catherine.
“Safi mrembo, karibu...”
“Asante! Hongera sana, sikufikiria kama kungekuwa na mtu mwenye akili kama zako,” alisema Catherine huku akiliachia tabasamu pana usoni mwake, Dylan akazidi kuchanganyikiwa.
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Asante sana...”
“Inaelekea unasoma sana?”
“Hapana! Sikumbuki mara ya mwisho kujisomea ilikuwa lini, labda nilipokuwa mdogo,” alisema Dylan.
“Mmh! Basi hongera zako!”
Catherine alijitahidi kuzungumza na kijana huyo, alitaka kumzoea kwa ukaribu, alizungumza naye huku muda wote akionekana kuwa mwenye furaha tele. Walipoona wamezoeana vya kutosha, Catherine akamchukua Dylan na kwenda kumtambulisha kwa mama yake kama rafiki yake mpya ambaye mwanamke huyo aliukubali urafiki huo kwa moyo mweupe.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa urafiki wao, mara kwa mara walikuwa wakichati kupitia simu zao, kila mmoja alimpenda mwenzake lakini hakukuwa na mtu aliyekuwa tayari kumwambia mwenzake kwamba alimpenda kwa moyo wa dhati.
Catherine alimuogopa Dylan, hakuamini kama mvulana huyo angekubali kuwa wake, hakujiamini kabisa, kila alipomfikiria, alihisi kabisa moyo wake ukiwa na hofu kubwa hivyo kupotezea ila kwa upande wa Dylan, aliogopa kumwambia msichana huyo ukweli kwa sababu tu kwa muonekano wake alionekana kuwa mtoto wa tajiri ambaye hakustahili kabisa kuwa naye.
Urafiki huo ukaendelea mpaka walipoingia chuoni, kwa miaka miwili, hawakuwa wameonana tena, kazi kubwa waliyokuwa wakiifanya ni kuwasiliana kwenye simu tu. Wakati Dylan akifaulu mtihani wake na kujiunga na Chuo cha Boston University School of Business kilichokuwa Massachusetts kwa ajili ya kuchukua masomo ya kitabibu huku Catherine akijiunga na Chuo Kikuu cha Harvard kilichokuwa hukohuko Massachusetts na kuchukua masomo ya sheria.
Hiyo ilionekana kuwa nafasi yao ya kuonana, wote walikuwa katika jimbo moja japokuwa vyuo vilikuwa mbalimbali mno lakini wakapanga kwamba ilikuwa ni lazima waonane kwani kwa kufanya hivyo ukaribu wao ungekuwa mkubwa na kuzoeana zaidi.
Kwa kuwa mchezo wa kikapu ulikuwa kwenye damu yake, Dylan akapata wakati mgumu sana, kila alipowaona watu wakicheza katika timu ya chuo, akapata hamu ya kutaka kucheza nao.
Hakukuwa na mtu aliyejua uwezo wake, wengi walipomuona, walimdharau na kumtania alikuwa na urefu wa bure na wakati hakuwa na uwezo wowote ule katika kucheza mpira wa kikapu.
Maneno hayo yalimkwaza sana lakini aliendelea kuvumilia mpaka pale alipoona kwamba uvumilivu umemshinda hivyo alitakiwa kuwaonyeshea watu hao yeye alikuwa nani katika mchezo huo.
Alipoomba kujiunga na timu ya chuo kwa upande wa mchezo wa kikapu, wengi walimpuuzia, walimdharau kwa kumuona hajui lakini alipopewa nafasi, kila mtu alishika mdomo kwa mshangao, katika maisha yao, hawakuwahi kumuona mchezaji aliyekuwa na uwezo mkubwa kama aliokuwa nao Dylan.
Siku hiyo alipoonyesha uwezo mkubwa uwanjani, wasichana wakashindwa kuvumilia, wengi wakaanza kujigonga huku wakitamani mvulana huyo atoke nao kimapenzi. Hilo lilikuwa suala lililomnyima furaha sana Dylan, hakutaka kuwa na msichana yeyote, katika maisha yake kipindi hicho, alihitaji kuwa peke yake kwani hakukuwa na kitu alichokipenda kama kutokuwa na msichana yeyote.
Hakuwahi kufanya mapenzi na msichana yeyote na wala hakuwahi kuwa kwenye uhusiano na msichana yeyote yule, kile alichokipenda moyoni mwake ni kuwa peke yake tu, alijitahidi kusoma, kucheza kikapu ili mwisho wa siku kufanikiwa na kuwa bilionea.
“Catherine.....” aliita Dylan kwenye simu.
“Nipo hapa...”
“Kuna kitu nataka kukwambia....”
“Kitu gani tena...”
“Ooh! Au basi...”
“Hapana! Niambie kitu gani!’
“Kuna kitu kinanisumbua tangu utotoni, sina raha nacho kabisa, kinanitesa na kuniua moyoni mwangu,” alisema Dylan kwa sauti ya chini.
