Utafiti waonesha kuwa mikopo toka China kwa nchi za Afrika ina gharama za chini kuliko ile ya nchi za Magharibi

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,008
1,032
1684826137090.png

Watafiti katika taasisi ya Uchumi wa Dunia ya Kiel ya Ujerumani, wamefanya utafiti na kufikia hitimisho kuwa mikopo inayotolewa na China kwa nchi za Afrika ni ya gharama nafuu kuliko ile inayotolewa na nchi za magharibi, au inayotolewa na wakopeshaji wa kibiashara. Hitimisho hilo limefikiwa wakati baadhi ya wanasiasa wa nchi za magharibi wanaendelea kutumia mikopo inayotolewa na China kwa nchi za Afrika kama njia ya kuichafua China.

Kwa muda mrefu sasa ukosefu wa fedha umekuwa ni kikwazo kikubwa kwa nchi za Afrika kugharamia miradi yake ya maendeleo. Kuibuka kiuchumi kwa China, kumekuwa ni jibu zuri la kukabiliana na kikwazo hicho na China imekuwa ni chanzo mbadala kwa nchi za Afrika ambazo zimekuwa zikipata changamoto kubwa ya kupata mikopo kutoka kwa nchi za magharibi, ambazo mikopo yake imekuwa na riba kubwa na masharti mengi magumu.

China kuwa chanzo mbadala cha mikopo kwa nchi za Afrika, hakuzifurahishi nchi za magharibi, ambazo zinaona vyanzo vya mapato yake yanayotokana na kuzikopesha fedha nchi za Afrika kwa riba kubwa vinatoweka. Ndio maana tumekuwa tunasikia mara kwa mara kauli ya “mtego wa madeni”, ambayo hadi sasa hakuna aliyewahi kuthibitisha kuwa kauli hiyo ina mashiko.

Watafiti mashuhuri kuhusu maswala ya madeni ya Afrika wa taasisi ya Kiel ya Ujerumani Bw. David Mihalyi na Christoph Trebesch, wameeleza wazi kuwa ikilinganishwa na wakopeshaji binafsi ambao wengi ni wa nchi za magharibi, riba ya mikopo ya China ni asilimia 2 na 3.2, wakati ile ya wakopeshaji binafsi ni kati ya asilimia 6.2 na 6.4. Ni wazi kabisa kuwa riba hizo zinaonesha ni nani kati ya wakopeshaji hawa wawili anayemtwisha mzigo wa deni mkopaji.

Watafiti hao pia wamefikia hatua ya kuyatetea mashirika ya fedha ya kimataifa, yaani Benki ya Dunia na IMF, kwamba yanatoa riba ndogo kuliko China, yaani kati ya asilimia 0.8 na 1.0. Kwa kuangalia kijuu juu ni kuwa riba za mikopo ya mashirika ya fedha ya kimataifa ziko chini, ikilinganishwa na za China. Lakini kitu ambacho watafiti hao hawaweki wazi, ni mlolongo wa masharti ya kiuchumi, kijamii na kisiasa yanayoambatana na mikopo hiyo yenye riba nafuu. Kuna wakati baadhi ya wanasiasa wa nchi za magharibi walifikia hatua ya kusema msimamo wa nchi za Afrika kuhusu mapenzi ya jinsia moja, itakuwa ni sharti la kupewa misaada kutoka kwa nchi za magharibi.

Watafiti hao pia hawajazungumzia muda mrefu unaotumika kutoka kipindi cha kuomba mkopo hadi mkopo unapotolewa. Kuna wakati mikopo inaombwa ili kukabiliana na dharura mbalimbali, lakini kuanzia kipindi cha kuomba mkopo hadi kutolewa kwa mikopo hiyo, hali ya muombaji inakuwa mbaya kiasi kwamba hata mkopo wenyewe unakuwa haifanyi kazi ya kile ulichoombewa.

Nchi nyingi za Afrika zinatambua kuwa mikopo ya China ni ya haraka, yenye ufanisi na haina masharti ya ajabu kama yanayotolewa na baadhi ya nchi za magharibi. Hivi ndivyo vinafanya mikopo ya China iwe na mvuto kwa nchi nyingi za Afrika.

Hata hivyo ni vizuri ikikumbukwa kuwa licha ya kelele zote zinazoendelea kuhusu suala la madeni barani Afrika, Benki ya Dunia ndio mkopeshaji mkuu kwa nchi za Afrika. Ni kweli kuwa China ni mkopesha mkuu kama nchi, lakini undani kuhusu deni la Afrika unaonesha kuwa changamoto kubwa kuhusu deni bado iko kwenye nchi za magharibi.
 

