Dah!.Naanzaje kwa mfano... Fanya mpango unipatie bank account number nikujaze ya weekend kwanza...
NYEMO CHILONGANI.Ahhahhahah nyemo ameshaanza
Madame asantee
Hawajuani lakiniAiseee... Ndugu wanataka kunjunjana....
Aiseee... Ndugu wanataka kunjunjana....
Sehemu ya saba naona haipoHahaha hataki kusubiri
HahahahaDylan mbona unaniangusha asee,mpe mwenzio kitu roho inataka bwana wewe mwenyewe hapo ulipo unateseka!me sipendi mambo yakutesana bana
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.
Sehemu ya Kumi na Moja.
Catherine hakutaka kuamini alichokisikia, moyo wake ulikuwa kwenye mapenzi ya dhati kwa mwanaume huyo ambaye alimpenda kwa moyo wake wote. Kila alipomwangalia, alizidi kumpenda ila maneno aliyomwambia kwamba hawezi kuwa naye, yalimchanganya.
Alishindwa kuvumilia kabisa, hapohapo machozi yakaanza kumtoka machozi mwake na kutiririka mashavuni mwake. Alisafiri kutoka Cambridge mpaka Boston kwa ajili ya kumwambia mwanaume huyo kwamba alikuwa akimpenda, alipoufikisha ujumbe wake huo, eti mwanaume huyo akamwambia kwamba hawezi kuwa mpenzi wake.
“Dylan, ninakupenda sana, naomba uwe wangu,” alisema msichana huyo huku akionekana kuumia moyoni mwake.
“Catherine, haujui ni kitu gani kinaendelea katika maisha yangu,” alisema Dylan kwa sauti ya chini, alionekana kuwa na huzuni mno.
“Kitu gani?”
“Ndiyo maana nakwambia achana na mimi, mbali na umasikini, sitokufanya uyafurahie mapenzi...” alisema Dylan.
“Dylan, nakuomba tafadhali, naomba uwe wangu,” alisema msichana huyo.
Japokuwa Catherine aliomboleza kwa kumtaka mwanaume huyo awe naye lakini hilo halikuwezekana hata kidogo, bado aliendelea kusisitiza kwamba hakutaka awe mpenzi wake hivyo aachwe kama alivyokuwa.
“Naomba nikuulize swali...” alisema Catherine.
“Uliza...”
“Unanipenda?”
“Ndiyo! Ninakupenda sana Catherine...”
“Namaanisha kimapenzi...unanipenda?”
“Na mimi nimemaanisha kimapenzi, ninakupenda mno,” alisema Dylan.
“Kwa nini hutaki kuwa mpenzi wangu?” aliuliza Catherine.
“Kwa sababu sitaki ulie, hilo tu...”
“Hutaki nilie, kwa sababu gani? Una msichana mwingine?”
“Sina na sitegemei kuwa na msichana yeyote katika maisha yangu, nitabaki peke yangu milele, ila suala la kuwa nawe, haliwezekani,” alisema Dylan huku macho yake tu yakionyesha ni jinsi gani alimaanisha alichokisema.
Hakupata alichokitaka, alikuwa mnyonge na wala hakutaka kukaa huko Boston, alichokifanya ni kuondoka zake na kurudi New York kwani kwa jinsi alivyochanganyikiwa, asingeweza kabisa kurudi chuoni na kusoma.
Njiani, ndani ya ndege, alikuwa na mawazo lukuki, hakukuwa na siku ambayo moyo wake uliumia kama siku hiyo, hapo kabla alikuwa na uhakika kwamba angeanzisha uhusiano wa kimapenzi na Dylan lakini kitu alichokutana nacho huko kilimnyong’onyeza na hakuwa na nguvu hata kidogo.
*****
“Amefanana na mimi?” aliuliza Bwana James.
“Ndiyo! Amefanana na wewe, kama mapacha,” alisema bi Claire huku akimwangalia mume wake usoni.
“Anaitwa nani?”
“Dylan Christopher, ni mrefu kama wewe...”
“Hahaha! Basi tutakuwa wawili-wawili...” alisema Bwana James.
Bi Claire aliamua kumtaarifu mume wake juu ya mfanano aliokuwa nao na kijana ambaye walikutana naye wakati walipokwenda Ikulu kula chakula na rais. Bwana James alipoambiwa, alionekana kuwa mwenye furaha tele hasa baada ya kuona kwamba hata watu aliokuwa nao, wote walimfananisha na huyo kijana.
