Utajiri kutoka JamiiForums

Njanga Tz

JF-Expert Member
Mar 19, 2015
843
653
Toka niwe member hapa sijawahi fikiria siku moja nitakuja kukutana na mawazo mbadala ya kubadilisha status ya uchumi wangu hapa. Nilikuwa shabiki namba moja wa jukwaa la SIASA,kimsingi sio dhambi kushabikia jukwaa hilo lakini dhambi ni pale unaposhabikia halaf huingizi kitu.

Kuna siku moja nikakaa nikatulia kusoma jukwaa hili la Biashara, Uchumi na Ujasiriamali, MAKENIKIA niliyoyaokota hapo yamenifanya nisirudi tena kusoma jukwaa la SIASA.

Nilipitia mabandiko kibao hapa, lakini nilivuitwa sana na mijadala kuhusu biashara ya nafaka, na kwa kupitia IDEA za hapa nilichukua hatua za kuanzisha biashara hiyo kama ifuatavyo;

Nilitumia mtaji wa milioni tatu tu. Nilitafuta fremu niliyolipia laki moja kwa mwezi, nikailipia miezi sita yaani laki saba pamoja na udalali. Nikabakiwa na milioni mbili na laki tatu. Nikatumia hiyo pesa kununua mzigo wa kuanzia biashara, nikanunua Mchele, Maharage, Unga na Mafuta ya Alizeti ya Singida.

Siku ya kwanza ya biashara niliuza laki moja na ishirini lakini toka hapo kwa wastani nauza laki tatu na nusu kwa siku na hivyo kwa wiki nauza wastani wa milioni 2.4M na kwa mwezi ni milioni 9.6.

Hii biashara nilifanya kama kutest nikaweka mtaji mdogo lakini nmegundua ukitaka kuendelea ondoa uwoga. Kwa hii miezi mitatu niliyofanya hii biashara faida ninayoipata kwa kila mwezi baada ya kuondoa takataka zote inakaribia mara mbili na nusu ya mshahara wangu kwa mwezi(Mshahara wa serikali TGSE).

NB: Ubunifu unahusika; kupaki vizuri, usafi na mrembo wa kuchangamkia wateja.

Tuamke utajiri uko mikononi mwetu.
 
Nilitafuta fremu niliyolipia laki moja kwa mwezi, nikailipia miezi sita yaani laki saba pamoja na udalali huko Tabata.Nikabakiwa na milioni mbili na laki tatu.Nikatumia hiyo pesa kununua mzigo wa kuanzia biashara, nikanunua Mchele,Maharage,Unga na Mafuta ya Alizeti ya Singida.Siku ya kwanza ya biashara niliuza laki moja na ishirini lakini toka hapo kwa wastani nauza laki tatu na nusu kwa siku na hivyo kwa wiki nauza wastani wa milioni 2.4M na kwa mwezi ni milioni 9.6.Hii biashara nilifanya kama kutest nikaweka mtaji mdogo lakini nmegundua ukitaka kuendelea ondoa uwoga. Kwa hii miezi mitatu niliyofanya hii biashara faida ninayoipta kwa kila mwezi baada yakuondoa takataka zote inakaribia mara mbili na nusu ya mshahara wangu kwa mwezi(Mshahara wa serikali TGSE ).
Nimejifunza kitu kwenye hili bandiko lako

Viva Viva! JamiiForums
 
Hapo kwenye "mrembo wa kuchangamkia wateja" bajeti yake ya malipo ipo kwenye hayo unayoita "matakataka"??

Badilisha mindset yako mkuu. Sio uungwana hata kidogo kumdharau mtu anayefanya biashara yako ishamiri.
 
Nimejifunza kitu kwenye hili bandiko lako

Long live! JamiiForums
Mkuu nashukuru kama umejifunza, mimi sijawahi andika wala kucoment chochote kwenye hili jukwaa la Biashara ila nikafanyia kazi ideas za hapa. Believe me mkuu baada ya mwaka nitaleta ushahidi mwingine hapa.Mimi nashangaaga sana kwann wachaga wanakomaa na maduka hapa mjini? Kumbe kuna siri nzito sana, Hapo mkuu sijaloga wala kutoa kafara mtu,je nikiroga na kutoa kafara?JOKES
 
Hapo kwenye "mrembo wa kuchangamkia wateja" bajeti yake ya malipo ipo kwenye hayo unayoita "matakataka"??