“Kitu gani jamani?”
“Nikuulize swali?”
“Niulize...”
“Unanipenda?”
“Ndiyo, tena sana...”
“Ila...au subiri...naomba nikwambie siku nyingine, ila jua kwamba ni kitu kinachoniumiza sana moyoni mwangu...” alisema Dylan, hakutaka kusikia Catherine angesema nini, alichokifanya ni kukata simu, kilichofuatia ni sauti ndogo ya kilio cha kwikwi.
****
Mapenzi yalimuumiza mno, kila siku alikuwa mtu wa kumfikiria Dylan tu, alimpenda mvulana huyo na alikuwa tayari kwa kila kitu. Kitendo cha kumwambia kwamba kulikuwa na kitu alitaka kumwambia lakini akanyamaza, kilimpa mawazo mengi Catherine kiasi kwamba alibaki akiwa na mawazo tele.
Hakutaka kukubali, alichokifanya ni kuchukua simu yake na kuanza kumpigia tena, simu iliita, iliita na kuita lakini haikupokelewa kabisa. Hakutaka kukubali, hakutaka kuona anashindwa, aliendelea kumpigia lakini ikatokea kipindi ambacho simu hiyo haikuwa ikipatikana kabisa.
Kichwa chake kilichanganyikiwa mno, hakutaka kubaki chuoni, kitendo cha mvulana huyo kutokupokea simu kilimchanganya sana, alichokitaka kusikia ni kile ambacho Dylan alitaka kumwambia.
Chuoni hakukukalika tena, alichokifanya ni kuondoka na kuelekea katika stesheni ya treni za umeme na kupanda moja ambayo alitaka impeleke kutoka katika Jiji la Cambridge mpaka Boston alipokuwa akisoma Dylan.
Ndani ya treni alikuwa na mawazo mengi, hakuonekana kuwa na raha kabisa, mapenzi yalikichanganya kichwa chake. Hakukuwa na kitu kingine alichokifikiria zaidi ya Dylan tu.
Baada ya dakika thelathini, treni ikaanza kuingia katika Jiji la Boston, kwa haraka sana Catherine akasimama na kwenda mlangoni, alikuwa na presha kubwa ya kutaka kuteremka, amuwahi rafiki yake wa kiume na kuzungumza naye.
Treni iliposimama, hakutaka kubaki ndani ya treni ile, akatoka na kuanza kuondoka. Alitoka ndani ya jengo la kituo hicho na kufuata teksi moja na kuingia ndani, dereva aliyekuwa nje akisubiri abiria, akaingia ndani.
“Where to?” (Unakwenda wapi?) aliuliza dereva mara baada ya salamu.
“Boston University..”
Dereva akawasha gari na kisha kuanza safari ya kuelekea huko. Njiani, hakutaka kuzungumza kitu chochote, bado aliendelea na jitihada zake za kumtafuta Dylan kwenye simu pasipo mafanikio yoyote yale.
Walichukua dakika ishirini ndipo wakafika katika geti la chuo hicho na kusimamisha teksi, harakaharaka Catherine akalipa na kuteremka. Idadi kubwa ya wanachuo ilikuwa katika eneo la chuo hicho, kila mmoja alionekana kuwa bize huku wengi wakiwa wamekaa kimakundi-makundi wakijadiliana.
Hakutaka kujali sana, alichokifanya ni kuelekea ndani kabisa ambapo huko akaanza kumuulizia Dylan. Jina la mvulana huyo lilikuwa kubwa, uwezo wake darasani ulimfanya watu wengi kumfahamu, wengi walimuita kwa jina la kompyuta kutokana na uwezo wake mkubwa aliokuwa nao.
“Mmh! Sijui kama yupo...”
“Kwani leo hajaonekana?”
“Nilimuona kwenye uwanja wa kikapu, baada ya hapo, kuna watu walimfuata, sijui ameelekea wapi,” alisema mwanaume aliyeulizwa na Catherine.
“Wanaume gani?”
“Siwafahamu, walikuwa na miili mikubwa, sidhani kama kuna usalama...”
“Sawa! Nashukuru!”
Japokuwa alimkosa Dylan chuoni lakini hakutaka kuondoka Boston, lengo lake kubwa lililomtoa Cambridge na kumpeleka Boston lilikuwa ni kuonana na mvulana huyo tu. Alihisi kulikuwa na tatizo, hakuwa tayari kuondoka na kurudi chuo, iwe isiwe ilikuwa ni lazima kumuona.
Ilipofika saa mbili usiku, akasikia simu yake ikiita, kwanza akahisi kwamba walikuwa wazazi wake ambao walikuwa na kawaida ya kumpigia simu kila siku usiku, alipoichukua simu na kuangalia kioo, hakuamini, alikuwa Dylan.
“Halo Dylan...” aliita Catherine.