Mawazo juu ya kijana huyo yalimsumbua kichwani mwake, alitamani kuonana naye hata siku moja lakini kutokana na ubize mkubwa aliokuwa nao, alishindwa kabisa. Kila siku alikuwa mtu wa kukaa ofisini mwake, mezani kulikuwa na mafaili mengi yaliyokuwa na karatasi ambazo alitakiwa kuziandika na kuhakikisha kila kitu kinakwenda kama kinavyotakiwa kwenda.
Fedha hazikuisha, kila siku ziliendelea kuingia katika akaunti yake na kumfanya kuwa bilionea mkubwa. Aliyakumbuka maisha aliyoishi kabla, yalikuwa ya kimasikini ambapo alishindwa hata kupata dola mia tano.
Hakutaka kuishi maisha hayo tena, alitaka kupata fedha zaidi na kumfanya kuwa tajiri mkubwa baadaye. Alihakikisha familia yake ikipata kila kitu, hakutaka kuiona ikiteseka au ikipata matatizo yoyote yale.
Maisha yaliendelea, mwaka wa kwanza ukapita, wa pili ukaingia na ndipo mawazo juu ya huyo kijana yalipoanza kurudi tena kichwani mwake. Hakujua ni kwa sababu gani lakini kila siku alipokuwa akikaa ofisini mwake, kitu cha kwanza kilikuwa ni kumfikiria kijana huyo, mawazo juu yake yaliendelea kumtesa kila siku.
“Huyo kijana yupo wapi?” aliuliza Bwana James.
“Catherine alisema yupo Boston...”
“Ninataka kuonana naye, mawazo juu yake yamekuwa yakinitesa sana, au hata picha zake unazo?” aliuliza Bwana James.
“Hapana, ila nina uhakika Catherine anazo...”
“Hebu mpigie simu...”
Bi Claire akafanya kama alivyoambiwa, akampigia simu binti yake lakini haikuweza kupatikana zaidi ya kuambiwa aache ujumbe mfupi wa maneno. Hakuacha ujumbe wowote ule, akaikata simu kwa lengo la kujaribu hapo baadaye.
Baada ya kupita saa mbili, binti yao, Catherine akarudi nyumbani hapo. Kwanza kila mmoja alishangaa, muda huo alitakiwa kuwa chuoni, wakati wanajiuliza hilo, wakagundua kwamba binti yao hakuwa sawa kabisa, alionekana kuwa na mawazo tele, tena hata macho yake yaliwatisha, yalikuwa mekundu hali iliyoonyesha kwamba muda mchache uliopita alikuwa akilia.
“Kuna nini?” aliuliza mama yake. Catherine hakujibu zaidi ya kuelekea chumbani kwake.
Wakahisi kulikuwa na tatizo, alichokifanya bi Claire ni kumfuata binti yake, alitaka kufahamu ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea mpaka kumrudisha nyumbani tena huku akionekana kuwa na huzuni.
“Moyo unaniuma mama...” alisema Catherine huku akiyafuta machozi yake.
“Kuna nini?”
Mama yake alikuwa kila kitu katika maisha yake, alimchukulia kama rafiki yake wa karibu na kila kitu kilichomsumbua, hakumficha, alimwambia ukweli.
Alichokifanya Catherine ni kumwambia mama yake kila kitu kilichokuwa kikiendelea moyoni mwake, alimwambia ukweli kwamba alimpenda sana Dylan tangu siku ya kwanza alipokutana naye, akajitahidi kuwa naye karibu na hatimaye kutamani kuwa mpenzi wake.
“Sasa kipi kinakuliza?” aliuliza mama yake.
“Amenikataa, amesema hataki kuwa mpenzi wangu,” alijibu Catherine huku akilia kama mtoto.
Mama yake akawa na jukumu kubwa la kumbembeleza binti yake. Alimuonea huruma, alikuwa binti yake wa kwanza hivyo kumuona akilia huku akiteseka moyoni mwake, hakika ilimuuma mno.
“Nyamaza, baba yako atakusaidia...” alisema bi Claire kwa sauti ya chini.
“Baba atanisaidia?”
“Ndiyo! Anataka kwenda kuonana naye, nitamwambia kuhusu hilo pia, atakusaidia,” alisema bi Claire huku akimfariji binti yake.