Watafiti katika taasisi ya Uchumi wa Dunia ya Kiel ya Ujerumani, wamefanya utafiti na kufikia hitimisho kuwa mikopo inayotolewa na China kwa nchi za Afrika ni ya gharama nafuu kuliko ile inayotolewa na nchi za magharibi, au inayotolewa na wakopeshaji wa kibiashara. Hitimisho hilo limefikiwa wakati baadhi ya wanasiasa wa nchi za magharibi wanaendelea kutumia mikopo inayotolewa na China kwa nchi za Afrika kama njia ya kuichafua China.

Kwa muda mrefu sasa ukosefu wa fedha umekuwa ni kikwazo kikubwa kwa nchi za Afrika kugharamia miradi yake ya maendeleo. Kuibuka kiuchumi kwa China, kumekuwa ni jibu zuri la kukabiliana na kikwazo hicho na China imekuwa ni chanzo mbadala kwa nchi za Afrika ambazo zimekuwa zikipata changamoto kubwa ya kupata mikopo kutoka kwa nchi za magharibi, ambazo mikopo yake imekuwa na riba kubwa na masharti mengi magumu.

China kuwa chanzo mbadala cha mikopo kwa nchi za Afrika, hakuzifurahishi nchi za magharibi, ambazo zinaona vyanzo vya mapato yake yanayotokana na kuzikopesha fedha nchi za Afrika kwa riba kubwa vinatoweka. Ndio maana tumekuwa tunasikia mara kwa mara kauli ya “mtego wa madeni”, ambayo hadi sasa hakuna aliyewahi kuthibitisha kuwa kauli hiyo ina mashiko.

Watafiti mashuhuri kuhusu maswala ya madeni ya Afrika wa taasisi ya Kiel ya Ujerumani Bw. David Mihalyi na Christoph Trebesch, wameeleza wazi kuwa ikilinganishwa na wakopeshaji binafsi ambao wengi ni wa nchi za magharibi, riba ya mikopo ya China ni asilimia 2 na 3.2, wakati ile ya wakopeshaji binafsi ni kati ya asilimia 6.2 na 6.4. Ni wazi kabisa kuwa riba hizo zinaonesha ni nani kati ya wakopeshaji hawa wawili anayemtwisha mzigo wa deni mkopaji.

Watafiti hao pia wamefikia hatua ya kuyatetea mashirika ya fedha ya kimataifa, yaani Benki ya Dunia na IMF, kwamba yanatoa riba ndogo kuliko China, yaani kati ya asilimia 0.8 na 1.0. Kwa kuangalia kijuu juu ni kuwa riba za mikopo ya mashirika ya fedha ya kimataifa ziko chini, ikilinganishwa na za China. Lakini kitu ambacho watafiti hao hawaweki wazi, ni mlolongo wa masharti ya kiuchumi, kijamii na kisiasa yanayoambatana na mikopo hiyo yenye riba nafuu. Kuna wakati baadhi ya wanasiasa wa nchi za magharibi walifikia hatua ya kusema msimamo wa nchi za Afrika kuhusu mapenzi ya jinsia moja, itakuwa ni sharti la kupewa misaada kutoka kwa nchi za magharibi.

Watafiti hao pia hawajazungumzia muda mrefu unaotumika kutoka kipindi cha kuomba mkopo hadi mkopo unapotolewa. Kuna wakati mikopo inaombwa ili kukabiliana na dharura mbalimbali, lakini kuanzia kipindi cha kuomba mkopo hadi kutolewa kwa mikopo hiyo, hali ya muombaji inakuwa mbaya kiasi kwamba hata mkopo wenyewe unakuwa haifanyi kazi ya kile ulichoombewa.

Nchi nyingi za Afrika zinatambua kuwa mikopo ya China ni ya haraka, yenye ufanisi na haina masharti ya ajabu kama yanayotolewa na baadhi ya nchi za magharibi. Hivi ndivyo vinafanya mikopo ya China iwe na mvuto kwa nchi nyingi za Afrika.

Hata hivyo ni vizuri ikikumbukwa kuwa licha ya kelele zote zinazoendelea kuhusu suala la madeni barani Afrika, Benki ya Dunia ndio mkopeshaji mkuu kwa nchi za Afrika. Ni kweli kuwa China ni mkopesha mkuu kama nchi, lakini undani kuhusu deni la Afrika unaonesha kuwa changamoto kubwa kuhusu deni bado iko kwenye nchi za magharibi.
We mchina tafiti hizo ziko wapi?
 
Back
Top Bottom