“Upo wapi? Chuo au nyumbani?” ilisikika sauti ya Dylan.
“Nipo hotelini...”
“Hotelini?”
“Ndiyo!”
“Unafanya nini?”
“Nimekuja kukuona!”
“Kwa hiyo upo Boston?”
“Ndiyo!”
“Hoteli gani?”
“San Marino...”
“Sawa! Ngoja nije nikuone...”
“Kweli?”
“Ndiyo! Nipe dakika kadhaa, nina habari njema...”
“Ipi hiyo?”
“Usijali rafiki, nakuja...”
Catherine alijikuta akishusha pumzi ndefu na kuachia tabasamu pana, hakuamini kile alichokisikia kwamba mvulana aliyekuwa akimpenda alikuwa njiani kuelekea katika hoteli ile aliyokuwepo.
Tangu mara ya mwisho kuonana naye katika ikulu ya Marekani, hakuwahi kuonana naye tena mpaka kipindi hicho. Miaka miwili ilikuwa imepita, hakuwahi kumuona zaidi ya kuwasiliana naye kwenye simu tu.
Baada ya dakika arobaini na tano, simu ya mezani ikaanza kulia, akaifuata, akaipokea, sauti aliyoisikia ni ya dada wa mapokezi ambaye alimpa taarifa kwamba kulikuwa na mgeni wake aliyetaka kumuona.
“Mwambie aje...”
Catherine akajiweka vizuri chumbani kwake, akavaa nguo ya kulalia harakaharaka kwani siku hiyo, tena katika usiku kama huo ndiyo ilikuwa yenyewe ya kumfanya Dylan awe mpenzi wake kwa namna alivyojipanga kumtega hasa kwa mikao ya ajabu-ajabu kitandani.
Baada ya dakika kadhaa, akasikia mlango ukigongwa, kwa kuwa alikuwa ameshauacha wazi, akamkaribisha mgongaji, Dylan akaufungua mlango na kuingia ndani. Hali aliyomkuta msichana huyo haikuwa ya kawaida, alivalia nguo ya kulalia iliyoonyesha maungo yake ya ndani, mpaka nguo ya ndani, nyekundu aliyoivaa, ilionekana vizuri.
“Karibu Dylan,” alisema Catherine kwa sauti nyembamba ambayo aliamini ingezisismua ngoma za masikio ya Dylan.
Dylan akameza mate, akabaki akimwangalia Catherine kwa macho yenye matamanio lakini usiku huo alitaka kupinga kufanya naye kitu chochote kile, hakuwa mpenzi wake japokuwa alijisikia hali ya tofauti sana moyoni mwake.
“Kuna nini mpe...Dylan?” aliuliza Catherine.
“Sikiliza, nimechaguliwa kujiunga na timu ya mpira wa kikapu ya Boston...” alisema Dylan huku akitoa tabasamu pana.
“Unasemaje?”
“Ninakwenda kuwa bilionea Catherine, ninakwenda kutajirika...” alisema Dylan kwa sauti kubwa, Catherine aliyekuwa kitandani akasimama na kumsogelea, kilichofuatia ni kumkumbatia kwa nguvu kana kwamba hakutaka atoke mikononi mwake.
“Dylan....” aliita Catherine.
“Nipo hapa...”
“Ninakupenda sana...” alisema Catherine.
“Unasemaje?”
“Ninakupenda...”
“Mimi?”
“Ndiyo!”
“Masikini mimi?”
“Ndiyo! Ninakupenda sana, naomba uwe wangu...”
“Niwe wako mimi?”
“Ndiyo!”
“Hapana Catherine...”
“Kwa nini?”
“Sikiliza Catherine, nina maana yangu kukwambia hivyo...” alisema Dylan.
Dylan akajitoa katika mikono ya Catherine, japokuwa msichana huyo alitamani waendelee kukumbatiana lakini kwa Dylan hakutaka kabisa kuendelea kuwa hivyo kwani isingeleta picha nzuri na wakati hakutaka kabisa kuwa mpenzi wake.
“Naomba uniache Catherine, siwezi kuwa mpenzi wako...” alisema Dylan huku akimtoa msichana huyo mikononii mwake, maumivu aliyoyasikia Catherine moyoni mwake, hayakuweza kusimulika.

Je, nini kitaendelea?
 
Dylan mbona unaniangusha asee,mpe mwenzio kitu roho inataka bwana wewe mwenyewe hapo ulipo unateseka!me sipendi mambo yakutesana bana
 
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.

Sehemu ya Kumi na Moja.

Catherine hakutaka kuamini alichokisikia, moyo wake ulikuwa kwenye mapenzi ya dhati kwa mwanaume huyo ambaye alimpenda kwa moyo wake wote. Kila alipomwangalia, alizidi kumpenda ila maneno aliyomwambia kwamba hawezi kuwa naye, yalimchanganya.