Alichokifanya mwanamke huyo ni kuelekea sebuleni ambapo akamkuta mume wake akiwa ametulia kochini huku akionekana kuwa na mawazo lukuki. Kwa mwendo wa taratibu akamsogelea na kuanza kuzungumza naye.
“Kuna nini?” aliuliza Bwana James.
“Catherine analia...”
“Kisa?”
Bi Claire hakuwa na jinsi, alichokifanya ni kuanza kumuhadithia mume wake kile alichoambiwa na binti yake kule chumbani. Bwana James alihuzunika, katika maisha yake hakutaka kabisa kuona binti yake akilia, hivyo kitendo cha kusikia kwamba binti yake alilia kisa tu kukataliwa na huyo Dylan, ilimuuma mno.
“Tuna fedha, unalijua hilo?” aliamua kumuuliza mke wake.
“Ndiyo!”
“Kama tuna fedha, kipi kinashindikana? Kununua mapenzi?” aliuliza mzee huyo.
“Hakuna kinachoshindikana!”
“Basi ni lazima tukutane na huyo Dylan haraka iwezekanavyo, sipendi kumuona binti yangu akiwa na huzuni, sipendi kumuona akilia,” alisema Bwana James.
Huo ndiyo ulikuwa ukweli, alimpenda mno binti yake mkubwa hata zaidi ya alivyompenda binti yake mdogo, Laura. Kwake, msichana huyo alikuwa kila kitu kitendo cha kuambiwa kwamba alikuwa akilia kisa tu kulikuwa na mwanaume alimkataa, ilimchanganya akili yake.
Aliamini katika fedha kwamba unapokuwa na fedha hakuna kitu chochote kile kinachoshindikana hivyo kama huyo Dylan amekataa kuwa na binti yake, aliamini kama angetumia fedha basi ingekuwa rahisi kwake kumpata na kumuingiza katika mikono ya binti yake.
“Mwambie tunamfuata, tutazungumza naye,” alisema Bwana James huku akionekana kumaanisha alichokisema.
Catherine alipopewa taarifa juu ya kile alichoambiwa, kidogo moyo wake ulikuwa na ahueni kwani hata yeye aliamini kwamba fedha zingeweza kubadilisha kitu chochote kile.
Wakapanga siku ya safari, haikuwa wiki hiyo ila ingefanyika wiki mbiliz zinazofuata. Katika kipindi chote cha kusubiria hiyo safari, bado Catherine alikuwa akiwasiliana na Dylan huku akimsisitiza awe mpenzi wake lakini mwanaume huyo alikataa kwa kusema kwamba alikuwa na sababu yake kubwa, ila ya pili, hakutaka kumuona msichana huyo akiwa kwenye majonzi makubwa.
Siku zikaendelea kukatika, baada ya wiki moja, hapo ndipo familia hiyo ikapanda ndege binafsi na kuelekea Boston. Njiani, walikuwa wakizungumza lakini kichwa cha Catherine kilikuwa na mawazo tele, hakuamini kama kweli Dylan angeweza kukubaliana naye na hatimaye kuwa na uhusiano wa kimapenzi.
Wazazi wake waliendelea kumfariji kwa kumwambia kwamba kila kitu kingewezekana kwani fedha ndicho kitu kilichokuwa na mafanikio makubwa kama tu kingetumika kama kinavyotakiwa.
Walichukua saa mbili, ndege ikatua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Boston ambapo wakateremka na kuanza kwenda hotelini huku wakiwa wamepokelewa kwa magari maalumu, ya kifahari ambayo hayakuwa na uwezo wa kupenyeza risasi.
Bwana James alikuwa bilionea mkubwa, kila alipopita, alinukia fedha, alikuwa mtu anayelindwa sana nchini Marekani kiasi kwamba hata wabaya wake kumpata ilikuwa kazi kubwa.
Baada ya kufika katika hoteli ambayo waliweka oda kwa kuchukua hoteli nzima, wakatulia vyumbani mwao. Japokuwa kwa upande wa Bwana James alionekana kama kupoteza muda, ila alifanya hivyo kama njia mojawapo ya kumfanya binti yake awe na furaha maishani mwake, hakutaka kumuona akilia au akiteseka maishani mwake, kwa kifupi, hakutaka kumuona binti yake huyo akilia kwa uchungu.
Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumamosi.
Madame Karim kaunganishwa uko na kinondoni sweetheart unakumbuka tulihisigi ni yeyeKaribu mamii
Karibu mamii