Mgambilwa ni mntu
JF-Expert Member
- May 30, 2017
- 2,869
- 3,188
Tanzania ni mojawapo wa nchi chache duniani zenye utajiri mkubwa wa wanyama wa mwituni na ndiyo maana maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya Hifadhi za Taifa (National Parks); Mbuga za Wanyama (Game Reserve) na Hifadhi za Misitu nchini ni wastani wa theluthi (1/3) ya ukubwa Nchi nzima. Ikiwa na km za mraba 945,000 Tanzania ni ya 12 kwa ukubwa wa eneo na ya 5 kwa watu barani Afrika.
Ukitoa Mbuga ya Selous (1920), Hifadhi na Mbuga zote nchini zilianzishwa baada ya mwaka 1951 kwa kuanzia na Serengeti, Mkomazi na Rungwa (1951). Zoezi la kuanzisha ama kupandisha maeneo yaliyotengwa limeendelea hadi miaka ya 1990 na mpaka miaka ya 2000s (Hifadhi ya Saanane). Uanzishwaji wa mbuga hizo ukiacha maeneo machache haukuhusu kuhamisha watu Bali maeneo hayo hayakuwa yamekaliwa na watu.
Kumbuka kipindi cha kuelekea uhuru wakati Hifadhi zinaanza kuanzishwa, Tanganyika ili kuwa na wakazi wapatao milioni 8 lakini ukirudi nyuma kipindi cha wajerumani (1910s) idadi ya watanganyika ilkuwa ni milioni 5 pekee. Linganisha Idadi hiyo ndogo na nchi za Rwanda yenye km za mraba 26,000 (watu milioni 2) na Burundi km za mraba 24,000 (watu millions 1.5) kwa kipindi hicho.
Licha ya kwamba watu wameongezeka sana nchini na kuwa nchi ya 5 Afrika kutoka ya 9 miaka ya 1970s, hiyo inaonyesha kuwa eneo kubwa la nchi limekuwa na mvua chache ama magonjwa ya yellow fever na mbung'o kiasi cha kutokaliwa na watu wengi. Mfano mzuri ni Pori kubwa la Selous na la Mikoa ya Tabora na Katavi.
Hivyo tukijivunia Mbuga zeta za wanyama tukumbuke kuwa ni maeneo yaliyoachwa kwa kutofaa kwa makazi na shughuli za kilimo.
Ukitoa Mbuga ya Selous (1920), Hifadhi na Mbuga zote nchini zilianzishwa baada ya mwaka 1951 kwa kuanzia na Serengeti, Mkomazi na Rungwa (1951). Zoezi la kuanzisha ama kupandisha maeneo yaliyotengwa limeendelea hadi miaka ya 1990 na mpaka miaka ya 2000s (Hifadhi ya Saanane). Uanzishwaji wa mbuga hizo ukiacha maeneo machache haukuhusu kuhamisha watu Bali maeneo hayo hayakuwa yamekaliwa na watu.
Kumbuka kipindi cha kuelekea uhuru wakati Hifadhi zinaanza kuanzishwa, Tanganyika ili kuwa na wakazi wapatao milioni 8 lakini ukirudi nyuma kipindi cha wajerumani (1910s) idadi ya watanganyika ilkuwa ni milioni 5 pekee. Linganisha Idadi hiyo ndogo na nchi za Rwanda yenye km za mraba 26,000 (watu milioni 2) na Burundi km za mraba 24,000 (watu millions 1.5) kwa kipindi hicho.
Licha ya kwamba watu wameongezeka sana nchini na kuwa nchi ya 5 Afrika kutoka ya 9 miaka ya 1970s, hiyo inaonyesha kuwa eneo kubwa la nchi limekuwa na mvua chache ama magonjwa ya yellow fever na mbung'o kiasi cha kutokaliwa na watu wengi. Mfano mzuri ni Pori kubwa la Selous na la Mikoa ya Tabora na Katavi.
Hivyo tukijivunia Mbuga zeta za wanyama tukumbuke kuwa ni maeneo yaliyoachwa kwa kutofaa kwa makazi na shughuli za kilimo.