Badilisha mindset yako mkuu. Sio uungwana hata kidogo kumdharau mtu anayefanya biashara yako ishamiri.
Mkuu mm sijadharau hata ukienda tigo au voda pale si tunakutana na wadada wanaochangamkia wateja vizuri? sijamaanisha unavyofikiri wewe.
 
Hapo mkuu sijaloga wala kutoa kafara mtu,je nikiroga na kutoa kafara?
Hapo ndipo inajidhhirisha kuwa uthubutu ndio siri ya mafanikio.

Wanao kosa huu uthubutu huisha kusema "jamaa ameloga, Jamaa siku hizi freemason" sijui.

Hongera mkuu kwa uthubutu, kila kitu kinawezekana chibi ya jua.
 
Mkuu nashukuru kama umejifunza, mimi sijawahi andika wala kucoment chochote kwenye hili jukwaa la Biashara ila nikafanyia kazi ideas za hapa. Believe me mkuu baada ya mwaka nitaleta ushahidi mwingine hapa.Mimi nashangaaga sana kwann wachaga wanakomaa na maduka hapa mjini? Kumbe kuna siri nzito sana, Hapo mkuu sijaloga wala kutoa kafara mtu,je nikiroga na kutoa kafara?JOKES
Duuh!. Mkuu, una wazo lolote la kwenda kutoa kafara na kuloga? Basi liondoe, utaishi maisha ya wasiwasi na pasipo raha. Endelezea harakati zako vema, Mungu atakagusa.
 
Safi sana mkuu. Piga kazi endelea kupaa na kuongezeka. Asante kwa mrejesho wa kutia moyo sana.
 
Duuh!. Mkuu, una wazo lolote la kwenda kutoa kafara na kuloga? Basi liondoe, utaishi maisha ya wasiwasi na pasipo raha. Endelezea harakati zako vema, Mungu atakagusa.
Mkuu nmemalizia na neno JOKES, Sina imani hiyo
 
Vizuri mkuu. Umetupa moyo sisi wengine tunaopitia nyuzi za biashara halafu tunaogopa kujaribu. Umeongelea suala la kupack vizuri, Je unapack kwenye mifuko ya plastic hii transparent au packaging yake ikoje? Na una pack kilo ngapi ngapi?
Na vipi kuhusu kupima kwa mizani kutokana na matakwa ya mteja? Samahani kwa maswali mengi
 
Nmependa San mkuu, ngoja na Mimi nipitie jukwaa hilo
Pitia utakutana na watu wenye mawazo mazuri, ukitaka kuanzisha biashara angalia location nzuri tafuta na mtu hata mmoja mwenye experience akupe ABC.Mimi nilitumia muda wangu wa ziada kutafuta location na rafiki yangu alinikutanisha na mama mmoja mwenye experience ya kutosha. Naweza sema nimefaulu asilimia 75
 
Vizuri mkuu. Umetupa moyo sisi wengine tunaopitia nyuzi za biashara halafu tunaogopa kujaribu. Umeongelea suala la kupack vizuri, Je unapack kwenye mifuko ya plastic hii transparent au packaging yake ikoje? Na una pack kilo ngapi ngapi?
Na vipi kuhusu kupima kwa mizani kutokana na matakwa ya mteja? Samahani kwa maswali mengi
Asante mkuu. Mifuko natumia ya plastic transparent ya kilo 5 inauzwa Tandika na Kariakoo.Napaki maharage mchele sukari. Pia nilinunua mizani pale kariakoo shimoni laki moja na 35, napima kidogo kidogo. mwezi huu mtukufu kuna tambi pia za kiupima. Hilo ni muhimu kutokana na hali zetu za kiuchumi tunahitaji nusu kilo,robo kuendeleza maisha.
 
Asante mkuu. Mifuko natumia ya plastic transparent ya kilo 5 inauzwa Tandika na Kariakoo.Napaki maharage mchele sukari. Pia nilinunua mizani pale kariakoo shimoni laki moja na 35, napima kidogo kidogo. mwezi huu mtukufu kuna tambi pia za kiupima. Hilo ni muhimu kutokana na hali zetu za kiuchumi tunahitaji nusu kilo,robo kuendeleza maisha.
Asante sana.
 
Back
Top Bottom