Alishindwa kuvumilia kabisa, hapohapo machozi yakaanza kumtoka machozi mwake na kutiririka mashavuni mwake. Alisafiri kutoka Cambridge mpaka Boston kwa ajili ya kumwambia mwanaume huyo kwamba alikuwa akimpenda, alipoufikisha ujumbe wake huo, eti mwanaume huyo akamwambia kwamba hawezi kuwa mpenzi wake.
“Dylan, ninakupenda sana, naomba uwe wangu,” alisema msichana huyo huku akionekana kuumia moyoni mwake.
“Catherine, haujui ni kitu gani kinaendelea katika maisha yangu,” alisema Dylan kwa sauti ya chini, alionekana kuwa na huzuni mno.
“Kitu gani?”
“Ndiyo maana nakwambia achana na mimi, mbali na umasikini, sitokufanya uyafurahie mapenzi...” alisema Dylan.
“Dylan, nakuomba tafadhali, naomba uwe wangu,” alisema msichana huyo.
Japokuwa Catherine aliomboleza kwa kumtaka mwanaume huyo awe naye lakini hilo halikuwezekana hata kidogo, bado aliendelea kusisitiza kwamba hakutaka awe mpenzi wake hivyo aachwe kama alivyokuwa.
“Naomba nikuulize swali...” alisema Catherine.
“Uliza...”
“Unanipenda?”
“Ndiyo! Ninakupenda sana Catherine...”
“Namaanisha kimapenzi...unanipenda?”
“Na mimi nimemaanisha kimapenzi, ninakupenda mno,” alisema Dylan.
“Kwa nini hutaki kuwa mpenzi wangu?” aliuliza Catherine.
“Kwa sababu sitaki ulie, hilo tu...”
“Hutaki nilie, kwa sababu gani? Una msichana mwingine?”
“Sina na sitegemei kuwa na msichana yeyote katika maisha yangu, nitabaki peke yangu milele, ila suala la kuwa nawe, haliwezekani,” alisema Dylan huku macho yake tu yakionyesha ni jinsi gani alimaanisha alichokisema.
Hakupata alichokitaka, alikuwa mnyonge na wala hakutaka kukaa huko Boston, alichokifanya ni kuondoka zake na kurudi New York kwani kwa jinsi alivyochanganyikiwa, asingeweza kabisa kurudi chuoni na kusoma.
Njiani, ndani ya ndege, alikuwa na mawazo lukuki, hakukuwa na siku ambayo moyo wake uliumia kama siku hiyo, hapo kabla alikuwa na uhakika kwamba angeanzisha uhusiano wa kimapenzi na Dylan lakini kitu alichokutana nacho huko kilimnyong’onyeza na hakuwa na nguvu hata kidogo.
*****
“Amefanana na mimi?” aliuliza Bwana James.
“Ndiyo! Amefanana na wewe, kama mapacha,” alisema bi Claire huku akimwangalia mume wake usoni.
“Anaitwa nani?”
“Dylan Christopher, ni mrefu kama wewe...”
“Hahaha! Basi tutakuwa wawili-wawili...” alisema Bwana James.
Bi Claire aliamua kumtaarifu mume wake juu ya mfanano aliokuwa nao na kijana ambaye walikutana naye wakati walipokwenda Ikulu kula chakula na rais. Bwana James alipoambiwa, alionekana kuwa mwenye furaha tele hasa baada ya kuona kwamba hata watu aliokuwa nao, wote walimfananisha na huyo kijana.
Mawazo juu ya kijana huyo yalimsumbua kichwani mwake, alitamani kuonana naye hata siku moja lakini kutokana na ubize mkubwa aliokuwa nao, alishindwa kabisa. Kila siku alikuwa mtu wa kukaa ofisini mwake, mezani kulikuwa na mafaili mengi yaliyokuwa na karatasi ambazo alitakiwa kuziandika na kuhakikisha kila kitu kinakwenda kama kinavyotakiwa kwenda.
Fedha hazikuisha, kila siku ziliendelea kuingia katika akaunti yake na kumfanya kuwa bilionea mkubwa. Aliyakumbuka maisha aliyoishi kabla, yalikuwa ya kimasikini ambapo alishindwa hata kupata dola mia tano.
Hakutaka kuishi maisha hayo tena, alitaka kupata fedha zaidi na kumfanya kuwa tajiri mkubwa baadaye. Alihakikisha familia yake ikipata kila kitu, hakutaka kuiona ikiteseka au ikipata matatizo yoyote yale.
Maisha yaliendelea, mwaka wa kwanza ukapita, wa pili ukaingia na ndipo mawazo juu ya huyo kijana yalipoanza kurudi tena kichwani mwake. Hakujua ni kwa sababu gani lakini kila siku alipokuwa akikaa ofisini mwake, kitu cha kwanza kilikuwa ni kumfikiria kijana huyo, mawazo juu yake yaliendelea kumtesa kila siku.
“Huyo kijana yupo wapi?” aliuliza Bwana James.
