Utajiri wa DiamondPlatnumz Wafikia Bilioni 18

Traveller X

JF-Expert Member
May 2, 2017
271
305

Inasemekana hii imetokana na mafanikio yake kwenye biashara zake mbali na muziki ambapo ameingiza mkwanja mrefu sana kwenye DiamondKaranga,ChibuPafyum,Ubalozi wake kwenye kampuni kubwa kama Vodacom na nyingine kibao,

Mpaka june 2016 Diamond alikua na utajiri upatao USD 4 Million sawa na bilioni 8 za kitanzania lakini mpaka kufikia august mwaka 2017 utajiri wake umeongezeka mara mbili.

Diamond kwasasa ndiye msanii tajiri zaidi afrika mashariki akishika nafasi ya Jose Chameleon ambae kwasasa inasemekana ni choka mbaya:

Bado nafatilia kujua Alikiba atakua na utajiri wa kiasi gani mpaka sasa.
 
Unakuwa msanii mkubwa afuu njaa kalii..acha kuimba tu

Utu wa mtu ni kazi, pesa ni matokeo.

Kuna watu wanakuwa matajiri kwa sababu wamecheza bahati NASIBU wakashinda.Hawajui kazi yoyote.

Utawasifia kwamba wanajua kazi kuliko watu waliojikita kufanya kazi kila siku?

Kuna wengine usanii wao wakishiba wanakosa feeling, mpaka wawe na njaa ndiyo wanapata feeling ya kuimba vizuri.

Sasa msanii kama huyo ukimlaumu kwa sababu ana njaa kali, unakuwa hujaelewa sanaa yake.

Mzee Morris Nyunyusa kafa na njaa kali kwa standard za utajiri wa Diamond Platnumz mnaousema.

Lakini je, unaweza kusema Diamond Platnumz ni msanii mahiri kuliko Mzee Morris Nyunyusa?
 


Inasemekana hii imetokana na mafanikio yake kwenye biashara zake mbali na muziki ambapo ameingiza mkwanja mrefu sana kwenye DiamondKaranga,ChibuPafyum,Ubalozi wake kwenye kampuni kubwa kama Vodacom na nyingine kibao,

Mpaka june 2016 Diamond alikua na utajiri upatao USD 4 Million sawa na bilioni 8 za kitanzania lakini mpaka kufikia august mwaka 2017 utajiri wake umeongezeka mara mbili.

Diamond kwasasa ndiye msanii tajiri zaidi afrika mashariki akishika nafasi ya Jose Chameleon ambae kwasasa inasemekana ni choka mbaya:

Bado nafatilia kujua Alikiba atakua na utajiri wa kiasi gani mpaka sasa.

Unaanzaje kufuatilia habari nyingine wakati hii yenyewe umeishia kwenye Inasemekana? Thibitisha kwanza hii ndiyo urukie kwingine.
Wewe vipi wewe ebwoo!! Unadhani hayo mafanikio huwa yanakuja kuja tu!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom