Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,272
Ninaomba tujadili hii mada, maana halisi ya utajiri ni nini? Pesa na mali vinaweza kukupa furaha duniani? Kuna raha gani ya kuwa tajiri ilhali umezungukwa na masikini katika nchi, mji mtaa hata kijiji unachoishi?
Watafiti wa uchumi wanasema 5% ya wakazi wa dunia hii ndiyo wanaomiliki utajiri wa dunia hii. Utajiri huu ungegawanywa sawa kwa kila binadamu wote tungeweza kuondoa umasikini wa kutupwa (absolute poverty).
Duniani tunaishi na tunakufa, kuna faida gani ya kuua, kufanya makafara au kuiba ili uwe tajiri. Uwe tajiri ili iweje?
Kwa maoni yangu ninadhani kitu cha muhimu ni kupambana ili kupata mahitaji ya lazima. Nyumba, chakula, matibabu, elimu, dini, nguo na familia.
Watu wengi hawafahamu hili kuwa unaweza kuwa tajiri lakini kama huna familia utajiri wako hauna maana. Ni mara chache mno watoto wako kukuibia mpaka ufilisike. Hata hivyo, utakapo kosa mtu wa kuongea nae uzeeni utajiri wako utakuaaidia nini?
Watafiti wa uchumi wanasema 5% ya wakazi wa dunia hii ndiyo wanaomiliki utajiri wa dunia hii. Utajiri huu ungegawanywa sawa kwa kila binadamu wote tungeweza kuondoa umasikini wa kutupwa (absolute poverty).
Duniani tunaishi na tunakufa, kuna faida gani ya kuua, kufanya makafara au kuiba ili uwe tajiri. Uwe tajiri ili iweje?
Kwa maoni yangu ninadhani kitu cha muhimu ni kupambana ili kupata mahitaji ya lazima. Nyumba, chakula, matibabu, elimu, dini, nguo na familia.
Watu wengi hawafahamu hili kuwa unaweza kuwa tajiri lakini kama huna familia utajiri wako hauna maana. Ni mara chache mno watoto wako kukuibia mpaka ufilisike. Hata hivyo, utakapo kosa mtu wa kuongea nae uzeeni utajiri wako utakuaaidia nini?