“Catherine alisema yupo Boston...”
“Ninataka kuonana naye, mawazo juu yake yamekuwa yakinitesa sana, au hata picha zake unazo?” aliuliza Bwana James.
“Hapana, ila nina uhakika Catherine anazo...”
“Hebu mpigie simu...”
Bi Claire akafanya kama alivyoambiwa, akampigia simu binti yake lakini haikuweza kupatikana zaidi ya kuambiwa aache ujumbe mfupi wa maneno. Hakuacha ujumbe wowote ule, akaikata simu kwa lengo la kujaribu hapo baadaye.
Baada ya kupita saa mbili, binti yao, Catherine akarudi nyumbani hapo. Kwanza kila mmoja alishangaa, muda huo alitakiwa kuwa chuoni, wakati wanajiuliza hilo, wakagundua kwamba binti yao hakuwa sawa kabisa, alionekana kuwa na mawazo tele, tena hata macho yake yaliwatisha, yalikuwa mekundu hali iliyoonyesha kwamba muda mchache uliopita alikuwa akilia.
“Kuna nini?” aliuliza mama yake. Catherine hakujibu zaidi ya kuelekea chumbani kwake.
Wakahisi kulikuwa na tatizo, alichokifanya bi Claire ni kumfuata binti yake, alitaka kufahamu ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea mpaka kumrudisha nyumbani tena huku akionekana kuwa na huzuni.
“Moyo unaniuma mama...” alisema Catherine huku akiyafuta machozi yake.
“Kuna nini?”
Mama yake alikuwa kila kitu katika maisha yake, alimchukulia kama rafiki yake wa karibu na kila kitu kilichomsumbua, hakumficha, alimwambia ukweli.
Alichokifanya Catherine ni kumwambia mama yake kila kitu kilichokuwa kikiendelea moyoni mwake, alimwambia ukweli kwamba alimpenda sana Dylan tangu siku ya kwanza alipokutana naye, akajitahidi kuwa naye karibu na hatimaye kutamani kuwa mpenzi wake.
“Sasa kipi kinakuliza?” aliuliza mama yake.
“Amenikataa, amesema hataki kuwa mpenzi wangu,” alijibu Catherine huku akilia kama mtoto.
Mama yake akawa na jukumu kubwa la kumbembeleza binti yake. Alimuonea huruma, alikuwa binti yake wa kwanza hivyo kumuona akilia huku akiteseka moyoni mwake, hakika ilimuuma mno.
“Nyamaza, baba yako atakusaidia...” alisema bi Claire kwa sauti ya chini.
“Baba atanisaidia?”
“Ndiyo! Anataka kwenda kuonana naye, nitamwambia kuhusu hilo pia, atakusaidia,” alisema bi Claire huku akimfariji binti yake.
Alichokifanya mwanamke huyo ni kuelekea sebuleni ambapo akamkuta mume wake akiwa ametulia kochini huku akionekana kuwa na mawazo lukuki. Kwa mwendo wa taratibu akamsogelea na kuanza kuzungumza naye.
“Kuna nini?” aliuliza Bwana James.
“Catherine analia...”
“Kisa?”
Bi Claire hakuwa na jinsi, alichokifanya ni kuanza kumuhadithia mume wake kile alichoambiwa na binti yake kule chumbani. Bwana James alihuzunika, katika maisha yake hakutaka kabisa kuona binti yake akilia, hivyo kitendo cha kusikia kwamba binti yake alilia kisa tu kukataliwa na huyo Dylan, ilimuuma mno.
“Tuna fedha, unalijua hilo?” aliamua kumuuliza mke wake.
“Ndiyo!”
“Kama tuna fedha, kipi kinashindikana? Kununua mapenzi?” aliuliza mzee huyo.
“Hakuna kinachoshindikana!”
“Basi ni lazima tukutane na huyo Dylan haraka iwezekanavyo, sipendi kumuona binti yangu akiwa na huzuni, sipendi kumuona akilia,” alisema Bwana James.
Huo ndiyo ulikuwa ukweli, alimpenda mno binti yake mkubwa hata zaidi ya alivyompenda binti yake mdogo, Laura. Kwake, msichana huyo alikuwa kila kitu kitendo cha kuambiwa kwamba alikuwa akilia kisa tu kulikuwa na mwanaume alimkataa, ilimchanganya akili yake.
Aliamini katika fedha kwamba unapokuwa na fedha hakuna kitu chochote kile kinachoshindikana hivyo kama huyo Dylan amekataa kuwa na binti yake, aliamini kama angetumia fedha basi ingekuwa rahisi kwake kumpata na kumuingiza katika mikono ya binti yake.
“Mwambie tunamfuata, tutazungumza naye,” alisema Bwana James huku akionekana kumaanisha alichokisema.
Catherine alipopewa taarifa juu ya kile alichoambiwa, kidogo moyo wake ulikuwa na ahueni kwani hata yeye aliamini kwamba fedha zingeweza kubadilisha kitu chochote kile.
Wakapanga siku ya safari, haikuwa wiki hiyo ila ingefanyika wiki mbiliz zinazofuata. Katika kipindi chote cha kusubiria hiyo safari, bado Catherine alikuwa akiwasiliana na Dylan huku akimsisitiza awe mpenzi wake lakini mwanaume huyo alikataa kwa kusema kwamba alikuwa na sababu yake kubwa, ila ya pili, hakutaka kumuona msichana huyo akiwa kwenye majonzi makubwa.
Siku zikaendelea kukatika, baada ya wiki moja, hapo ndipo familia hiyo ikapanda ndege binafsi na kuelekea Boston. Njiani, walikuwa wakizungumza lakini kichwa cha Catherine kilikuwa na mawazo tele, hakuamini kama kweli Dylan angeweza kukubaliana naye na hatimaye kuwa na uhusiano wa kimapenzi.
Wazazi wake waliendelea kumfariji kwa kumwambia kwamba kila kitu kingewezekana kwani fedha ndicho kitu kilichokuwa na mafanikio makubwa kama tu kingetumika kama kinavyotakiwa.
Walichukua saa mbili, ndege ikatua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Boston ambapo wakateremka na kuanza kwenda hotelini huku wakiwa wamepokelewa kwa magari maalumu, ya kifahari ambayo hayakuwa na uwezo wa kupenyeza risasi.
Bwana James alikuwa bilionea mkubwa, kila alipopita, alinukia fedha, alikuwa mtu anayelindwa sana nchini Marekani kiasi kwamba hata wabaya wake kumpata ilikuwa kazi kubwa.
Baada ya kufika katika hoteli ambayo waliweka oda kwa kuchukua hoteli nzima, wakatulia vyumbani mwao. Japokuwa kwa upande wa Bwana James alionekana kama kupoteza muda, ila alifanya hivyo kama njia mojawapo ya kumfanya binti yake awe na furaha maishani mwake, hakutaka kumuona akilia au akiteseka maishani mwake, kwa kifupi, hakutaka kumuona binti yake huyo akilia kwa uchungu.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumamosi.
 
Asante madame kipenzi
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.

Sehemu ya Kumi na Moja.

Catherine hakutaka kuamini alichokisikia, moyo wake ulikuwa kwenye mapenzi ya dhati kwa mwanaume huyo ambaye alimpenda kwa moyo wake wote. Kila alipomwangalia, alizidi kumpenda ila maneno aliyomwambia kwamba hawezi kuwa naye, yalimchanganya.
Alishindwa kuvumilia kabisa, hapohapo machozi yakaanza kumtoka machozi mwake na kutiririka mashavuni mwake. Alisafiri kutoka Cambridge mpaka Boston kwa ajili ya kumwambia mwanaume huyo kwamba alikuwa akimpenda, alipoufikisha ujumbe wake huo, eti mwanaume huyo akamwambia kwamba hawezi kuwa mpenzi wake.
“Dylan, ninakupenda sana, naomba uwe wangu,” alisema msichana huyo huku akionekana kuumia moyoni mwake.
“Catherine, haujui ni kitu gani kinaendelea katika maisha yangu,” alisema Dylan kwa sauti ya chini, alionekana kuwa na huzuni mno.
“Kitu gani?”
“Ndiyo maana nakwambia achana na mimi, mbali na umasikini, sitokufanya uyafurahie mapenzi...” alisema Dylan.
“Dylan, nakuomba tafadhali, naomba uwe wangu,” alisema msichana huyo.
Japokuwa Catherine aliomboleza kwa kumtaka mwanaume huyo awe naye lakini hilo halikuwezekana hata kidogo, bado aliendelea kusisitiza kwamba hakutaka awe mpenzi wake hivyo aachwe kama alivyokuwa.
“Naomba nikuulize swali...” alisema Catherine.
“Uliza...”
“Unanipenda?”
“Ndiyo! Ninakupenda sana Catherine...”
“Namaanisha kimapenzi...unanipenda?”
“Na mimi nimemaanisha kimapenzi, ninakupenda mno,” alisema Dylan.
“Kwa nini hutaki kuwa mpenzi wangu?” aliuliza Catherine.
“Kwa sababu sitaki ulie, hilo tu...”
“Hutaki nilie, kwa sababu gani? Una msichana mwingine?”
“Sina na sitegemei kuwa na msichana yeyote katika maisha yangu, nitabaki peke yangu milele, ila suala la kuwa nawe, haliwezekani,” alisema Dylan huku macho yake tu yakionyesha ni jinsi gani alimaanisha alichokisema.
Hakupata alichokitaka, alikuwa mnyonge na wala hakutaka kukaa huko Boston, alichokifanya ni kuondoka zake na kurudi New York kwani kwa jinsi alivyochanganyikiwa, asingeweza kabisa kurudi chuoni na kusoma.
Njiani, ndani ya ndege, alikuwa na mawazo lukuki, hakukuwa na siku ambayo moyo wake uliumia kama siku hiyo, hapo kabla alikuwa na uhakika kwamba angeanzisha uhusiano wa kimapenzi na Dylan lakini kitu alichokutana nacho huko kilimnyong’onyeza na hakuwa na nguvu hata kidogo.
*****
“Amefanana na mimi?” aliuliza Bwana James.
“Ndiyo! Amefanana na wewe, kama mapacha,” alisema bi Claire huku akimwangalia mume wake usoni.
“Anaitwa nani?”
“Dylan Christopher, ni mrefu kama wewe...”
“Hahaha! Basi tutakuwa wawili-wawili...” alisema Bwana James.
Bi Claire aliamua kumtaarifu mume wake juu ya mfanano aliokuwa nao na kijana ambaye walikutana naye wakati walipokwenda Ikulu kula chakula na rais. Bwana James alipoambiwa, alionekana kuwa mwenye furaha tele hasa baada ya kuona kwamba hata watu aliokuwa nao, wote walimfananisha na huyo kijana.
Mawazo juu ya kijana huyo yalimsumbua kichwani mwake, alitamani kuonana naye hata siku moja lakini kutokana na ubize mkubwa aliokuwa nao, alishindwa kabisa. Kila siku alikuwa mtu wa kukaa ofisini mwake, mezani kulikuwa na mafaili mengi yaliyokuwa na karatasi ambazo alitakiwa kuziandika na kuhakikisha kila kitu kinakwenda kama kinavyotakiwa kwenda.
Fedha hazikuisha, kila siku ziliendelea kuingia katika akaunti yake na kumfanya kuwa bilionea mkubwa. Aliyakumbuka maisha aliyoishi kabla, yalikuwa ya kimasikini ambapo alishindwa hata kupata dola mia tano.
Hakutaka kuishi maisha hayo tena, alitaka kupata fedha zaidi na kumfanya kuwa tajiri mkubwa baadaye. Alihakikisha familia yake ikipata kila kitu, hakutaka kuiona ikiteseka au ikipata matatizo yoyote yale.
Maisha yaliendelea, mwaka wa kwanza ukapita, wa pili ukaingia na ndipo mawazo juu ya huyo kijana yalipoanza kurudi tena kichwani mwake. Hakujua ni kwa sababu gani lakini kila siku alipokuwa akikaa ofisini mwake, kitu cha kwanza kilikuwa ni kumfikiria kijana huyo, mawazo juu yake yaliendelea kumtesa kila siku.
“Huyo kijana yupo wapi?” aliuliza Bwana James.
“Catherine alisema yupo Boston...”
“Ninataka kuonana naye, mawazo juu yake yamekuwa yakinitesa sana, au hata picha zake unazo?” aliuliza Bwana James.
“Hapana, ila nina uhakika Catherine anazo...”
“Hebu mpigie simu...”
Bi Claire akafanya kama alivyoambiwa, akampigia simu binti yake lakini haikuweza kupatikana zaidi ya kuambiwa aache ujumbe mfupi wa maneno. Hakuacha ujumbe wowote ule, akaikata simu kwa lengo la kujaribu hapo baadaye.
Baada ya kupita saa mbili, binti yao, Catherine akarudi nyumbani hapo. Kwanza kila mmoja alishangaa, muda huo alitakiwa kuwa chuoni, wakati wanajiuliza hilo, wakagundua kwamba binti yao hakuwa sawa kabisa, alionekana kuwa na mawazo tele, tena hata macho yake yaliwatisha, yalikuwa mekundu hali iliyoonyesha kwamba muda mchache uliopita alikuwa akilia.
“Kuna nini?” aliuliza mama yake. Catherine hakujibu zaidi ya kuelekea chumbani kwake.
Wakahisi kulikuwa na tatizo, alichokifanya bi Claire ni kumfuata binti yake, alitaka kufahamu ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea mpaka kumrudisha nyumbani tena huku akionekana kuwa na huzuni.
“Moyo unaniuma mama...” alisema Catherine huku akiyafuta machozi yake.
“Kuna nini?”
Mama yake alikuwa kila kitu katika maisha yake, alimchukulia kama rafiki yake wa karibu na kila kitu kilichomsumbua, hakumficha, alimwambia ukweli.
Alichokifanya Catherine ni kumwambia mama yake kila kitu kilichokuwa kikiendelea moyoni mwake, alimwambia ukweli kwamba alimpenda sana Dylan tangu siku ya kwanza alipokutana naye, akajitahidi kuwa naye karibu na hatimaye kutamani kuwa mpenzi wake.
“Sasa kipi kinakuliza?” aliuliza mama yake.
“Amenikataa, amesema hataki kuwa mpenzi wangu,” alijibu Catherine huku akilia kama mtoto.
Mama yake akawa na jukumu kubwa la kumbembeleza binti yake. Alimuonea huruma, alikuwa binti yake wa kwanza hivyo kumuona akilia huku akiteseka moyoni mwake, hakika ilimuuma mno.
“Nyamaza, baba yako atakusaidia...” alisema bi Claire kwa sauti ya chini.
“Baba atanisaidia?”
“Ndiyo! Anataka kwenda kuonana naye, nitamwambia kuhusu hilo pia, atakusaidia,” alisema bi Claire huku akimfariji binti yake.
Alichokifanya mwanamke huyo ni kuelekea sebuleni ambapo akamkuta mume wake akiwa ametulia kochini huku akionekana kuwa na mawazo lukuki. Kwa mwendo wa taratibu akamsogelea na kuanza kuzungumza naye.
“Kuna nini?” aliuliza Bwana James.
“Catherine analia...”
“Kisa?”
Bi Claire hakuwa na jinsi, alichokifanya ni kuanza kumuhadithia mume wake kile alichoambiwa na binti yake kule chumbani. Bwana James alihuzunika, katika maisha yake hakutaka kabisa kuona binti yake akilia, hivyo kitendo cha kusikia kwamba binti yake alilia kisa tu kukataliwa na huyo Dylan, ilimuuma mno.
“Tuna fedha, unalijua hilo?” aliamua kumuuliza mke wake.
“Ndiyo!”
“Kama tuna fedha, kipi kinashindikana? Kununua mapenzi?” aliuliza mzee huyo.
“Hakuna kinachoshindikana!”
“Basi ni lazima tukutane na huyo Dylan haraka iwezekanavyo, sipendi kumuona binti yangu akiwa na huzuni, sipendi kumuona akilia,” alisema Bwana James.
Huo ndiyo ulikuwa ukweli, alimpenda mno binti yake mkubwa hata zaidi ya alivyompenda binti yake mdogo, Laura. Kwake, msichana huyo alikuwa kila kitu kitendo cha kuambiwa kwamba alikuwa akilia kisa tu kulikuwa na mwanaume alimkataa, ilimchanganya akili yake.
Aliamini katika fedha kwamba unapokuwa na fedha hakuna kitu chochote kile kinachoshindikana hivyo kama huyo Dylan amekataa kuwa na binti yake, aliamini kama angetumia fedha basi ingekuwa rahisi kwake kumpata na kumuingiza katika mikono ya binti yake.
“Mwambie tunamfuata, tutazungumza naye,” alisema Bwana James huku akionekana kumaanisha alichokisema.
Catherine alipopewa taarifa juu ya kile alichoambiwa, kidogo moyo wake ulikuwa na ahueni kwani hata yeye aliamini kwamba fedha zingeweza kubadilisha kitu chochote kile.
Wakapanga siku ya safari, haikuwa wiki hiyo ila ingefanyika wiki mbiliz zinazofuata. Katika kipindi chote cha kusubiria hiyo safari, bado Catherine alikuwa akiwasiliana na Dylan huku akimsisitiza awe mpenzi wake lakini mwanaume huyo alikataa kwa kusema kwamba alikuwa na sababu yake kubwa, ila ya pili, hakutaka kumuona msichana huyo akiwa kwenye majonzi makubwa.
Siku zikaendelea kukatika, baada ya wiki moja, hapo ndipo familia hiyo ikapanda ndege binafsi na kuelekea Boston. Njiani, walikuwa wakizungumza lakini kichwa cha Catherine kilikuwa na mawazo tele, hakuamini kama kweli Dylan angeweza kukubaliana naye na hatimaye kuwa na uhusiano wa kimapenzi.
Wazazi wake waliendelea kumfariji kwa kumwambia kwamba kila kitu kingewezekana kwani fedha ndicho kitu kilichokuwa na mafanikio makubwa kama tu kingetumika kama kinavyotakiwa.
Walichukua saa mbili, ndege ikatua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Boston ambapo wakateremka na kuanza kwenda hotelini huku wakiwa wamepokelewa kwa magari maalumu, ya kifahari ambayo hayakuwa na uwezo wa kupenyeza risasi.
Bwana James alikuwa bilionea mkubwa, kila alipopita, alinukia fedha, alikuwa mtu anayelindwa sana nchini Marekani kiasi kwamba hata wabaya wake kumpata ilikuwa kazi kubwa.
Baada ya kufika katika hoteli ambayo waliweka oda kwa kuchukua hoteli nzima, wakatulia vyumbani mwao. Japokuwa kwa upande wa Bwana James alionekana kama kupoteza muda, ila alifanya hivyo kama njia mojawapo ya kumfanya binti yake awe na furaha maishani mwake, hakutaka kumuona akilia au akiteseka maishani mwake, kwa kifupi, hakutaka kumuona binti yake huyo akilia kwa uchungu.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumamosi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom